Abbas bin Ali bin Abi Talib (a.s)

Kutoka wikishia
Muonekano wa juu mahali alipozikwa Abbas bin Ali bin Abi Talib (a.s)

Abbas bin Ali bin Abi Talib (Kiarabu: العباس بن علي بن أبي طالب) (aliyezaliwa mwaka wa 26 na kufariki mwaka wa 61 Hijiria), umaarufu wake ni Abul Fadhl, naye ni mtoto wa tano wa Imamu Ali (a.s) na mtoto wa kwanza wa Ummul Banina. Sehemu muhimu zaidi ya maisha yake ni kuwepo kwake katika tukio la Karbala na kuuawa kwake kishahidi siku ya Ashura. Hakuna habari nyingi kuhusiana maisha yake na hali yake kiujumla ya kabla ya tukio la mwezi wa Muharram la mwaka 61 Hijiria. isipokuwa tu kwa mujibu wa baadhi ya ripoti ni kwamba, yeye alikuwepo katika vita vya Siffin.

Wakati wa tukio la Karbala, alikuwa kamanda na mshika bendera wa jeshi la Imamu Husein (a.s), naye ndiye aliyewaletea maji Imamu Hussein pamoja na wafuasi wake kutoka kutoka mto Furati (Euphrates). Abbas pamoja na ndugu zake walikataa barua mbili za amani kutoka kwa Ubaidullah bin Ziyad na wakapigana katika jeshi la Imam Hussein (a.s) hadi wakauawa kishahidi. Kwa mujibu wa baadhi ya vitabu vya tukio la mauwaji ya Karbala (مقتل), yeye aliuawa kishahidi siku ya Ashura huku mikono yake miwili ikiwa imekatwa, na rungu la chuma likiangukia kichwani mwake. Baadhi ya wanahistoria wameripoti ya kwamba; Baada ya kuanguka kwake, Imam Husein (a.s) alilikwenda na kusimama chini yake na kumlilia.

Baadhi ya vyanzo vingine vya kihistoria vimemtaja kuwa, yeye alikuwa ni mrefu sana na mwenye sura nzuri. Katika baadhi ya Hadithi, Maimamu wa Shia wameeleza ya kwamba; Bwana Abbas ni mwenye nafasi ya juu Peponi, na kuna karama nyingi zimesimuliwa kutoka kwake, karama hizo zinahusiana na watu kadhaa kukidhiwa haja na maombi yao kumpitia yeye. Nukuu za watu kukidhiwa mahitaji yao zimewahusifa watu mbali mbali, hata wasio Mashia na wasiokuwa Waislamu.

Mashia wanampa nafasi ya juu ya kiroho bwana Abbas; Wanamwita Babu Al-Hawaij na huomba maombi yao kupitia kwake (Wanatawassal kwake). Kaburi la bwana Abbas (a.s) lipo karibu na kaburi la Imam Hussein (a.s) ni moja kati ya sehemu muhimu sana zinazozuriwa na Mashia. Pia, Mashia wanamtabua yeye kwa jina la Saaqi Karbala (yaani mtoa huduma ya unyweshaji maji wa Karbala. Kwa upande wa Mashia, siku ya Tasua, ambayo ni siku ya mwezi 9 Muharram huwa ndio siku maalumu ya kuomboleza kifo cha bwana Abbas. Siku hii ni likizo ya kiserikali nchini Iran. Pia, nchini Iran, siku ya kuzaliwa kwa bwana Abbas, inaadhimishwa kama ni Siku ya Majeruhi Dunianii. Maeneo mengi yaliyojengwa kama ni wakfu wa bwana Abbas. Miongoni mwa majengo yaliojengwa kwa jina lake ni kama vile Saqaqhaane (Nyumba ya Kunywesha Maji), Abbasiyyah (Nyumba ya Abbas) na Saqaanfar (Nyumba ya Utoaji Huduma ya Maji ya Kunywa).

Ukosefu wa Nyenzo vya Utafiti Kuhusu Abbas bin Ali

Kwa mujibu wa baadhi ya watafiti, hakuna taarifa nyingi za kihistoria zinazopatikana kuhusu maisha ya Abbas bin Ali (a.s), yanayohusiana na kabla ya tukio la Karbala, kwa hiyo kuna hitilafu nyingi kuhusiana na kuzaliwa kwake pamoja na maisha yake kwa jumla.[1] Vitabu makhususi vilivyoandikwa kuhusiana na Abbas bin Ali, vinahusiana zaidi na karne ya 14 na 15; Abdul Wahid Muzaffar, mwandishi wa mkusanyiko wa juzuu tatu za habari kuhusiana na Abbas bin Ali zenye jina la Batal Al-Alqami, alifariki mwaka 1310 Hijiria, Mohammad Ibrahim Kalbasi Najafi, mwandishi wa kitabu Khasaa-isu Al-Abbasiyah, alifariki mwaka 1362 Hijiria[2], Muhammad Ali Urdubaadiy, mwandishi wa Hayatu Abi Al-Fadhli Al-Abbas, alifariki mwaka 1380 Hijiria, Mousawi Moqarram, mwandishi wa kitabu Qamar Bani Hashem Al-Abbas, alifariki mwaka 1391 Hijiria na Rabbaani Khalkhaliy ni mwandishi wa kitabu Chehre Derakhshani Qamar Bani Hashem, yeye aliyefariki mwaka 2009.

Jina na Ukoo Wake

Abbas bin Ali bin Abi Talib, ambaye anajulikana kwa lakabu maarufu sana ya Abul Fadhli, ni mtoto wa tano wa Imam Ali (a.s) na natija ya ndoa baina ya Ali bin Abi Talib na Fatima binti Hizam, anayejulikana kwa umaarufu wa Umm al-Banina. Abbas ni mtoto wa kwanza wa Umm al-Banin. [5]

Mama Yake

Mama yake Abbas alitambulishwa kwa Imam Ali (a.s) na Aqeel, ambaye alikuwa mjuzi wa kuelewa nasaba. Imam Ali (a.s) alimuomba Aqeel amtafutie mke atakayemzalia watoto mashujaa na shupavu. [6] Kuna baadhi wamesimulia kwamba, katika usiku wa Ashura, Zuhair bin Qain baada ya kupata habari kuhusiana na barua ya kupewa amani, alimwambia Abbas (a.s): Ewe mwana wa Amiru Al-Muuminiina pale baba yako alipotaka kuoa, alimwambia ami yako Aqeel amtafutie mke kutoka katika ukoo wa mashujaa ili amzalie mtoto shupavu na shujaa, mtoto ambaye atakuwa msaidizi wa Hussein (a.s) katika uwanja wa Karbala. [7] Urdobadi alibainisha ya kwamba; riwaya inayohusiana na mazungumzo ya Zuhair na Abbas hayapo katika kitabu chengine chochote kile isipokuwa katika kitabu Asrar Al-Shahada. [8]

Majina ya Umaarufu (Kuniya)

  • Abul Fadhli: Ndio jina mashuhuri zaidi la Abbas. [9] Wengine wamesema kwamba; Kwa kuwa mtu yeyote aliyeitwa Abbas katika familia ya Bani Hashem, alijulikana kwa umaarufu wa Abul Fadhli, bwana Abbas (a.s) pia aliitwa Abul Fadhli hata katika zama za utoto wake. Sayyid Abul-Razzaq Musawi Muqrim, akinukuu kutoka katika kitabu "Al-Jaradatu fi Usul Ansab Al-Alawiyyina amesema: "Abbas (s.a.w.w) alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Fadhli. Kwa hiyo, akwa ni maaru kwa jina la baba wa Fadhli. [11]
  • Abul Qasim: Pia ni moja ya majina maarufu ya Bwana Abbas (a.s), yeye aliitwa jina hilo kuwa alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Qasim. Jina hili pia limetajwa katika Ziaratu Arbaeen. [12]
  • Abul Qirbah: Baadhi wanaamini kwamba jina hili alipewa kwa sababu ya kumwaga maji kwenye mahema mara kadhaa wakati wa tukio la Karbala. Al-Qirbah (القِربَة): Ni chombo cha kuchukulia maji ambacho hutengenezwa kwa ngozi ya mnyama. Inasemekana Abul-Fadhli Abbas alichukua chombo hicho na kuwagilia maji juu ya mahema ya yao ya Karbala, kwa ajili ya kuzima moto uliowashwa na maaadui zao. [13] Jina hili limenukuliwa kotaka katika vyanzo kadhaa. [14]
  • Abul Farajah: Sababu ya jina hili ni kwamba Abbas (a.s) ni mtu mmoja ambaye wato huomba duwa kupitia jina lake, nao hupata matilaba yao kutoka kwa Mwenye Ezi Mungu kutokana na utukufu na ukaribu wake kwa Mola wake. [15] Jina Farajah lina maana ya kutatua na kuondoa matatizo. [16]

Lakabu

Kuna majina kadhaa ya lakabu aliyopewa Abbas (a.s), baadhi ya lakabu hizo ni za zamani na nyengine ni mapya, ambazo watu waliokuja baada yake wamezinasibisha lakabu hizo kwake yeye (a.s), kutokana na sifa na wasifu aliokuwa nao. [17] Baadhi ya lakabu zake ni:

