Nenda kwa yaliyomo

Dua ya Nadi Ali

Kutoka wikishia
Dua ya Nadi Ali
LughaKiarabu
MadaUbainishaji wa sifa na fadhila za Imam Ali (a.s).
ChanzoMisbah Kaf'ami • Zad al-Ma'ad


Dua ya Nadi Ali (Kiarabu: دعاء ناد عليا مظهر العجائب) ni anuani ya dua mbili zinazotoa wasifu wa Imam Ali (as) na ambayo inaanza na ibara isemayo: «نادِ عَلِياً مَظهَرَ [أو مُظهِرَ] العَجائِب» (muite Ali! Mwenye kudhihirisha maajabu. Inaelezwa kuwa, ilikuwa ni katika vita vya Uhud wakati, Mtume (s.a.w.w) aliponong'onezwa dua hii katika masikio yake na ulimwengu wa ghaibu.

Dua ya Nadi Ali Swaghir ni fupi na inaelezwa kuwa, inaondoa kila huzuni na ghamu kwa baraka za Utume wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Wilaya (uongozi) wa Imama Ali (a.s), Allama Majlisi amenukuu na kuileta dua hii katika kitabu chake cha Bihar al-Anwar, hata hivyo hakuashiria chanzo chake. Hata hivyo Yadullah Duzduzani, fakihi wa Kishia, amesema kuwa, Dua ya Nadi Ali Swaghir haina nyaraka za kuaminika ili kuifanya iwe na itibari. Pamoja na hayo, kumeandikwa vitabu vya kutoa ufafanuzi na maelezo kuhusiana na dua hii.

Dua ya Nadi Ali Kabir nayo ina madhumuni na maana inayoshabihiana na Dua ya Nadi Ali Swaghir; hata hivyo ukubwa wake ni mara kadhaa ya Dua ya Nadi Ali Swaghir.

Dua ya Nadi Ali Swaghir

Kwa mujibu wa kile kilichokuja katika ufafanuzi wa diwani ya mashairi inayonasibishwa na Imam Ali (a.s) iliyoandikwa na Maybudi Yazdi, alimu na msomi wa Kishafii wa karne ya 10 Hijria ni kwamba, Mtume (s.a.w.w) alisikia hivi katika vita vya Uhud kutoka kwa ulimwengu wa Ghaibu: «نَادِ عَلِيّاً مَظْهَرَ الْعَجَائِبِ، تَجِدْهُ عَوْناً لَكَ فِي النَّوَائِبِ، كُلُّ هَمٍّ وَ غَمٍّ سَيَنْجَلِي، بِوَلايَتِكَ يَا عَلِيُّ»[1] Maneno haya yana nyongeza katika kitabu cha Farhang Ghadir kilichoandikwa na Jawad Muhaddithi: «نَادِ عَلِيّاً مَظْهَرَ الْعَجَائِبِ، تَجِدْهُ عَوْناً لَكَ فِي النَّوَائِبِ، كُلُّ هَمٍّ وَ غَمٍّ سَيَنْجَلِي، بِنُبُوَّتِکَ یا مُحَمَّد، بِوَلايَتِكَ يَا عَلِيُّ ; Muite Ali, mwenye kudhihirisha maajabu, utampata ni mwenye kukusaidia katika mazonge au matatiizo yako; kila huzuni na ghamu inaondoka kwa baraka za Utume wako Ewe Muhammad, na kwa Wilaya (uongozi) wa Ali!».[2]

Allama Majlisi katika kitabu chake cha Bihar al-Anwar na Mirza Muhammad Taqi Sepehr katika kitabu chake cha Nasikh al-Tawarikh wameashiria hadithi na riwaya ya Maybudi Yazdi.[3] Hata hivyo katiika kitabu cha Bihar al-Awnar hakujaashiriwa chanzo cha dua hii.[4] Yadullah Duzduzani, mmoja wa mafakihi wa Kishia wa karne ya 15 Hijria, licha ya kuwa ametambua kuwa, kusoma dhikri na dua hii kwa ajiili ya matarajio ya thawabu hakuna tatizo, lakini ameeleza kwamba, hakuna nyaraka na hoja yenye itibari kuhusu hili.[5]

Taqi al-Din Ibrahim al-Kaf’ami, mwanazuoni wa Kishia wa karne ya 15 Hijria anasema katika kitabu chake cha Misbah kwamba aliona kipengee tajwa kikiwa na hati ya al-Shahid al-Awwal na anaongeza kusema kwamba, kilikuwa kikisomwa na kukaririwa ili kupata kitu kilichopotea na mtumwa aliyekimbia.[6] Muhaddith Nuri amenukuu katika kitabu chake cha Mustadrak al-Wasail nukta hii hii.[7] Allama Sayyid Muhammad Hussein Husseini Tehrani amenukuu kutoka kwa marehemu Sayyid Hashim Haddad ya kwamba, kila ambaye atasoma dua hii kila siku mara 110: «نادِ علیًّا مَظهَرَ العجائبَ، تَجِدْهُ عَونًا لکَ فی النَّوائب، کُلُّ همٍّ و غمٍّ سَیَنجَلی، بعَظَمَتِکَ یا اللَهُ، بِنُبوَّتِکَ یا محمّد، بولایتکَ یا علیُّ یا علیُّ یا علیّ» na akadumisha usomaji huu kwa muda wa siku tatu mfululizo, basi Mwenyezi Mungu atamjibu kila haja atakayomuomba.[8]

