Shahada mbili

Kutoka wikishia
(Elekezwa kutoka Shahada Mbili)

Shahada mbili ni kushuhudia na kukiri umoja na upweke wa Mwenyezi Mungu na utume wa Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w) na kukiri pia kukubali tawhiid na upweke wa Mwenyezi Mungu na utume na kwamba vitu viwili hivyo ni miongoni mwa misingi ya dini ya kiislaam. Shahada mbili zinatambulika kuwa ndio mpaka kati ya Uislaamu na ukafiri. Hivyo basi mtu ambae atatamka shahada mbili, huzingatiwa na kuhesabiwa kuwa ni muislaam na sharia na hukumu zakiislaam zitatumika kwake au juu yake.

Waislaamu katika tashahudi ya kila sala na katika adhana na Iqamah hutamka na kusoma shahada mbili. Mafaqihi na wanazuwoni wa kisheria wa kishia wamezungumzia shahada mbili katika milango mbali mbali ya kifiqhi. Kwa mujibu wa fat'wa zao ni kuwa ni wajibu kutamka na kusoma shahada mbili katika sala ya maiti baada ya takbira ya kwanza na kumtamkisha shahada mbili mtu ambae yuko karibu kukata roho na kuziandika juu ya kafan na sanda ya maiti ni jambo la sunna. Shahada mbili katika ujenzi wa kiislaam, fani ya uandishi na utengenezaji wa pesa pia ni sehemu ambazo shahada mbili zimetumika na kuzingatiwa na kutiliwa umuhimu katika maeneo hayo.

UTAMBULISHO

Shahada mbili: Ni kushuhudia juu ya Upweke na umoja wa Mwenyezi Mungu na kukiri na kushudia ujumbe wa Hadhrat Muhammad (s.a.w.w). (1) kwa mujibu wa maneno ya wanazuwoni wa kifiqhi wa kishia, shahada mbili ni kutamka jumla au sentensi hizi mbili au kuthibiti kwa madhumuni ya sentensi hizi : «أشْهَدُ أنْ لا الهَ الاّ الله وأشْهَدُ أنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللّه» Nashuhudia ya kwamba hakuna Mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu mmoja na nashuhdia ya kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Lazima madhumuni ya sentensi mbili hizi yathibiti.(2) Kwa mujibu wa maneno ya shekhe Swadouq ni kuwa shahada mbili ni kukiri na kukubali Tawhid (Upweke wa Mwenyezi Mungu) na Utume na hii ni misingi miwili kati ya misingi ya dini ya kiislaam.(3)

THAMANI YA KIFIQHI NA KISHERIA

Kwa mtazamo wa waislaam shahada mbili ni mpaka kati ya Uislaam na Ukafiri, kwa maana kwamba mtu ambae atatamka shahada mbili kwa ulimi wake, basi hukumu za kiislaamu zitatumika kwake (4) na miongoni mwa hukumu hizo ni kwamba mwili wake utahukumiwa kuwa ni twahara na msafi na nafsi yake na mali yake ni vyenye kuheshimika na kuhifadhika na kulindwa kwa mujibu wa sharia za kiislaam.(5)

Kwa mujibu wa maelezo ya shekhe Swadouq ni kuwa, katika baadhi ya riwaya Imani imefasieiwa kwa maana ya shahada mbili.(6) kwa msingi wa mtazamo na nadhia ya Allamah Twabatwabai (1281-1360sh) ni kwamba Imani ina daraja kadhaa kiasi kwamba daraja ya kwanza ya Imani, ni kuitakidi na kuamini kwa moyo na kuamini madhumuni ya shahada mbili Imani ambayo itamfanya mtu kutekeleza hukumu mbali mbali za kiislaam (furu'uid-dini).(7)

Katika vitabu vya kifiqhi na kisheria imezungumziwa shahada mbili katika maeneo na sehemu tofauti kama vile hukumu za maiti (Wafu) katika mlango wa Twahara (8) Tijara na miamala (9) mlango wa sala (10) na jihadi (11).