  • Qamar Bani Hashim (Mwezi wa Bani Hashim). [18]
  • Bab Al-Hawaij (Mlango wa Kutatua Matatizo). [19] Kulingana na mtazamo wa Al-Baghdad, lakabu hii ni maarufu miongoni mwa Mashia wote, hasa Mashia wa Iraq. [20] Watu wengi wanaamini kwamba, wakiomba dua na haja zao kupitia kwa bwana Abbas, basi bila shaka Mungu atawatimizia mahitaji yao. [21]
  • Saqqaa: Baadhi wanaamini kwamba lakabu hii ni maarufu miongoni mwa wanahistoria na watu wa fani ya kutambua nasaba. [22] Abbas (a.s) aliwaletea maji wanawake na watoto wa Karbala mara tatu. [23] Katika mashairi mafupi (rajzi) ya bwana Abbas (a.s), jina hili limeonekana kutajwa ndani yake, kama vile (اني انا العباس اغدوا بالسقی) ; Mimi ni Abbas na mimi huamkia asubuhi nikiwa ni mnyweshaji maji. [24]
  • Al-Shaheed (aliyeuwawa kishahidi). [25]
  • Mshika bendera. [26]
  • Bab Al-Hussein: Baadhi, wakitegeme karama zakwa Seyyid Ali Qazi Tabataba'i, mcha Mungu Shia, aliyesema kwamba: "bwana Abul Fadhli Al-Abbas (a.s) ni Kaaba ya mawalii wa Mungu". Hiyo ndiyo sababu ya yeye kupewa jina hilo. [27]

Maisha Yake

Kwa mujibu wa baadhi ya watafiti wa historia, hakuna taarifa nyingi za kihistoria zinazopatikana kuhusiana na maisha ya Abbas kabla ya tukio la Karbala. [28] Tukio pekee lililonukuliwa kutoka katika maisha yake ya kabla ya tukio la Karbala, ni kuwepo kwake katika vita vya Siffin, na pia nukta nyengine kuhusu yeye, ni kushiriki kwake katika maziko ya Imam Hassan Mojtaba (a.s). [29] Mengine yaliyosalia kuhusiana na maisha yake, yanahusiana na tukio la Karbala. [30]

Kuzaliwa Kwake

Kuna khitilafu juu ya mwaka wa kuzaliwa kwa Abbas (a.s). [31] Pengine khitilafu hizi zinatokana na riwaya zinazozungumzia idadi ya miaka ya Abbas (a.s) wakati wa kifo cha kishahidi cha baba yake (Imam Ali (a.s)). Ambapo kuna baadhi walioukadiria umri wake katika tukio hilo ni baina ya miaka 16 na 18. [32] Wengine waliukadiria umri wake kuwa ni miaka 14, ambapo kwa mtazamo huu, yeye atakuwa bado hakuwa baleghe katika kipindi cha tukio hilo. [33]

Kauli mashuhuri ni kwamba Abbas alizaliwa Madina mnamo mwaka wa 26 Hijiria. [34] Kwa mujibu wa mtazamo wa mwanahistoria ajulikanaye kwa jina la Urdubadi, ni kwamba; Hakuna kinachoweza kupatikana kuhusiana siku na mwezi wa kuzaliwa kwake katika vyanzo vya zamani, na ni kitabu tu kiitwacho Anisu Al-Shia kilichoandikwa katika Karne ya 13 Hijiria, ndicho kilicho nukuu siku ya kuzaliwa kwake. Ambapo ndani ya kitabu hicho, imeelezwa ya kwamba, yeye alizaliwa mwezi 4 Shaabani. [35] Mwandishi wa Khasaa-isu Al-Abbasiyah aliandika bila kutaja chanzo, kwamba Abbas alipozaliwa Imamu Ali (a.s) alimkumbatia na kumwita na kumpa jina la Abbas. Kisha akamsomea adhana na iqamah masikioni mwake, kisha akaibusu mikono yake huku akilia.” Katika kumjibu Ummul Banina, ambaye aliuliza sababu ya kulia kwake, alisema kwamba; Mikono miwili ya Abbas itakatwa akiwa katika jitihada za kumsaidia Hussein (a.s), na Mungu atampa mbawa mbili katika Akhera yake badala ya mikono yake miwili iliyokatwa. [36] Vitabu vyengine pia kwa kuutegemea nukuu hii, vimenukuu tukio la kilio cha Imamu (a.s) kwa huzuni kukatwa mikono miwili ya Abbas (a.s). [37]

Mke na Watoto Wake

Abbas (a.s) alimuoa Lubabah, mjukuu wa Abbas bin Abd Al-Muttalib, kati ya miaka 40 na 45 ya mwandamo. [39] Baadhi ya vyanzo vinamtaja baba yake Lubabah kawa ni Obaidullah bin Abbas. [40] na wengine wamesema yeye ni bint ya Abdullah bin Abbas. [41] Ibnu Habib Al-Baghdadi, mwanahistoria wa karne ya tatu ya mwandamo, alimchukulia mke wa Abbas Lubabah kuwa binti ya Ubaidullah na akamtambulisha binti ya Abdullah Lubabah kama ni mke wa Ali bin Abdullah Jafar. [42] Lubabah alimzalia Abbas watoto wawili wa kiume walioitwa Fadhlu na Ubaidullah. [43] na Baada ya Abbas kufa kishahidi, kwanza aliolewa na Waleed bin Utbah kisha akaolewa na Zaid bin Hassan. [44]

Ubaidullah, mtoto wa Abbas (a.s), alimuoa binti wa Imam Sajjad (a.s). [45] Baadhi ya waandishi wamewataja watoto wengine walionasibishwa na Abbas, nao ni: Hassan, Qasim, Muhammad na binti mmoja wa Hazrat Abbas. Wao walisema kwamba; Qasim na Muhammad walikufa kishahidi katika tukio Ashura baada ya baba yao kuuawa kishahidi katika tukio hilo. [46]

Imeripotiwa kwamba kizazi cha bwana Abbas kiliendelea kupitia kwa wanawe wawili, ambao ni Ubaidullah na Hassan. Watoto wa bwana Abbas ni ukoo maarufu miongoni mwa koo za Ma'alawiy, na wengi wao walikuwa ni wanazuoni, washairi, makadhi na watawala. [47] Kuna ripoti kadhaa zinazoelezea kuenea kwa kizazi cha bwana Abbas kutoka Kaskazini mwa Afrika hadi Iran. [48] Baadhi ya sababu za kuenea kwao huko ni kuhama kwa watoto wa bwana Abbas kutokana na ukandamizaji wa serikali mbali mbali maishani mwao. [49]

Vita vya Siffin

Kuwepo kwa Abbas (a.s) katika tukio la vita vya Siffin kumetajwa katika baadhi ya vitabu vilivyoandikwa baadaye. Katika vita hivyo, yeye alikuwa ni mmoja wa watu walioshambulia mto Furati chini ya uongozi wa Malik Ashtar katika Vita vya Siffin na kuchota maji kutoka katika mto huo kwa ajili ya askari wa Imam Ali (a.s). Kuuliwa kwa Ibnu Sha'athaa alikuja kutoka mji wa Sham pamoja na wanawe saba kupitia upanga wa Abbas, ni miongoni mwa ripoti zilizonukuliwa na kuandikwa ndani ya vitabu hivyo vya wa waandishi walikuja baadae. [51] Kwa mujibu wa baadhi ya waandishi, watu wa Syria walikuwa wakizihisabu nguvu za Ibn Sha'athaa kuwa sawa na wapambanaji elfu moja. [52] Pia kuna walipingana na nadhariya ya Abbas kushiriki katika vita vya Siffin, wakisema kwamba, nukuu hizi haziendani na ushahidi wa kihistoria. [53]

Kwa mujibu wa mtazamo wa Urdubadi aliyouelezea katika kitabu chake ni kwamba; Hadithi ya wasia wa Imam Ali kwa Abbas na nasaha zake kwake kuhusiana Imamu Hussein, ingawa ni maarufu, ila Hadithi hiyo haina mashiko madhubuti. [54]

Katika Tukio la Karbala

Makala Asili: Tukio la Karbala

Kuwepo katika tukio la Karbala ni sehemu muhimu zaidi ya maisha ya Abbas bin Ali (a.s) na umuhimu wake kwa Mashia, unatokana na jukumu alilokuwa nalo katika tukio hilo la Karbala. Abbas anahisabiwa kuwa ni mmoja wa watu mashuhuri zaidi katika tukio la msimamo wa Imam Husein. [55] Hata hivyo, katika vitabu vingi makhususi vilivyoandikwa kuhusiana naye, hakuna ripoti ya kihistoria au simulizi kuhusiana na Abbas kutoka wakati wa kuondoka kwa Imam Husein (a.s) kutoka Madina hadi Makka na kisha kutoka Makka hadi Kufa. Yaani hakuna ripoti zilizomripoti katika msafara huo wa kabla ya mwezi wa Muharram 61 Hijiria. [56]

