Dua ya thelathini na nane (38) ya kitabu cha Sahifa Sajjadiyya
Dua ya thelathini na nane (38) ya kitabu cha Sahifa Sajjadiyya: ni miongoni mwa dua zilizopekea kutoka kwa Imamu Ali bin al-Hussein Zain al-Abidin (a.s). Madhumuni ya dua hii ni kuwasilisha toba kwa mapungufu yaliyojitokeza katika utekelezaji wa haki za watu mbali mbali (kwa Kiarabu: huquq al-nas), na kuomba ukombozi kutokana na adhabu ya moto wa Jahannam. Lengo kuu la Imamu (a.s) katika dua hii, ni kuomba radhi kwa yafuatayo: kutothamini na kutoonesha shukrani kwa hisani alizotendewa na wengine; kushindwa kumtetea mja aliyedhulumiwa mbele ya umma (mbele yake); kutowapa kipaumbele wenye shida walioomba usaidizi, na badala yake kutanguliza mahitaji binafsi; kutostiri aibu na mapungufu ya wanadamu wengine; kutokubali ombi la msamaha aliloombwa na wengine; na uzembe wa jumla katika kutimiza wajibu na haki za watu.
Dua ya Thelathini na Nane ya Sahifa Sajjadiya imeshereshwa (imefasiriwa na kufafanuliwa) katika vitabu mbalimbali vilivyofasiri dua za kitabu cha Sahifa Sajjadiyya kupitia lugha tofauti. Miongoni mwa tafsiri fafanuzi hizo zilizofanya kazi yake kwa lugha ya Kifarsi (Kiajemi), ni kitabu kiitwacho 'Shuhud wa Shenakht', kilichoandikwa na Hassan Mamduhi Kermanshahi. Ama kitabu maarufu katika kazi hiyo kilichoandikwa lugha ya Kiarabu, ni kitabu kijulikanacho kwa jina la 'Riyad as-Salikin', kazi maridadi ya Sayyid Ali-Khan Madani. Katika dua ya thelathini na nane ya Sahifa Sajjadiyya, Imamu Sajjad (a.s), anawasilisha ombi la msamaha kwa Mola wake kutokana na mapungufu yanayotokea katika utekelezaji wa haki za binadamu (Haqq al-Nas). Aidha, anabainisha nukta za msingi kuhusu mienendo bora ya mahusiano ya kijamii. [1] Mafundisho ya dua hii yameorodheshwa katika vipengele vifuatavyo: • Umuhimu wa kuwalinda na kuwatetea watu wanaodhulumiwa na kunyanyaswa. • Umuhimu wa kutoa shukrani kwa wahisani na watenda wema. • Umuhimu wa kukubali maombi ya msamaha kutoka kwa wengine. • Uhalifu (uharamu) wa kuanika siri za wenza wa kiitikadi. • Ulazima wa kuzuia vitendo viovu katika mazingira ya uasi (vikao vinavyoasiwa Mungu ndani yake). • Umuhimu wa kutekeleza wajibu wa kuwapa wengine stahiki zao bila kuchelewa. • Uombaji radhi wa kweli kutokana na kosa fulani, hujumuisha kujifunza kutokana na kosa hilo na kuahidi kutolirudia utendaji wa kosa hilo. • Ulazima wa kukidhi mahitaji na maombi ya watu wengine (kwa kadiri ya uwezo wako). • Kuomba kuwezeshwa kufanya maamuzi madhubuti ya kuachana na vitendo vya dhambi. • Kuomba toba ya kweli (taubatu al-nasuha), itakayosababisha kupata upendo na radhi mbele za Mwenye Ezi Mungu. • Kumuomba Mwenye Ezi Mungu aipandikize hisia ya kuchukia dhambi moyoni mwa Wake, baada ya mja huyo kutubia dhambi zake. • Uhakika wa kwamba; Mwenye Ezi Mungu anawapenda wenye kutubia (At-Tawwabina). • Dhana ya Toba ianajumuisha mchakato wa kujutia makosa ya awali na kuwa tayari kupambana na vishawishi vya makosa yajayo. [2] Tafsiri Chambuzi za Dua ya Thalathini na Nane Kuna kazi nyingi zilizoandikwa kwa lugha mbali mbali kwa ajili ya kutoa tafsiri sahihi za Dua ya thelathini na nane sambamba na dua nyengine za kitabu cha Sahifa Sajjadiya. Miongoni mwa kazi zilizoandikwa kwa lugha ya Kifarsi, ni ile inayopatikana katika kitabu kiitwacho Shuhud wa Shenakht, kilichoandikwa na mwanachuoni aitwaye Mohammad-Hasan Mamduhi Kermanshahi, [3] pamoja na kitabu kiitwacho Sharh wa Tarjomeh Sahifa Sajjadiya, kazi ya Sayyid Ahmad Fehri. [4] Aidha kuna wanazuoni kadhaa wilijitahidi kuichambua Dua hii sambamba na dua nyengine za Sahifa Sajjadiyya kwa lugha ya