Dua ya Nadi Ali imeandikwa ikiwa na mabadiliko kidogo katika sentensi ya mwisho katika msikiti mkuu wa Bijapur (Vijayapur) kusini mwa India.[9] Sehemu iliyotajwa yenye tofauti ni: ، بِنُبوَّتِکَ یا محمّد، بولایتکَ یا علیُّ یا علیُّ یا علیّ»,[10] Ibara hii imendikwa pia katika ngome ya Ahmadnagar India na inaonekana kwa umbo la simba[11]

Mashairi ya Kifarsi

Washairi na malenga kadhaa wa Kifarsi wameashiria katika athari zao dua ya Nadi Ali Swaghir; miongoni mwao ni Mirza Muhammad Taqi mashuhuri kwa jina la Tabrizi.[12] Mshairi mwingine aliyeashiria hili ambaye jina lake halifahamiki alisema hivi katika baadhi ya beti zake za mashairi:[13]

Katika madhehebu yetu maneno ya haki ni Nadi Ali
Twaa na ibada ilipokubaliwa na Mungu ilikuwa Nadi Ali

Nadi Ali Kabir

Tuliashiria mwanzoni mwa makala hii kwamba, Nadi Ali ni anuani ya dua mbili ambazo ni Nadi Ali Swaghir na Nadi Ali Kabir. Nadi Ali Swaghir kama tulivyoashiria na ambayo ndio mashuhuri zaidi yenyewe ni fupi. Lakini kuna Nadi Ali Kabiri ambayo ni ndefu. Allama Majlisi amenukuu na kuleta maandiko ya dua kamili ya Nadi Ali Kabir katika kitabu chake cha Zad al-Ma’ad.[14]

Dua kamili ya Nadi Ali Kabir ni:

بِسمِ اللهِ الرَّحمن الرَّحیم
نَادِ عَلِيّاً مَظْهَرَ الْعَجَائِبِ تَجِدْهُ عَوْناً لَكَ فِي النَّوَائِبِ لِي إِلَى اللهِ حَاجَتِي وَعَلَيْهِ مُعَوَّلِي كُلَّمَا رَمْيَتُهُ وَرَمَيْتَ مُقْتَضَی كُلِّ هَمٍّ وَغَمٍّ سَيَنْجَلِي بِعَظَمَتِكَ يَا اللهُ وَبِنُبُوَّتِكَ يَا مُحَمَّدُ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَ آلِهِ وَ سَلَّمَ وَبِوَلَايَتِكَ يَا عَلِيُّ يَا عَلِيُّ يَا عَلِيُّ أَدْرِكْنِي بِحَقِّ لُطْفِكَ الْخَفِيِّ، اللهُ أَكْبَرُ اللهُ أَكْبَرُ اللهُ أَكْبَرُ أَنَا مِنْ شَرِّ أَعْدَائِكَ بَرِي‌ءٌ بَرِي‌ءٌ بَرِي‌ءٌ اللهُ صَمَدِي بِحَقِّ إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ يَا أَبَا الْغَيْثِ أَغِثْنِي يَا عَلِيُّ أَدْرِكْنِي يَا قَاهِرَ الْعَدُوِّ وَيَا وَالِيَ الْوَلِيِّ يَا مَظْهَرَ الْعَجَائِبِ يَا مُرْتَضَى عَلِيُّ يَا قَهَّارُ تَقَهَّرْتَ بِالْقَهْرِ وَالْقَهْرُ فِي قَهْرِ قَهْرِكَ يَا قَهَّارُ يَا ذَا الْبَطْشِ الشَّدِيدِ أَنْتَ الْقَاهِرُ الْجَبَّارُ الْمُهْلِكُ الْمُنْتَقِمُ الْقَوِيُّ وَ الَّذِي لَا يُطَاقُ انْتِقَامُهُ وَأُفَوِّضُ أَمْرِي إِلَى اللهِ إِنَّ اللهَ بَصِيرٌ بِالْعِبَادِ وَإِلَهُكُمْ إِلَهٌ وَاحِدٌ لَا إِلَهَ إِلَّا هُوَ الرَّحْمَنُ الرَّحِيمُ حَسْبِيَ اللهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ نِعْمَ الْمَوْلَى وَنِعْمَ النَّصِيرُ يَا غِيَاثَ الْمُسْتَغِيثِينَ أَغِثْنِي يَا رَاحِمَ الْمَسَاكِينِ ارْحَمْنِي يَا عَلِيُّ وَأَدْرِكْنِي يَا عَلِيُّ أَدْرِكْنِي يَا عَلِيُّ أَدْرِكْنِي بِرَحْمَتِكَ يَا أَرْحَمَ الرَّاحِمِينَ.[15]