Mihadhara Yake Huko Makka

Mwandishi wa kitabu "Khatib Kaabeh" amenasibisha moja ya khutba kwa Abbas (a.s). [57] Amefanya hivyo kwa kutegemea maelezo yaliyomo katika kitabu "Manaqib Sadati Al-Kirami" yeye mwenyewe katika maandishi yake, amekiri ya kwamba, yeye hajakiona kitabu hicho. [58] Kwa mujibu wa riwaya hii, bwana Abbas alitoa khutba akiwa juu ya paa la Al-Kaaba katika siku ya nane ya Dhul-Hijjah, ambamo alikosoa utiifu wa watu juu ya kumtii Yazid, alisisitiza katika ukosowaji wake huo sifa ya ulevi wa Yazid, na kuwafahamisha watu nafasi ya Imamu Hussein (a.s). Katika khutba hiyo alisema kwamba maadamu yu hai hatamruhusu mtu yeyote kumuua shahidi Imamu Hussein (a.s) na njia pekee ya kumuua shahidi Imamu ni kumuua Abbas. Bwana Juyaa Jihan Bakhshe, katika moja ya makala zake, akitegemea changamoto na tata za kiligha zilizomo katika khutba hiyo, pamoja na kule kutojulikana kwa mwandishi wa kitabu hicho pamoja na asili ya kitabu chenyewe, yeye amepingana na uhakika wa hutuba hiyo, na akaelezea wazi ya kwamba kisa cha hutuba hiyo hakikunukuliwa na katika kitabu chochote kile miongoni mwa vitabu. [60]

Kushikilia Bendera Siku ya Ashura

Bwana Abbas (a.s) alikuwa ni mshika bendera wa jeshi la Imamu Hussein (a.s) siku ya Ashura. Imam (a.s) alimkabidhi nafasi hiyo asubuhi ya Ashura. [61] Kwa mujibu wa baadhi ya ripoti, pale Imamu (a.s) alipomtaka Abbas kwenda uwanjani, alikumbushwa kubeba bendera yake. [62]

Kuchota na Kunywesha Maji

Kwa mujibu wa vyanzo vya kihistoria, wakati adui alipowakatia maji watu wa msafara wa Imamu Husein (a.s) kiu ilitanda miongoni mwa wanawake, watoto pamoja na masahaba zake. Katika hali hiyo, Imamu alimtuma Abbas pamoja na wapanda farasi thelathini na askari wa miguu ishirini wakiwa na mitungi ishirini ya maji kwenye fukweni mwa mto Furati (Euphrates) ili wachote maji. Ilikuwa ni wakati wa usiku, ambapo wao walisogelea ufukweni mwa mto huo, lakini Amru bin Hajjaj na wafuasi wake walitia nia ya kuwazuia wasiyafikie maji ya mto huo. Katika ahali Abbas na masahaba wake waliwarudisha nyuma na hatimaye wakafanikiwa kujaza maji kwenye vyombo walivyokuwa navyo. Wakati wanarudi kutoka mtoni, Amru bin Hajjaj na wafuasi wake waliwashambulia. Abbas na wapanda farasi wengine walifungia njia maadui hao, na kuwawezesha askari wa miguu kuyafikisha maji kambini. [63]

Kuikataa Barua Amani

Wakati msafara wa Hosseini ulipokuwa Karbala, adui alimtumia na ndugu zake barua mbili za amani.

Barua ya Amani Kutoka kwa Abdullah bin Abimahal

Wakati Shimru bin Dhil Al-Jaushan alipopokea barua kutoka kwa Bin Ziad, inayomtaka apambane na Imamu Husein (a.s) au ahakikishe kuwa amesalimu amri, alipokuwa akitoka kwenye kasri, Abdullah bin Abimahal, ambaye ni mtoto wa kaka yake Umm Al-Banina, ambaye pia alikuwa ni mmoja wa wafuasi wa Shamru, alipokea barua ya amani kutoka kwa Ubaidullah bin Ziad kwa ajili binamu zake, ambao ni Abbas na ndugu zake. Barua hiyo aliituma kwenye kambi ya Imam Husein kwa ajili ya watoto wa Umm Al-Banina kupitia mtumishi wake. Mjumbe wake alipofika kwa Abbas na ndugu zake, aliwaambia: Ami yenu amekutumieni barua hii ya amani. Wao waliipokea barua hiyo kisha wakasema: Msalimie ami yetu na mwambie kwamba sisi hatuhitaji barua ya amani, barua ya Mwenyezi Mungu ni bora kwetu kuliko barua ya amani ya Ibnu Sumayyah. [64]

Barua ya Amani Kutoka kwa Shimru Dhil Al-Joshan

Usiku wa tarehe 9 Muharram, Shimru alisimama mbele ya masahaba wa Hussein na akisema: Wako wapi wana wa dada yangu?! Abbas, Jafa'ar na Othman, walipomsikia wakatoka nje ya hema na kusema: Unataka nini? Shimru akasema: Nyinyi mupo katika amani, Wkamjibu kwa kusema: Ikiwa wewe ni mjomba wetu, basi Mwenyezi Mungu akulaani wewe na barua yako ya amani. Wewe umetuletea sisis barua ya amani, na ukamwacha mtoto wa Mtume bila ya amani! [65]

Ibn A'atham (aliyefariki mwaka wa 314 Hijiria) ameeleza katika moja ya maelezo yake ya kwamba: Wakati Shimru alipowaita wana wa Ummu Al-Banina, Hussein aliwaambia ndugu zake: Muitikieni hata akiwa ni fasiki, kwa sababu yeye ni miongoni mwa ami zenu. Bwana Abbas na ndugu zake wakamwambia Shimru: Unasema nini? Shimru akasema: Enyi watoto wa dada yangu! nyinyi mupo katika amani. Msijiangamize na kujiuwa pamoja na Hussein. Na badala yake mtiini Amirul Muuminiina Yazid. Hapo Abbas bin Ali alisema: Kifo kiwe juu yako, ewe Shimru! Mungu akulaani wewe na barua yako ya amani, Ewe adui wa Mungu! Je, hivi wewe unatuambia tumtii adui na tuache kumsaidia ndugu yetu?! [66]

Riwaya nyingine kutoka kwa Ibn Kathir (aliyefariki mwaka 774 Hijiria) zimenukuliwa kama ifuatavyo, kinyume na maandishi mengi ya kale: Ndugu zake Hussein walimwambia Shimru: Ukitupa amani sisi na ndugu yetu Hussein, sisi pia tutaikubali amani yako, vinginevyo hatuhitaji barua yako ya amani. [67] Lakini kidhahiri, riwaya za Ibn Kathir na Ibn A'atham, kwa sababu ya nyakati ambazo vitabu hivyo vimeandikwa na muktadha wa yaliyomo ndani yake, riwaya zake zinastahiki kutizamwa kiumakini zaidi, kwani riwaya hizo ziko kinyume na ripoti za vitabu vya kale. [68]

Kuuawa kwa Ndugu Zake Abbas

Kwa mujibu wa ripoti za kihistoria, matokeo na tija ya ndoa Imamu Ali (a.s) na Ummu Al-Banina, ilikuwa ni kuzaliwa watoto wanne wa kiume, nao ni: Abbas, Jafar, Abdullah na Othman. [69] Abbas aliwahimiza ndugu zake kupigana katika tukioi la Ashura. Ripoti hii imenukuliwa ndani ya vyanzo vya kihistoria, ikizungumzia sababu mbili tofauti zilizomfanya Abbas awahimize nduguze kupigana vita ndani ya uwanja wa Karbala.

Sababu ya Kiurithi

Kwa mujibu wa riwaya ya Abu Makhnaf (aliyefariki mwaka 157 Hijiria), Tabari (aliyefariki mwaka 310 Hijiria), na Ibn Athir (aliyefariki mwaka 630 Hijiria), ni kwamba: Abbas aliwaambia nduguze wa mama mmoja, ambao ni: Abdullah, Ja'afar na Othman: "Enyi watoto wa mama yangu, nendeni vitani mkapambane, ili nipate kukurithini kwa sababu nyinyi hamna watoto wa kukurithini." Nao walifanya vivyo hivyo walivyoagizwa na ndugu yao, na hatimaye wakauawa kishahidi. [70]

Lakini kwa mtazamo wa baadhi ya watutaarifa hii si sahihi, kwa sababu katika hali hiyo, Abbas alijua kwamba atauawa ndani ya vita hivyo, na kuomba urithi hakuleti maana yoyote baada ya kufa kwake. [71] Pia, ripoti hii haiendani na sheria ya urithi, kwa sababu kuwepo kwa Ummu Al-Banina na ukweli wa kwamba ndugu zake Abbas hawakuwa na mke wala watoto, kama hawakuwa nao, basi urithi haungekwenda kwa Abbas, ila Ummu Al-Binina ndiye atakayekuwa mrithi wa wanawe. [72]