Kiarabu, ili kuwarahisishia waumini ufahamu na welewa wa dua hizo. Miongoni mwa wanazuoni waliutmia muda wao kwa ajili ya kazi hiyo ni pamoja na; Maulana Sayyid Ali Khan Madani katika kitabu chake Riadhu as-Salikin, [5] Sheikh Muhammad Jawad Mughniyyah katika kitabu chake Fi Dhilali as-Sahifat as-Sajjadiyya, [6] Muhammad bin Muhammad Darabi katika kitabu chake Riyadh al-Arifin, [7] na Sayyid Muhammad Hussein Fadhlullah katika kitabu chake kiitwacho Afaq al-Ruh. [8] Vilevile, kuna baadhi ya wanazuoni waliofanya kazi ya kutoa maana za maneno na msamiati wa dua hii sambamba na dua nyengine za Sahifa Sajjadiyya, wakiuchambua msamiati wake kutpitia mfumo wa kilugha. Miongo mwa vitabu vilitomikia kazi hiyo ni kama vile; Ta'aliqat 'ala as-Sahifat as-Sajjadiyya, kazi ya Mwanazuoni ajulikanaye kwa jina la Faidhu Kashani, [9] na Sharhu as-Sahifat as-Sajjadiyya, kazi ya Sheikh Izzu al-Din al-Jaza'iri. [10] Matini ya Kiarabu na Maelezo ya Kiswahili ya Dua ya Thalathini na Nane
وَ كَانَ مِنْ دُعَائِهِ عَلَيْهِ السَّلَامُ فِي الِاعْتِذَارِ مِنْ تَبِعَاتِ الْعِبَادِ وَ مِنَ التَّقْصِيرِ فِي حُقُوقِهِمْ وَ فِي فَكَاكِ رَقَبَتِهِ مِنَ النَّارِ Na miongoni mwa dua zake (amani iwe juu yake) ilikuwa ni ile aliyoitumia katika kuomba radhi kutokana na madhara ya dhima zitokanazo na haki za watu, mapungufu yatokanayo na majukumu ya kuwatekelezea haki zao, pamaoja kuomba ukombozi wa kuikomboa nafsi yake kutokana na Moto wa Jahannam. اللَّهُمَّ إِنِّي أَعْتَذِرُ إِلَيْكَ مِنْ مَظْلُومٍ ظُلِمَ بِحَضْرَتِي فَلَمْ أَنْصُرْهُ، وَ مِنْ مَعْرُوفٍ أُسْدِيَ إِلَيَّ فَلَمْ أَشْكُرْهُ، وَ مِنْ مُسِيءٍ اعْتَذَرَ إِلَيَّ فَلَمْ أَعْذِرْهُ، وَ مِنْ ذِي فَاقَةٍ سَأَلَنِي فَلَمْ أُوثِرْهُ، وَ مِنْ حَقِّ ذِي حَقٍّ لَزِمَنِي لِمُؤْمِنٍ فَلَمْ أُوَفِّرْهُ، وَ مِنْ عَيْبِ مُؤْمِنٍ ظَهَرَ لِي فَلَمْ أَسْتُرْهُ، وَ مِنْ كُلِّ إِثْمٍ عَرَضَ لِي فَلَمْ أَهْجُرْهُ.
Ewe Mola, ninawasilisha kwako maombi yangu ya msamaha: kutokana na haki ya mnyonge aliyekandamizwa mbele yangu, nami nikashindwa kumnusuru (mnyonge huyo), na (ninaomba mshamaha Wako) kutokana na fadhila nilizotendewa, nami nikaacha kutoa shukrani (juu ya fadhila hizo), na kutokana na mkosaji aliyewasilisha kwangu maombi ya kunitaka radhi, nami nikakataa kumpa msamaha, na kwa yule mwenye uhitaji aliyenielekezea ombi lake, nami nikashindwa kumfadhilisha (mtanguliza yeye) badala ya nafsi yangu, na kutokana na ile haki ya muumini ambayo ilikuwa ni wajibu wangu (kuitekeleza haki hiyo), nami nikazembea katika kuitekeleza kikamilifu,na (ninaomba mshamaha Wako) kwa dosari (aibu) ya muumini fulani iliyonidhihirikia, nami nikaacha kuisitiri, na kwa kila tendo la uasi lililojitokeza mbele yangu, nami nikashindwa kuliepuka. أَعْتَذِرُ إِلَيْكَ -يَا إِلَهِي- مِنْهُنَّ وَ مِنْ نَظَائِرِهِنَّ اعْتِذَارَ نَدَامَةٍ يَكُونُ وَاعِظاً لِمَا بَيْنَ يَدَيَّ مِنْ أَشْبَاهِهِنَّ.
Ewe Mungu wangu, nakuomba msamaha kutokana na makosa hayo na yale yanayofanana nayo. Ni msamaha (ni toba) unaotokana na majuto ya kweli, ambao utakuwa onyo (somo) kwangu dhidi ya makosa kama hayo katika siku za usoni.
فَصَلِّ عَلَى مُحَمَّدٍ وَ آلِهِ، وَ اجْعَلْ نَدَامَتِي عَلَى مَا وَقَعْتُ فِيهِ مِنَ الزَّلَّاتِ، وَ عَزْمِي عَلَى تَرْكِ مَا يَعْرِضُ لِي مِنَ السَّيِّئَاتِ، تَوْبَةً تُوجِبُ لِي مَحَبَّتَكَ، يَا مُحِبَّ التَّوَّابِينَ.
Hivyo basi, mrehemu (mbariki) Muhammad na Aali zake. Na ijaalie nadama yangu juu ya mapungufu (makosa) niliyoangukia ndani yake, pamoja na dhamira yangu madhubuti ya kuviacha vitendo viovu vinavyojitokeza mbele yangu, kuwa ni nadama (toba) itakayonihakikishia upendo Wako, Ewe Mwenye kuwathamini wanaorejea Kwako.