Athari Zinazohusiana

Kumeandika makala na vitabu mbalimbali kuhusiana na dua ya Nadi Ali ambavyo vinabainisha sifa maalumu za dua hii’. Mmiongoni mwa athari hizo ni kitabu cha Kifarsi chenye anuani ya “Nadi Aliyan Madh’har al-Ajaaib…” ambacho kinapatikana katika makataba ya Mar’ashi Najafi katika mji wa Qom, Iran.[16]

Kadhalika Ali Sadrai Khui, ameashiria katika kitabu chake nakala za hati ya mkono za hadithi na elimu ya hadithi orodha ya vitabu vilivyotoa ufafanuzi wa dua ya “Nadi Aliyann Madh’har al-Ajaaib”.[17]

Rejea

  1. Mibodi Yazdi, Sherh Diwan Mansub Be Amir al-Mu'minin Ali ibn Abi Talib, Uhariri: Akram Shafa'i, uk. 434.
  2. Muhadithi, Farhange al-Ghadir, 1386 S, uk. 563.
  3. Allamah Majlisi, Bihar al-Anwar, 1403 AH, juz. 20, uk. 73; Sepahar, Nasikh al-Tawarikh, 1385 S, juz. 2, uk. 902.
  4. Allamah Majlisi, Bihar al-Anwar, 1403 AH, juz. 20, uk. 73
  5. Duzduzani Tabrizi, Istifta'at Hadhrat Ayatullah al-Udhma Duzduzani Tabrizi, 1379 AH, uk. 22.
  6. Kaf'ami, Misbah, Nashr Dar al-Ridha, uk. 183.
  7. Nouri, Mustadrak al-Wasa'il, 1408 AH, juz. 15, uk. 483.
  8. Husseini Tehrani, Sayyid Muhammad Hussein, Matlai al-Anwar, juz. 2, uk. 155
  9. Tarihi, Tarikh al-Shia Fi al-Hindi, 1427 AH, juz. 2, uk. 117.
  10. Tarihi, Tarikh al-Shia Fi al-Hindi, 1427 AH, juz. 2, uk. 117.
  11. Tarihi, Tarikh al-Shia Fi al-Hindi, 1427 AH, juz. 2, uk. 81.
  12. Muhadithi, Farhange Ghadir, 1386 S, uk. 564.
  13. Muhadithi, Farhange Ghadir, 1386 S, uk. 564.
  14. Majlisi, Zadu al-Ma'ad, Muasasat al-Alamy, juz. 1, uk. 429-430.
  15. Majlisi, Zadu al-Ma'ad, Muasasat al-Alamy, juz. 1, uk. 429-430.
  16. Rifa'i, Mu'jam Ma Kutab 'An al-Rasul wa Ahlul-Bayt, 1371 S, juz. 6, uk. 66.
  17. Tazama: Sadra'i al-Khu'i, Faharesteghan Nuskhehaye Khati Hadithi wa Ulumi Hadithi Shia, 1382 S, juz. 10, uk. 437, 459, na 537.

Vyanzo

  • Dūzdūzānī Tabrīzī, Yadullāh. Istiftāʾāt ḥaḍrat-i Āyatullāh al-ʿuẓmā Dūzdūzānī Tabrīzī. Tehran: Tābān, 1379 Sh.
  • Kafʿamī, Ibrāhīm b. ʿAlī al-. Al-Miṣbāḥ Junnat al-amān al-wāqīya wa jannat al-īmān al-bāqīya. Qom: Dār al-Raḍī, 1405 AH.
  • Majlisī, Muḥammad Bāqir al-. Biḥār al-anwār. Second edition. Beirut: Dār Iḥyāʾ al-Turāth al-ʿArabī, 1403 AH.
  • Majlisī, Muḥammad Bāqir al-. Zād al-maʿād. Edited by ʿAlā al-Dīn Aʿlamī. Beirut: Muʾassisat al-Aʿlamī li-l-Maṭbūʿāt, [n.d].
  • Maybudī, Ḥusayn b. Muʿīn al-Dīn. Diwān-i Amīr al-Muʾminīn (a). Edited by Akram Shafāʾī. Based on the version of the Tasawwuf-i Iran website.
  • Muḥaddithī, Javād. Farhang-i Ghadīr. Qom: Nashr-i Maʿrūf, 1386 Sh.
  • Nūrī, Mīrzā Ḥusayn al-. Mustadrak al-wasāʾil wa musṭanbit al-wasā'il. Qom: Muʾassisat Āl al-Bayt, 1408 AH.
  • Rufāʿī, ʿAbd al-Jabbār. Muʿjam mā kataba ʿan al-Rasūl wa Ahl Baytih. 1st edition. Tehran: Nashr-i Wizārat-i Irshād, 1371 Sh.
  • Sipihr, Muḥammad Taqī. Nāsikh al-tawārīkh. Tehran: Asāṭīr, 1385 Sh.
  • Ṭurayḥī, Muḥammad Saʿīd, Tārīkh al-Shīʿa fī l-Hind. Netherlands: Ākādimīyya al-kūfa, 1426/2005.