Mwanzo

WikiShia
Ensaiklopidia ya Maktaba Ahlul Bayt (a.s.), inayosimamiwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s.)
645 Makala / mabadiliko 13,390 kwa Kiswahili

Makala ya Wiki

Tukio la Karbala au Tukio la Ashura (Kiarabu: واقعة کربلا أو واقعة عاشوراء) ni tukio la vita vya jeshi la Kufa dhidi ya Imamu Hussein (a.s) na masahaba zake huko Karbala,. Tukio la Karbala lilitokea tarehe 10 Muharram (Mfunguo nne) mwaka 61 Hijiria, baada ya Imamu Hussein (a.s) kukataa kutoa kiapo cha utiifu cha kutawazishwa Yazid bin Muawiah kushika nafasi ya Ukhalifa. Jambo hilo ndilo lililopelekea kuuawa kishahidi Imamu na masahaba zake, kisha kutekwa kwa familia yake baada ya vita hivyo.

Kadhia ya Karbala linachukuliwa kuwa ni tukio la kuhuzunisha zaidi katika historia ya Uislamu. Kulingana na umuhimu wa tukio hilo, Mashia huadhimisha maombolezo makubwa zaidi kuliko mengine yote katika kumbukumbu ya kila mwaka ya tukio hilo adhimu.

Read more ...

Other featured articles: Al-IstisqaaMaimamu wa KishiaAbd al-Nabi al-Jazairi


Je, wajua ...
  • ... Kifo cha Fatima Zahra, binti ya Mtume (s.a.w.w) ni miongoni mwa vifo vilivyo na utata zaidi katika Uislamu na hata kaburi lake halijulikani lilipo?
  • ... Kitendo cha kusengenya kimefananishwa na mtu kula nyama ya nduguye aliyekufa?
  • ... Ramadhani, ndio mwezi pekee jina lake limekuja katika Qur'an?
  • ... Aya ya 7 ya Surat al-Bayyinah ni miongoni mwa Aya ambazo zilizoteremka kuelezea fadhila na ubora wa Ali bin Abi Talib (a.s)?
  • ... Shia ndio madhehebu inayoamini na kuitikadi kuwa Khalifa au Kiongozi baada ya Mtume (s.a.w.w) anapaswa kuchaguliwa na M.mungu kisha kuainishwa na Mtume?
Makala Zilizo Pendekezwa


  • Jeshi la Omar bin Sa’d « Ni jeshi lililokuwa limekusanywa na Omar bin Sa’d kwa amri ya Ubaidullah ibn Ziyad na katika siku ya Ashura lilipigana na Imamu Hussein (a.s) na maswahaba zake katika jangwa la Karbala, Iraq na kuwaua shahidi; kisha likawachukua mateka watu wa nyumba ya Imam Hussein (a.s).»
  • Mukhtar ibnu Abi Ubaid al-Thaqafi «Ni miongoni mwa tabiina (waliokutana na masahaba wa Mtume) ambaye alianzisha harakati na mapinduzi kwa ajili ya kulipiza kisasi cha damu ya Imamu Hussein (a.s). Katika tukio la Karbala, Mukhtari alikuwa na jukumu la kuwa mwenyeji wa Muslim bin Aqil, mjumbe wa Imamu Hussein (a.s) katika mji wa Kufa na alishirikiana naye mpaka alipouawa shahidi, kisha Ubaydullah bin Ziyad akamtia jela. Kwa msingi huo, hakuweko katika tukio la siku ya Ashura huko Karbala.»
  • Harakati za Imamu Hussein (a.s) «Ni harakati za Imamu Hussein (a.s) dhidi ya utawala wa Yazid bin Muawiya ili kuonesha upinzani wake dhidi ya utawala huo. Harakati hizi ndizo zilisababisha kuuawa kwake shahidi pamoja na wafuasi wake mnamo tarehe 10 Muharram mwaka wa 61 Hijiria, na kuishia kutekwa wa familia yake ndani ya tukio hilo. Harakati hizi zilianza kwa kukataa Imam Hussein (a.s) kutoa kiapo cha utiifu cha kumtambua Yazid mbele ya gavana wa Madina ambaye ni mwakilishi wa Yazid. Jambo hili lilifungua ukurasa mpya wa tarehe ambapo Imamu Hussein (a.s) aliondoka Madina mnamo Rajab mwaka wa 60 Hijiria yeye na familia yake, na hatima ya safari hii ilimalizika kwa kurudi kwa mateka mjini Madina.»
  • Imamu Hussein (a.s) «Alizaliwa mwaka wa 4 Hijiria na kufariki mwaka wa 61 Hijiria. Hussein bin Ali bin Abi Talib (a.s) kwa upande wa madhehebu ya Kishia anatambuliwa kiumaarufu kama: Imamu Hussein (a.s). Lakabu mbili maarufu ni; Aba Abdullah na Sayyid Al-Shuhadaa. Hussein bin Ali (a.s) ni Imamu wa tatu miongoni mwa Maimamu wa Kishia. Aliuawa kishahidi katika tukio la Ashura katika ardhi ya Karbala. Yeye ni mtoto wa pili wa Imam Ali na bibi Fatima Al-Zahraa (a.s) na ni mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w).»
  • Abbas bin Ali bin Abi Talib (a.s) «Alizaliwa mwaka wa 26 na kufariki mwaka wa 61 Hijiria, na ni maarufu kwa jina la Abul-Fadhl, naye ni mtoto wa tano wa Imamu Ali (a.s) na mtoto wa kwanza wa Ummul Banina. Sehemu muhimu zaidi ya maisha yake ni kuwepo kwake katika tukio la Karbala na kuuawa kwake kishahidi siku ya Ashura.»
  • Akhera «Ni ulimwengu baada ya kifo na mauti na ni ulimwengu ujao baada ya maisha ya dunia.»
  • Ulul-amri «Ina maana ya wenye mamlaka, na hao wenye mamlaka ni watu ambao ni wajibu kuwatii kwa msingi wa Aya ya Ulul-Amr. Istilahi hii imekuja na kuelezwa ndani ya aya ya 59 ya surat al-Nisaa.»
  • Kafara ya swaumu «Ni adhabu ambayo huwekwa kutokana na kubatilisha na kuharibu funga ya mwezi wa Ramadhan, funga ya nadhiri ya muda maalumu na pia kadhwaa au malipo ya funga ya mwezi wa Ramadhan ikiwa itaharibiwa na kubatilishwa baada ya adhana ya adhuhuri, funga ambayo ilikuwa ni wajibu kwa mukallaf (mwenye kuwajibishwa).»
  • Safari ya Kisheria «Ni safari ambayo ndani yake msafiri analazimika kusali sala zake kwa kupunguza (Sala za rakaa nne azisali rakaa mbili) na hapaswi kufunga Swaumu.»
Kategoria Kuu
Jamii inayoitwa Beliefs‎ haikupatikana
Jamii inayoitwa Culture‎ haikupatikana
Jamii inayoitwa Geography‎ haikupatikana
Jamii inayoitwa History‎ haikupatikana
Jamii inayoitwa People‎ haikupatikana
Jamii inayoitwa Politics‎ haikupatikana
Jamii inayoitwa Religion‎ haikupatikana
Jamii inayoitwa Sciences‎ haikupatikana
Jamii inayoitwa Works‎ haikupatikana
Lugha