Ili Ashuhudie Mapambano Yao

Katika riwaya nyingine, Sheikh Mufid (aliyefariki mwaka 413 Hijiria), Tabrasi (aliyefariki mwaka 548 Hijiria), Ibn Nama (aliyefariki maka 645 Hijiria), na Ibn Hatim (aliyefariki mwaka 664 Hijiria) wamesimulia ya kwamba: Abbas bin Ali alipoona, wengi miongoni mwa watu wake tayari wameshauliwa kishahidi, aliwaambia ndugu zake wa upande wa umamani, ambao ni: Abdullah, Ja'afar na Othman akisema: "Enyi watoto wa mama yangu! Nendeni uwanjani ili nikushuhudieni jinsi ya nyinyi mtakavyouawa kishahidi katika njia ya Mwenyezi Mungu. Mimi Ninakunasihini kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, kwa sababu nyinyi hamna watoto.” [73] Pengine sababu iliyomfanya Abbas kuwapeleka ndugu zake uwanjani kabla yake, ni kwa ajli ya kupata thawabu za kuwatayarisha kwa ajili ya jihad na pia kupata malipo ya subira kwa ajili ya kifo cha kishahidi cha ndugu zake. [74]

Mashairi ya Hamasa ya Siku ya Ashura

Kuna mashairi tofauti kutoka kwa Abbas (a.s) yaliyoripotiwa wakati wa tukio la Karbala; [75] miongoni mwayo ni shairi lifuatalo: أقسَمتُ بِالله الأَعَزِّ الأَعظَم‏ * وَ بِالحَجونِ صادِقاً وَ زَمزَم‏ وَ بِالحَطيمِ وَالفَنَا المُحَرَّمِ * لَيُخضَبَنَّ اليَومَ جِسمي بِدَمي دونَ الحُسَينِ ذِي الفَخارِ الأَقدَمِ * إمامُ أهلِ الفَضلِ وَالتَّكَرُّم[76]

Ninaapa kwa Mwenyezi Mungu mtukufu na Adhimu kuliko kila adhimu, na pia kwa Hajoon (mava ilioko Makka) na kwa maji ya Zamzam * Ninaapa kwa nyumba ya Mungu na eneo la Msikiti Mkuu kwamba leo mwili wangu utakuwa na rangi ya damu iliokoza * Kwenye miguuni ya Husein ambaye ndiye mmiliki aliye wa mwanzo katika sifa bora na heshima, kiongozi wa watu wema na waliotakasika na kila sifa mbaya.

لا أرهَب الموتَ إذ الموتُ زقا * حتى أُوارى في المصاليت لقا نفسي لنفس المصطفى الطُّهر وَقا * اني أنا العباس أغدو بالسِّقا و لا أخاف الشر يوم المُلتقى * و لا أخاف الشر يوم الملتقى[77] Siogopi kifo, pale sauti ya kifo inapoita * mpaka nianguke kati ya watu waliotahiniwa na kufunikwa na udongo, roho yangu ni ngao na muhanga wa maisha ya Hossein, mteule aliyetoharika, mimi ni Abbas, ninayekuja na mtungi wa maji, na siku ya vita, hakuna ninachokiogopa kutoka kwa maadui.

وَاللهِ إن قَطَعتُمُ يَميني * إنّي اُحامي أبَداً عَن ديني‏ وعَن إمامٍ صادِقِ اليَقينِ * نَجلِ النَّبِيِّ الطّاهِرِ الأَمين Wallahi ingawaje mmenikata mkono wa kulia wangu * bado milele na milele nitaendelea kuilinda dini yangu. Nitamlinda Imamu mwenye ukweli yakinifu * mwana wa Mtume mwaminifu.

Kifo Chake cha Kishahidi

Kwa mujibu wa maandishi ya Mohammad Hassan Modhaffar, maoni ya wanahistoria wengi ni kwamba; Abbas (a.s) bila shaka aliuawa kishahidi mnamo tarehe 10 Muharram. Mudhaffar alitaja kauli nyengine mbili tofauti moja ya kauli hizo inasema kuwa yeye aliuliwa mwezi 7 Muharram na huku kauli ya pili ikisema kuwa tukio hilo limetokea mnamo mwezi 9 Muharram. Ila yeye amezihisabu kauli hizi kuwa ni kauli dhaifu, na ni kauli nadra sana. [80]

Kuna nukuu mbalimbali kuhusiana na mambaano ya Abbas (a.s) katika siku ya Ashura, na jinsi alivyouawa kishahidi katika tukio hilo. [81] Kwa mujibu wa baadhi ya vyanzo, Abbas hakwenda uwanjani hadi alipouawa kishahidi sahaba wa mwisho wa Imam Hussein pamoja watu wa ukoo wa Bani Hashim. [82]

Kwa mujibu wa kauli ya Sheikh Mufid, Imamu Hussein na Abbas bin Ali (a.s) walikwenda uwanjani wote wawili kwa pamoja, lakini jeshi la Omar Saad liliwatawanya na kuwanya kila mmoja awe mbali na mwenziwe katika mapambano hayo. Imamu Hussein alijeruhiwa na akarudi hemani, na Abbas alipigana peke yake mpaka akajeruhiwa vibaya sana na hakuweza tena kupigana. Hapo ndio, Zaid bin Warqa Hanafi na Hakim bin Tufail Sinbisi walipomvamia na kumuua. [83]

Sheikh Mufid hakunukuu ufafanuzi mwengine zaidi ya huo. Pia hata katika kijulikanacho kwa jina la Waq’at Al-Taff (Maqatl Abi Makhnaf), hakuna ufafanuzi wa wazi juu ya cha kishahidi cha bwana Abbas. [84] Walioelekezewa vidole katika kumua Abbas katika matini ya Ziara Naahiyeh Ghairi Mash-huur, ni: Yazid bin Waqqad na Hakiim bin Al-Tufail Al-Ta'ee. [85]

Kwa mujibu wa baadhi ya vyanzo vyengine, baada ya kuuawa kishahidi kwa masahaba wote na familia ya Bani Hashim, Abbas alipanga kupeleka maji kwa ajili ya famili na watoto walioko mahemani. Ili kukamilisha lengo hilo, alianzisha shambulio kuelekea mtoni Furati, na alifanikiwa kuwatawanya walinzi waliokuwa wakiulinda mto huo. Akiwa njiani kutokea mtoni humo, madui walimshambulia, yeye akapigana nao kwenye mtende, akiwa anaelekea mahemani. Hapo ndipo Zaid bin Warqaa Juhani aliporuka kutoka nyuma ya mtende na akampiga panga mkono wa kulia. Abbas aliushika upanga wake kwa mkono wa kushoto na kuendelea kupigana na maadui zake. Hakiim bin Tufail Al-Ta'i, ambaye alikuwa amejificha nyuma ya mti, akampiga kwenye mkono wa kushoto na kisha akachukuwa gongo (rungu) na kulikita juu ya kichwa cha Abbas na kummaliza. [86]

Kwa mujibu wa riwaya ya Khaarazmi, wakati Abbas (a.s) alipouawa kishahidi, Imamu Hussein (a.s) aliudogelea mwili wa nduguye, akalia sana kwa uchungu kisha akasema: "اَلآنَ اِنکَسَرَ ظَهری وَ قَلَّت حیلَتی" ; “Sasa uti wa wangu mgongo umevunjika na nguvu (mbinu) zangu zimenguka.” [87] Kwa muji wa nukuu hizi za Khwarazmi, yeye kumuhisabu bwana Abbas kuwa ndiye mtu wa mwisho aliyeingia vitani katika tukio la Karbala. [88]

Tizama Pia: Mshale Wenye Ncha Tatu

Kuto Kunywa Maji kwa Heshima ya Imam Husein (a.s)

Kwa mujibu wa maoni ya Fakhr Al-Din Tariihiy, mwanachuoni wa karne ya 11, kupitia kitabu Al-Muntakhab Abbas, anasema; "Abbas alipoingia katika mto wa Furati (Euphrates), alichota maji kwa viganij vyake ili anywe, lakini alipoyakaribisha maji hayo mbele ya uso wake, alikumbuka kiu ya Hussein na kuachana na maji hayo. Akatoka mtoni hapo na kiu yake, huku akiwa na mtungi uliojaa maji. [89] Pia Allamah Majlisi katika Bihar al-Anwar amenukuu kisa hichi bila kutaja jina la chanzo kikuu cha nukuu hiyo. [90] Habibullah Chaaichian, mtunga mashairi na mwombolezaji wa Ahl Al-Bait (a.s), akiashiria tukio hili, aliandika mashairi yafuatayo kwa lugha ya Kiajemi:

کربلا کعبه‌ی عشق است و من اندر احرام شد در این قبله‌ی عشاق دو تا تقصیرم دست من خورد به آبی که نصیب تو نشد چشم من داد از آن آبِ روان تصویرم باید این دیده و این دست دهم قربانی تا که تکمیل شود حجّ من و تقدیرم

Karbala ni Kaaba ya mapenzi, na mimi niko ndani vazi la Ihramu, ukelele wa jicho langu unaililia ile taswira ya maji yanayotirirka.

