wikishia:مقالات پیشنهادی/مقاله

Kutoka wikishia


  • Kukusanya baina ya Sala mbili « Ni namna ya kuzisali sala mbili kwa wakati mmoja kwa sharti ya kuwa sala hizo zinashirikiana katika wakati mmoja, mfano; kusali sala ya Adhuhuri na Alasiri kwa pamoja wakati wa mchana na wakati maaalum unaoruhusiwa kuzisali au kusali sala ya Magharibi na Isha kwa pamoja baada ya kuzama kwa jua na kuingia kwa wakati shirikishi. Kwa upande wa madhehebu ya Shia, wamejuzisha kukusanya baina ya sala mbili kwa mashiko ya Hadithi za Bwana Mtume (s.a.w.w) zinazopatikana katika vitabu vyao na vitabu vya Ahlu-sunna na pia sira ya Maimamu wao (a.s).Ama Ahlu-sunna wao hawakubaliani na suala la kukusanya baina ya sala mbili isipokuwa katika mazingira maalumu tu, kama vile kuwa mgonjwa au safarini.»
  • Kusali kimya kimya «humaanisha kusoma kimya kimya nyiradi au dhikri za swala bila kunyanyua sauti. Dhikri hizo ni kama vile tasbihi nne maarufu za swala zisomwazo badala ya Surat al-Fatiha, Pia Surat al-Fatihah na Surah zisomwazo baada Surat al-Fatihah.»
  • Akhera «Ni ulimwengu baada ya kifo na mauti na ni ulimwengu ujao baada ya maisha ya dunia.»
  • Sadaka za lazima «Ni wajibu wa kimali unaoelezewa katika Uislamu ambao unabeba maudhui mbalimbali kama vile zaka ya mali, zakat al-fitr na kafara.»
  • Ulul-amri «Ina maana ya wenye mamlaka, na hao wenye mamlaka ni watu ambao ni wajibu kuwatii kwa msingi wa Aya ya Ulul-Amr. Istilahi hii imekuja na kuelezwa ndani ya aya ya 59 ya surat al-Nisaa.»
  • Kafara ya swaumu «Ni adhabu ambayo huwekwa kutokana na kubatilisha na kuharibu funga ya mwezi wa Ramadhan, funga ya nadhiri ya muda maalumu na pia kadhwaa au malipo ya funga ya mwezi wa Ramadhan ikiwa itaharibiwa na kubatilishwa baada ya adhana ya adhuhuri, funga ambayo ilikuwa ni wajibu kwa mukallaf (mwenye kuwajibishwa).»
  • Safari ya Kisheria «Ni safari ambayo ndani yake msafiri analazimika kusali sala zake kwa kupunguza (Sala za rakaa nne azisali rakaa mbili) na hapaswi kufunga Swaumu.»