Mkono wangu uligusa maji ambayo hukubahatika nayo, ambapo ingelikamilika hija na hatima yangu, ni wajibu kutoa muhanga mkono pamoja na jicho langu. [91]

Urdubadi amejaribu kuthibitisha kufanyika kwa tukio hili kwa kuchambua baadhi ya mashairi na sehemu ya maandishi ya Ziara Nahiyah Al-Muqaddasah. [92] Joya Jahanbakhsh, ambaye ni mtafiti wa mila na desturi, katika moja ya dokezo fulani, amesema kwamba tukio hili halikuonekana kunukuliwa katika Maandiko ya kale. Yeye ana wasiwasi ya kwamba, pengine tukio hili linaweza kuwa na mizizi katika maombolezo ya kale yaliomo katika kitabu Muqatil Al-Taalibiina, ambapo imeandikwa ndani ya kitabu hicho ya kwamba: "Abul Fadhli alimpelea maji Hussein na kujinyima yeye mwenyewe maji haji hayo bila kujali kiu kali aliyonayo".[Angalia 1] [93]]

Sifa Zake

Baadhi wanaona ya kwamba; Moja ya sifa muhimu zinazompa Abbas daraja maalumu, ni kuishi na kuwa pamoja na Imam Ali, Imam Hassan, na Imamu Hussein (a.s). [94] Aburazzaq Muqarram katika kitabu Al-'Abbas, amenukuu ibara kutoka katika kitabu Asraru Al-Shahada ambayo inasadikiwa kuwa ni Hadithi kutoka Maasumina (watu watoharifu), ya kwamba; Abbas alikuwa na nafsi maalumu ya elimu. [95] Ja'afar Naqdi ameandika kuhusiana na Abbas (a.s) akisema: “Yeye katika masuala ya elimu, uchamungu, dua na ibadani, ni mmoja wa watukufu wa ukoo wa Ahlul-Bait .” [96] Baadhi wanaamini kwamba; Ingawa Abbas hakuwa miongoni mwa Ma'asumina (watu waliotoharishwa) kidaraja, ila yeye ndiye mtu wa karibu zaidi wa daraja hiyo. [97] Bwana Abbas (a.s) amewadiriki Maimamu watano watoharifu katika maisha yake, nao ni: Imam Ali, Imamu Hassan, Imamu Hussein, Imam Sajjad na Imam Baqir (a.s). ambapo Imamu Hussein, Imam Sajjad na Imam Baqir (a.s) walikuwepo katika tukio la Karbala. [98] Kwa hiyo moja sifa zilizotajwa na waandishi mbalimbali, ni kule yeye katika zama za Maimamu hao watano.

Waandishi waliukuja baadae wameandika kwamba; Abbas (a.s) katu yeye hakujiona yupo sawa kidaraja na kaka zake wawili, yaani Imamu Hassan na Imamu Husein (a.s), ambao ni wakubwa zake kiumri. Mara zote aliwahisabu kuwa Maimamu wake na alikuwa mtiifu na mwenye kuwanyenyekea. [99] Daima alipokuwa pamoja nao, Alikuwa akitumia ibara isemayo "Yaa Ibnu Rasoolullah", "Yaa Sayyidiy" na kadhalika, pale alipokuwa akizungumza nao. [100]

Kalbasi katika kitabu “Khasaa-isu Al-Abasiyyah” amenukuu akisema kwamba; Abbas (a.s) alikuwa na uso wenye kupendeza, ndio maana akaitwa Qamar Bani Hashim (Mwezi wa Ukoo wa Hashim). [101] Imeripotiwa kutoka kwa muuwaji ya kwamba, pale alipomuuwa Abbas (a.s), alisema: Mimi nimeshamuuwa yule mwenye mwili unaopendeza, ambaye alikuwa na dalili ya kusujudu katikati ya kipaji chake cha uso. [102] Kulingana na baadhi ya ripoti, imeelezwa ya kwamba; Yeye alihisabiwa kuwa ni mtu mwenye maumbile maalumu mingoni mwa watu wa ukoo wa Bani Hashim, ambaye alikuwa na mwili wenye nguvu na mrefu, kiasi kwamba alipokuwa ameketi juu ya farasi, miguu yake ilikuwa ikiburura chini. [103]

Pia Mojawapo ya sifa za Abbas (a.s), zilizodaiwa na mwandishi ajulikanaye kwa jina la Kalbsi, ni kwamba; Ushujaa wa Abbas ni sifa maarufu aliyosifika nayo, kiasi ya kwamba hakukua na rafiki wala adui aliweza kuikanusha sifa hiyo. [104] Wengi wamemsifu yeye kwa sifa za ukarimu na kuwa na mkono mkunjufu, jambo ambalo likawa ni sifa ya kupigiwa mfano ndani ya jamii. [105]

Hadhi ya Abbas (a.s) Mbinguni na Wivu wa Mashahidi Wengine

Abbas anahisabiwa kuwa ni mmoja wa masahaba wa Imam Hussein (a.s) wenye msisitizo na umashuhuri zaidi katika tukio la Ashura.[106] Yeye ndiye aliyekuwa mshika bendera wa jeshi la Imam Hussein (a.s) katika tukio la Karbala. [107] Imam Hussein (a.s) kuhusiana naye alisema akimwambia: “Roho yangu iwe ni mhanga kwako ewe ndugu yangu.” [108] Pia pale Abbas alipoanguka, Imamu Hussein (a.s) aliusogelea mwili wake na kuulilia. [109] Baadhi ya watu mbali mbali, wameyahisabu matendo hayo ya Imamu Hussein (a.s), kuwa ni jambo linaloashiria daraja na hadhi ya Abbas mbele ya Imamu wa tatu wa Mashia (Imamu Hussein (a.s)). [110]

Pia katika Hatidhi imezungumziwa hadhi maalumu ya bwana Abbas ya huko peponi. Kwa mujibu wa moja ya Hadithi hizo ni kwamba; Imam Sajjad (a.s) alisema, Mungu amrehemu ami yangu Abbas, ambaye alijitoa muhanga kwa ajili ya kaka yake Imamu Hussein (a.s), naye katika njia hiyo akakatwa mikono yake miwili. Ila Mwenyezi Mungu siku ya Kiama atampa mbawa mbili badala ya mikono yake hiyo miwili, ili aruke pamoja na Malaika wa peponi kwa mbawa hizo mbili, kama vile Ja'afar bin Abi Talib pia alivyopewa mbawa mbili". [111] Imam aliendelea kusema kwamba; "ami yangu, Abbas ana hadhi na nafasi kumbwa mbele ya Mwenyezi Mungu kiasi ya kwamba mashahidi wote Siku ya Kiyama watamuonea wivu kutokana na nafasi yake hiyo." [112] Pia, Abu Nasr Bukhari amesimulia Hadithi kutoka kwa Imamu Swadiq (a.s), ambapo ndani ya Hadithi hiyo Abbas amesifiwa kwa sifa ya «نافذ البصیرة» “Nafidhu Al-Basira” (mwenye utambuzi wa kina), na akamtambulishwa kuwa ni muumini mwenye imani pevu, aliye pambana katika jihadi sambamba na Imamu Hussein (a.s) hatimae kuuawa kishahidi. [113] Riwaya hii pia inapatikana katika vyanzo vingine mbali mbali. [114]

Sayyid Abdul Al-Razzaq Muqarram anasema katika kitabu chake Maktal Al-Hussein kwamba; Imam Sajjad (a.s) aliomba msaada kutoka kwa Bani Asad ili kuizika miili ya mashahidi wote wa Karbala baada ya tukio la Ashura, lakini hakuomba msaada kutoka kwao kwa ajili ya kuuzika mwili Imam Hussein na Abbas (a.s). Yeye aliwambia watu wa Bani Asad ya kwamba; mimi sihitaji msaada katika kuwazika mashahidi wa Karbala wawili hawa, kwani wapo wanaonisadia katika kuwazika mashahidi hawa. [115]

Matini ya Amali ya Ziara

Kwa mujibu wa ripoti ya kitabu "Sire wa Siimaye Abbas bin Ali", kuna idadi ya matini 11 zimesimuliwa katika vitabu tofauti kwa ajili ya amali ya kumzuru bwana Abbas. [116], ambazo baadhi yake huchukuliwa kuwa ni mukhtasari wa amali kutika katika matini nyengine. [117] Kati ya matini kumi na moja zilizotajwa, tatu mingoni mwazo, zimenukuliwa kutoka kwa Imamu Swadiq (a.s) [118] huku baadhi yake zikiwa zimetiliwa shaka katika ya kwamba yawezekana kuwa hazitokani na Ma'asumina (Waliotoharishwa). [119]

Katika matini ya amali (ziara) hizo, kuna ibara zinazomsifu bwana Abbas mfano wake ni; Abdu Saleh, mtu anayejisalimisha kwa mrithi wa Mtume (s.a.w.w) na akamkubali na kuwa mtiifu kwake, mtiifu kwa Mwenyezi Mungu, kwa Mtume na kwa Maimamu (a.s), na mtu anayefanana na Badriyyuun (watu waliopigana vita vya Badri) katika kufanya jihadi kwenye njia ya Mwenyezi Mungu. [120] Pia, baadhi ya watu, wakiegemea baadhi vipengele vya matini kuhusiana na amali za ziara zilizoko katika matini ya Ziaratu Nahiyah Al-Muqaddah [Maelezo 2], inayohusiana na bwana Abbas, wamesisitiza kuwa; Vipengele hvyo vinaashiria ukubwa wa hadhi ya Abbas mblele ya Imamu Zaman (a.t.f.s). [121]

Karama za Abbas

Karama za Hadhrat Abbas ni maarufu sana miongoni mwa Mashia, na kuna ripoti nyingi kuhusu kuponya wagonjwa au kutatua matatizo mengine ya watu kumwomba Mungu kupitia utukufu na baraka za bwana Abbas (a.s). Kitabu "Dar Al-Qamah Karamat Al-Abbasiyah" kimekusanya ripoti 72 kuhusiana na karama hizo. [122] Bwana Rabbani Khalkhali vile vile katika kitabu; "Chehre Derakhshani Qamar Bani Hashim" amekusanya karama zipatazo 400 kutoka kwa Abbas (a.s). Yeye ameziwek kila ripoti 250 katika kila juzuu maalumu. Walakini tatizo lililopo ni kwamba, baadhi ya ripotii hizi zimesimuliwa mara mbali. Kwa mujibu wa vyanzo hivi, matokeo ya karama za bwana Abbas hayahusiani na matokeo kutoka kwa Mashia peke yao, bali pia karama hizo zimeripotiwa kutoka kwa waumini wa dini na madhehebu mengine tofauit, kama vile Sunni, Wakristo, Mayahudi (کلیمیین), na Wazoroastria. [123]

Abbas (a.s) Katika Mila na Tamaduni za Shia

Inajulikana wazi ya kwamba Mashia wana mapenzi na shauku kubwa kwa bwana Abbas (a.s). Wao wanamhisabu yeye kuwa ndiye mtu mwenye cheo cha juu zaidi baada ya Ma'asumina Kumi na nne (a.s). [124] Muhammad Baghdadi ameweka sura ya kitabu chake inayozungumzia uhusiano uliopo kati ya Mashia na Abul Fadhli (a.s)., na shauku ya mapenzi iliopo ndani ya nyoyo za Shia juu ya Abbas (a.s). Ambapo kwa mtazamo wake, jambo hilo liko wazi kabisa na kabisa mbele ya walimwengu. [125] Uhusiano huu umemfanya bwana Abbas kuwa na nafasi muhimu katika utamaduni wa Shia katika dua zao, pamoja na nembo mbali mbali zinazotumiwa kama ni alama maalumu katika tamaduni za Mashia.

Kuomba Dua Kupitia Hadhi ya Abbas Mbele ya Mungu

Kwa sababu ya nafasi maalum aliyonayo bwana Abbas miongoni mwa Mashia, watu hulitumia jia la Abbas katika dua zao na kumuomba Mungu awakidhie haja zao kwa baraka za bwana Abbas. [126] Baadhi pia wamenukuu karama kadhaa kutoka kwa bwana zilizoripotiwa kutoka kwa Masunni, Wakristo, Wayahudi na Waarmenia (Wakiristo wa kabila la Armenia).

Maombolezo ya Siku ya Tasua

Katika sherehe za kidini za muongo wa Muharram, tarehe 9 Muharram imetengwa kwa ajili ya maombolezo ya bwana Abbas (a.s). Ukiachana na ya siku ya mwezi 10 Muharram, ambayo ndiyo siku kubwa kuliko zote za majonzi na maombolezo ya Shia, ambapo mashia huadhimisha maombolezo yao misikitini, majumbani na katika majengo mengine ya ibada, mwezi 9 Muharram ndiyo siku inayochukua nafasi ya pili kwa ukubwa wa huzuni katika mwezi wa Muharram. Siku mbili hizi ni siku za mapumziko nchini Iran na baadhi ya nchi nyingine za Kiislamu. [128] Moja ya programu ambazo hufanyika kila mara katika maadhimisho na maombolezo hayo, ni usomaji wa mashairi ya kupitia mfumo maarufu ujulikanao kwa lugha ya Kiajemi kwa jina la "Doo Dame" (usomaji unaotegemea pumzi mbili) ambamo waombolezaji wa Hossein (a.s) hujigawa katika makundi mawili, kundi moja husoma. mshororo wa kwanza na kundi jingine husoma mshororo wa pili.

Tizama Pia: Enyi watu wa Jemedari na Mshika Bendera hajaja

Siku ya Al-Abbas (یوم العباس) huko Zanjan: Kila mwaka jioni ya siku ya mwezi 8 ya Muharram, umati mkubwa wa waombolezaji wa mji wa Zanjani hukusanyika kutea jengo la Husseinieh Azam (jengo la ibada) lililoko mjini Zanjan hadi kufikia jengo la Imamzadeh Sayyied Ibrahim. Hukusanyika katika eneo hilo na kuomboleza maombolezo kwa ajili ya tukio la Karbala. Kulingana na baadhi ya ripoti kuhusiana na mwaka 1369 Shamsia, ni kwamba; Zaidi ya kondoo 9,700 walichinjwa na kutolewa sadaka katika maadhimisho hayo. Zipoti za mwaka mwaka wa 1395 Shamsia nazo zimeashiria kuchinjwa kiasi cha kondoo 12,000 ambo wametolewa sadaka na watu mbali mbali. [130] Katika miaka ya hivi karibuni, takriban watu laki tano hushiriki katika maombolezo hiyo kila mwaka. Maadhimisho ya maombolezo hayo yanayofanyika mjini Zanjani, yamesajiliwa kama ni moja ya mambo ya urithi wa kiroho (kidini) ndani ya Iran. [131]

Uradi wa Yaa Kashifa Al-Karab (ذکر یا کاشف الکرب)

Uradi wa (یا کاشفَ الکَرْبِ عنْ وَجهِ الْحُسَین اِکْشِفْ کَرْبی بِحَقِّ أَخیکَ الحُسَین) "Ya Kashifa Al-karab an wajhi Al-Hussein", Ikshif karbiy bihaqqi akhiika Al-Husssein" ((Ewe mwenye kuondoa shida kutoka usoni mwa Hussein, niondolee shida yangu kwa baraka ya ndugu yako Hussein). Uradi huu najulikana kama moja ya nyiradi na dua kupitia baraka za bwana Abbas, na wakati mwingine uradi hupendekezwa ukaririwe mara 133, idadi ambayo ni idadi ya (jina la Abbas kwa mujibu wa hesabu ya Abjad. [132] Isipokua Hadithi hii haikutajwa katika vitabu vya Hadith vya Shia.

Mila na Nembo Nyingine

  • Kuzungusha bendera: bendera ni moja ya alama zinazotumika katika maadhimisho ya maombolezo ya Imamu Hussein (a.s). Bendera huwa ni nembo maalumu ya kumkumbuka bwana Abbas, mshika bendera wa Karbala. [133]
  • Saqqaai: Ni moja ya mila ya kusoma mashairi ya huzuni ambayo hufanyika katika masiku ya maombolezo, haswa Tasua (mwezi 9 Muharram) na Ashura (mwezi 10 Muharram) nchini Iran. Maadhimisho hayo wakati mwingine hufanyika kwa namna ya maombolezo ya pamoja, na wakati mwingine watu huwa wanawapa wengine maji kwa ajili ya kuzima kiu, watu ambao wapo katika eneo hilo la maombolezo hayo. Katika hali ya kwanza, huwa kuna mashairi na maombolezo maalum yanayosomwa. Na katika sura ya pili, Saqaai (mgawa maji) huvaa nguo maalum na kuwanywesha waombolezaji kwa mtungi au chombo maalumu kilichotengezwa kwa ngozi ya mnyama. [134] Washiriki wa timu ya wanyeshaji maji (Saqqaai), wanakuwa na alama (nembo) maalumu za kisaqqaai. Wanyweshaji hao mkono mmoja wanashikilia mdomo wa mtungi wa maji wanaoubeba, na mkono mwingine, hushikilia kibakuli. Huwa wanaenda na kurudi kati ya waombolezaji na kuwapa maji wenye kiu, hufanya hivyo huku wakisoma mashairi ya kukumbusha kiu ya Imamu Hussein (a.s) na masahaba zake. Lengo lao ni kuwafanya wanywao maji hayo wamkumbuke Imamu Hussein na Masahaba zake. Kwa mfano, wanyeshaji kitongoji cha Sarwistan kilioko mjini Shiraz, husoma mashairi haya: Kunywa maji na kumlaani Yazid na hiyo ndiyo haki yake/ Toa muhanga yako ili iwe ni muhanga wa kaburi la mfalme Mashahidi. [135] Utamaduni wa Saqqaai ni wa kawaida katika miji mingi ya Kishia ya Iraq pamoja na Iran, [ 136] na athari za utamaduni wa Saqqaai huonekana kwenye majengo mengi yaliojengwa kwa jina la bwana Abbas kwa ajili ya kutoa huduma ya kunywesha watu maji. [137]
  • Kuapa kwa jina la Abbas (a.s): Kuapa kwa jina la Abbas ni jambo la kawaida miongoni mwa Mashia na hata Masunni. Kwa mujibu wa nukuu za baadhi ya watu kadhaa ni kwamba; Mashia wengi wanaapa kwa jina la Abbas ili kumaliza ugomvi na uhasama wao. Na wengine wanaona kiapo pekee cha kweli huwa ni kiapo kwa jina la Abbas.[138] Baadhi ya makabila ya Shia yanathibitisha na kuyaunganisha maagano, mapatano, mikataba na mikataba yao kwa kuapa kwa jina Abbas (a.s) [139] Sababu ya maalum inayowafanya washikamane na kiapo cha Abbas (a.s), ni ujasiri, uaminifu, wivu wa kutetea haki, adabu, kuheshimu fadhila pamoja na uungwana aliokuwa nao Abbas (a.s).” [140] Kuna baadhi ya ripoti kuhusiana na imani ya Masunni katika kuamini kiapo cha jina la Abbas, hasa Masunni wa Iraq. Miongoni mwa ripoti kuhusiana jambo hilo ni nukuu ya Hardan Tikriti, Waziri wa zamani wa Ulinzi wa Iraq, amesema kuwa alikuwa pamoja na Ahmed Hassan Al-Bakr (mmoja wa marais wa zamani wa Iraq) na Saddam na wengine kadhaa. Katika jopo hilo walitaka kufanya makubaliano na kuimarisha makubaliano yao ili wasije kusalitiana, hivyo wakaamua kuapa. Ingawa baadhi yao walipendekeza kweda kwenye kaburi la Abu Hanifa, ila hatimaye waliamua kwenda kwenye kaburi la Abbas na kuapa katika eneo hilo.[141]
  • Karamu ya chakula cha Abu Alfadhli: Karamu au chakula cha nadhiri, ni aina ya karamu za Kishia zinazoadhimishwa na jamii ya wanawake. [142] Ambayo hufanyika kwa kutandaza karamu ya chakula na kufanya ibada ya kusoma dua maalum. Maadhimisho hayo ni Mojawapo ya maadhimisho muhimu ya karamu za Abu Al-Fadhli. [143]
  • Abbasiyyehaa au Bait Al-Abbas: Ni sehemu ambazo zimejengwa kwa jina la bwana Abbas (a.s) na kwa ajili ya maombolezo ya kifo chake. Baadhi pia wamesema kwamba programu nyingine nyingi pia huwa zinafanyika katika maeneo hayo, na matumizi yake ni sawa na matumizi ya Husseiniyeh (nyumba zilizojengwa kwa jina la Imamu Hussein. [144]
  • Siku ya Mashujaa: Katika kalenda rasmi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, siku ya mwezi nne ya Sha'ban, ambayo ni siku kuzaliwa kwa bwana Abbas (a.s), inatambulika kama Siku ya Mashujaa. [145]
  • Alama na nembo ya kiganja, ambayo hutumika katika baadhi ya maeneo ya Shia, huwekwa kwenye bendera kama ni nembo inayowakilisha ile mikono ya bwana Abbas iliyokatwa vitani Karbala. Baadhi ya Mashia wengine huitumia nembo hiyo kama ni alama inayowakilisha watu watano watukufu wa Aalu-Abba au Ahlul-Kisaa. [146]

Maeneo na Majengo Yanayo Husiana na Abbas (a.s)

Kaburi Bwana Abbas lilojengewa mwaka 1395.

Kuna majengo na maeneo mengi nchini Iran na Iraq yanayoheshimiwa na watu kwa muda wa miaka nenda na mika rudi. Kwa kawaida watu huenda hapo kwa ajili ya kulipa nadhiri na kutoa sadaka zao. Watu wengi wanaamani ya kwamba iwapo watamuomba Mola wao kupitia jina na baraka za Abbas, basi bila shaka matilaba yao yatakamilishwa.

Kaburi la Hazrat Abbas (a.s)

Makala Asili: Kaburi la Abul-Fadhl al-Abbas (a.s)

Kaburi la Abbas lipo katika mji wa Karbala, kiasi cha mita 378 kaskazini mashariki mwa kaburi la Imam Hussein (a.s). Eneo hilo ni moja ya maeneo muhimu ya yanayotembelewa na Mashia, kwa nia ya kulizuru kaburi la bwana Abbas. Eneo la kati lililopo baina ya kaburi la bwana Abbas na kaburi la Imam Hussein (a.s) linatambulikana kwa lugha ya Kiarabu kwa jina la (بین الحرمین), yaani eneo baina ya makaburi mawili matukufu. [147] Kwa mtazamo wa wanahistoria wengi, Abbas (a.s) alizikwa kwenye sehemu aliyofia kishahidi juu yake, ambayo ni kando ya mto Alqamah. [148] Mtazamo huo unatokana na imani ya kihistoria ya kwamba; Imamu Hussein (a.s) hakuondoa mwili wa bwana Abbas na kuuweka pamoja na mashahidi wengi, bali aliuwacha katika eneo lile lile aliofariki juu yake. [148]

Baadhi ya waandishi kama vile Abdul Razzaq Muqarram wanaamini ya kwamba; Yawezekana sababu iliyomfanya Imamu Hussein (a.s) ni yeye kutaka ndugu yake awe sehemu maalumu ya kaburi takatifu. Na si kwamba hakuuchukuwa mwili wa bwana Abbas na kuupeleka kwenye hema, inatokana na ombi la bwana Abbas mwenyewe, au inatokana na Imamu Hussein (a.s) kushindwa kuuhamisha mwili wa Abbas kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye mwili wake. [149] Muqram hakutaja nyaraka zozote za kauli yake. Ila Abdul Razzaq Muqarram hakutoa ithibati zozote zile kuhusiana na madai yake hayo.

Eneo Takatifu la Kiganja cha Abbas (مقام کف العباس)

Eneo takatifu la kiganja cha Abbas
Makala Kuu: Kiganja cha Abbas

Maqam Kaf Al-Abbas (مقام کف العباس) ni jina la sehemu mbili ambazo inasemekana kwamba hayo ndiyo maeneo ambayo mikono ya bwana Abbas (a.s) ilitenganishwa na mwili wake na kuanguka chini ya maeneo hayo. Maeneo hayo mawili yapo kaskazini-mashariki na kusini-mashariki nje ya kaburi la bwana Abbas (a.s) kwenye mlango wa vichochoro viwili vinavyokabilia na soko. Kwenye maeneo hayo kuna nembo mbili zimetengenezwa kwa ajili ya kuashiria maeneo na wenye kwenda kufanya ziara huwa maeneo hayo. [150]

Alama ya Mguu na Vituo vya Maji

Kuna alama mbalimbali za miguu nchini Iran yaliyopewa inayonasibiswa na Abbas. Kila mara watu huenda kwenye sehemu zenye alama hizo ili kulipa nadhiri zao na kuomba mahitaji yao na kufanya shughuli zao nyingine za kidini katika maeneo hayo. [151] Miongoni mwa miji abayo ni mashuri yenye alama hizo ni Bushehr na Shiraz. [152] Kwa mujibu wa kauli ya Khalkhali, katika mjini wa Lar kuna eneo lenye alama inayonasibishwa na Abbas, ambapo Masunni wa eneo hilo huenda huko kila Jumanne pamoja na familia zao kuomba mahitaji yao na kutoa nadhiri katika eneo hilo. [153]

  • Saqaqhana: Ni moja ya nembo za kidini za Mashia, nayo ni sehemu ndogo inayojengwa katika sehemu zenye mapito ya watu. Sehemu hizo mara nyingi hujengwa kwenye mapito makuu ya watu, kama vile barabara za umma ili kuwapa maji wapita njia kwa nia ya kupata thawabu. Katika utamaduni wa Shia, sehemu hizo huwa ni ukumbusho wa kifo cha bwana Abbas (a.s) katika tukio la Karbala. Kwa hiyo sehemu hiyo ya kunywea maji hupambwa kwa maandishi ya jina la Imam Hussein (a.s) na Abbas (a.s). watu wengine huwasha mishumaa katika sehemu hiyo wakitaraji kupata maombi yao, wengine nao hufunga kitambaa kwa dhana ya kukidhiwa haja zao. [155] Kuna vibabda vyingi vya maji vilivyojengwa katika sehemu mbalimbali duniani viliyopewa jina la Abbas. [156]
  • Saqqanifar: au Saqinifar au Saqaataalar ni jina la majengo ya kitamaduni katika eneo la Mazandarani nchini Iran, majengo ambayo hutumika kwa ajili ya kuadhimisha shughuli za maombolezo na kuweka nadhiri. Majengo haya kwa ujumla hujengwa karibu na sehemu za kidini, kama vile msikiti, zawiya au huseiniyyah. Saqanfar huhusishwa na bwana Abbas (a.s) na wengine huziita kwa jina la "Abul Fadhliy". [157]

Michoro Inayo Nasibishwa na Sura ya Abbas

Picha ya sura maarufu ya Abbas (a.s) iliyotumika katika filamu

Kuna michoro kadhaa katika jumla ya utamaduni wa Mashia inayojulikana kama picha ya uso wa Abbas bin Ali. Picha hizo pia hutumiwa vikundi vinavyoshughilia harakati za uombolezaji. Wengi miongoni mwa wanazuoni hawaafikiani uhalisia wa michoro hiyo. Kwa mtazamo wa wazuoni wa Kishia ni kwamba, iwapo picha hizo zitakuwa hazidhalilishi na kuvunja heshima ya Abbas bin Ali (a.s), basi hakutakuwa na tatizo kutumia picha na michoro hiyo, ila wamesisitiza kuachana na kutumia picha hizo. [158]

Katika miaka ya hivi karibuni, filamu mbili zilitengenezwa zikizingatia tukio la Ashura, ambazo ni; Mukhtarnameh na Rastakhiz, sehemu zinazohusiana na bwana Abbas katika filamu ya Mukhtarnameh ziliondolewa kutokana na kutowafikiana na maoni ya wa baadhi ya wanazuozi ya kuto juzu kuonyesha uso wa bwana Abbas. [159] Pia filamu ya Rastakhiz haikupata ruhusa ya kuoneshwa kwa sababu hiy hiyo. [160] [Maelezo 3]

Orodha ya Vitabu Husika

Kuna vitabu kadhaa vilivyondikwa kuhusiana na wasifu wa bwana Abbas (a.s), baadhi yake ni:

  1. Kitabu kuhusu Maisha ya Qamar Bani Hashem (bwana Abbas), chenye jina la Dhuhuri 'Ishqi 'Ali, kilichoandikwa na, Hossein Badruddin, Chapa ya Tehran, Taasisi ya Mehtab, 1382 Shamsia.
  2. Saqi Khoban: Kitabu kuhusiana na wasifu wa bwana Abulfadhli Al-Abbas, kilichoandikwa na Mohammad Chaqai Araki, Qom, Kitengo cha Uchapishaji cha Mortaza, 1376 Shamsia.
  3. Zindegi Hazrat Abulfazl Al-Abbas Alamdar Karbala, cha Redha Dashti, Tehran, Taasisi ya Paazineh, mwaka 1382 Shamsia.
  4. Chehre Derakhshani Qamar Bani Hashim Abulfadhli Al-Abbas, cha Ali Rabbani Khalkhali, Qom, Taasisi ya uchapishaji ya Al-Hussein, 1378 Shamsia, kimechapwa katika Juzuu 3.
  5. Abu Al-Qirbah: Ni kitabu kinachohusiana na Wasifu wa bwana Abu Al-Fadhli (a.s), kilichoandikwa na Majid Zujaaji Mujarrad Kaashani, Chapa ya Tehran, Subhan, 1379 Shamsia.
  6. Abbas (a.s) Sepah Saalaare Karbala: kimeandikwa kuhusu Wasifu wa Abbas (a.s) kimeandikwa na Shabgahi Shabestri, Chapa ya Tehran ya Taasisi ya Harufiyeh, 1381 Shamsia.
  7. Abbas bin Ali (a.s), kilichoandikwa na Javad Mohaddithiy, toleo la 9 la mkusanyiko wa makala ya Ashenaye ba Uswah, Chapa ya Taasisi ya Bostan Ketab Qom, toleo la 8, 1393 Shamsia. [161]
  8. Abul Fadhli Al-Abbas (a.s): Kitabu kuhusu utafiti juu ya maisha na wasifu wa Abbas bin Ali (a.s), kilichoandikwa na Javad Khormaian, Chapa ya Rahe Sabz, chapa ya kwanza, 1386 Shamsia.

Rejea

  1. Baghdadi, al-Abbas, 1433 AH, uk. 73-75; Mahmoudi, Mahe Bi-Ghurub, 1379 S, uk. 38.
  2. Mahdawi, ‘Ighlam Isfahan, 1386 S, juz. 1, uk. 110.

Vyanzo

  • Abū l-Faraj al-Iṣfahānī, ʿAlī b. al-Ḥusayn. Maqātil al-ṭālibīyyīn. Beirut: Muʿasisat al-Aʿlamī li-l-Maṭbūʿāt, 1408 AH.
  • Abū Mikhnaf, Lūṭ b. Yaḥyā. Waqʿat al-ṭaf. Edited by Hādī Yūsifī Gharawī. Qom: Majmaʿ Jahānī Ahl al-Bayt, 1433 AH.
  • Amīn, Sayyid Muhsin al-. Aʿyān al-shīʿa. Beirut: Dār al-Taʿāruf, 1406 AH.
  • Baghdādī, Muḥammad b. Ḥabīb al-. Al-Muḥabbar. Beirut: Manshūrāt Dār al-Āfāq al-Jadīda, [n.d].
  • Balādhurī, Aḥmad b. Yaḥyā al-. Ansāb al-ashrāf. Edited by Suhayl Zaka. Beirut: Dār al-Fikr, 1417 AH.
  • Bīrjandī, Muḥammad Bāqir. Kibrīt al-aḥmar. Tehran: Kitāb Furūshī-yi Islāmīyya, 1377 Sh.
  • Ḥillī, Jaʿfar b. Muḥammad al-. Muthīr al-aḥzān. Translated to Farsi by ʿAlī Karamī. Qom: Nashr-i Ḥādhiq, 1380 Sh.
  • Ibn Aʿtham al-Kūfī. Al-Futūḥ. Edited by ʿAli Shīrī. Beirut: Dār al-Aḍwāʾ, 1411 AH.
  • Ibn Qūlawayh, Jaʿfar b. Muḥammad. Kāmil al-zīyārat. Tehran: Payām-i Ḥaqq, 1377 Sh.
  • Ibn Shahrāshūb, Muḥammad b. ʿAlī. Manāqib Āl Abī Ṭālib. Najaf: Maṭbaʿat al-Ḥaydaīyya, 1376 AH.
  • Khwārizmī, Muwaffaq b. Aḥmad al-. Maqtal al-Ḥusayn. Edited by Muhamad al-Samāwī. Qom: Anwār al-Hudā, 1418 AH.
  • Majlisī, Muḥammad Bāqir al-. Biḥār al-anwār li durar akhbar al-aʾimma al-aṭhār. Beirut: Muʾassisat al-Wafāʾ, 1403 AH.
  • Māzandarānī, Muḥammad Mahdī. Maʿalī l-sibtayn. Beirut: Muʿasisat al-Nuʿmān, 1412 AH.
  • Mufīd, Muḥammad b. Muḥammad -al. Al-Irshād. Edited by Saʿid b. Jubayr. Qom: [n.p], 1428 AH.
  • Mufid, Muhammad b. Muhammad -al. Al-Irshad. Translated to Farsi by Ḥasan Mūsawī Mujāb. Qom: Surūr, 1388 Sh.
  • Muqarram, ʿAbd al-Razāq al-. Hādisi-yi Karbala dar maqtal-i muqarram. Translated to Farsi by Muhammad Jawad Mulaʾīnīya. Qom: Jilwa-yi Kamāl, 1387 Sh.
  • Muzaffar, ʿAbd al-Wāhid b. Aḥmad al-. Baṭl al-ʿalqamī. Najaf: al-Maṭbaʿa al-Haydarīyya, [n.p].
  • Nāṣirī, Muḥammad ʿAlī al-. Mawlid al-ʿAbbās b. ʿAlī Qom: Sharīf al-Raḍī, 1372 Sh.
  • Pīshwāyī, Mahdī. Maqtal-i jamiʿ-i Sayyid al-shuhadāʾ. Qom: Muʾasisa-yi Amūzishī Pazhūhishī-yi Imām Khomeini, 1390 Sh.
  • Qummī, ʿAbbās. Nafas al-mahmūm. Qom: Hijrat, 1376 Sh.
  • Rabbānī Khalkhālī, ʿAlī. Chihra-yi dirakhshān-i qamar-i banī hāshim al-ʿAbbās. Qom: Makab al-Ḥusayn, 1378 Sh.
  • Ṣadūq, Muḥammad b. ʿAlī al-. Al-Khiṣāl. Edited by ʿAlī Akbar Ghaffārī. Beirut: Muʿasisat al-Aʿlamī li-l Maṭbūʿāt, [n.d].
  • Sibt b. al-Jawzī. Tadhkirat al-khawāṣ. Edited by Ḥusayn Taqīzāda. Tehran: al-Majmaʿ al-ʿĀlamī li-Ahl al-Bayt, 1426 AH.
  • Ṭabarī, Muḥammad b. Jarīr al-. Tārīkh al-umam wa l-mulūk. Edited by Muḥammad Abū l-Faḍl Ibrāhīm. Beirut: [n.p], 1382 AH.
  • Tabrisi, Faḍl b. al-Ḥasan al-. Iʿlām al-wara bi-aʿlām al-hudā. Qom: [n.p], 1417 AH.
  • Zubayrī, Musʿab b. ʿAbd al-. Nasab Quraysh. Beirut: Dār al-Maʿārif li-l-Maṭbūʿāt, 1953.