Adabu na hukumu kwa mujibu wa mtizamo na maono ya wanazuwoni wengi wa kisheria wa kishia, kutamka shahada mbili katika sala ya maiti baada ya takbira ya kwanza ni jambo la wajibu. Wanazuwoni wengine wamesema kuwa kufanya hivyo ni sunna.(12) Kumtamkisha shahada mbili na uimamu wa maimau kumi na mbili (a.s) mtu ambae yuko katika hali ya kukata roho ni jambo la sunna.(13) Na ni sunna kuandika shahada mbili juu ya kafan na sanda ya maiti na iandikwe kwamba yeye anashuhudia shahada mbili na ana kiri shahada mbili.(14) Wanazuwoni wa fiqhi walio wengi, wanasema kuwa kutamka na kusoma shahada mbili katika hotuba za sala ya ijumaa kupitia imamu wa jamaa ni jambo la sunna.(15). Kwa mujibu wa maneno ya Swahibul-jawahiir ni kuwa miongoni mwa adabu za biashara, ni kutamka shahada mbili wakati unapokaa mahala pa biashara.(16)

Matumizi ya shahada mbili katika tamaduni za kiislaam

Matumizi ya shahada mbili katika mambo yaujenzi na fani za kiislaam. Katika dua na ibada mbali mbali za waislaam ibara za shahada mbili zinamatumizi mengi sana (17) kwa mfano, waislaam huitamka katika tashahudi ya kila sala (18) na pia katika Adhana na Iqaamah (19) hutamkwa shahada mbili katika maeneo hayo. Shahada mbili katika Ujenzi (miimar) ya kiislaam, katika fani ya uandishi na utengenezaji wa sarafu pia ni maeneo ambayo shahada mbili zimetumika.(20)

UFAFANUZI (MAELEZO YA UFAFANUZI)

  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j41, ukurasa 630.
  • Kama mfano angalia kitabu cha Najafy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j41, ukurasa 630
  • Angalia kitabu cha shekhe Swadouq, Manlaa yahdhuruhul-faqiih, cha mwaka 1413q, j1, ukurasa 299.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j41, ukurasa 630, Twabatwabai, Al-miizaan, cha mwaka 1417q, j1, ukurasa 301-303.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j21, ukurasa 143.
  • Angalia kitabu cha shekhe Swadouq, Manlaa yahdhuruhul-faqiih, cha mwaka 1413q, j1, ukurasa 299-300
  • Twabatwabai, Al-miizaan, cha mwaka 1417q, j1, ukurasa 301-303.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j12, ukurasa 40, Yazdiy twabatwabai, Al-ur'watul-wuthqaa miizaan, cha mwaka 1409q, j1, ukurasa 417.
  • Kama mfano angalia kitabu cha :Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j22, ukurasa 452.
  • Kama mfano angalia kitabu cha :Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j10, ukurasa 245,246,264.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j41, ukurasa 630.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j12, ukurasa 40.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j4, ukurasa 14.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j9, ukurasa 224.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j11, ukurasa 216, Najafiy, Kashful-ghitwa, cha mwaka 1422q, j3, ukurasa 255.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j22, ukurasa 452.
  • Kama mfano angalia kitabu cha shekhe Tuusiy, Misbahul-mutahajjidi, cha mwaka 1411q, j1, ukurasa 15,16,49.
  • Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j10, ukurasa 245,246.
  • Shekhe Tuusiy, Misbahul-mutahajjid, cha mwaka 1411q, j1, ukurasa 29, Najafiy, Jawaahirul-kalaam, cha mwaka 1404q, j9, ukurasa 81-82.
  • Kama mfano angalia kwenye kitabu: Afruugh, (Madhaamiin wa anaasiri shii'i dar Honar asri swafawiy baa negaahi be honar qaali boofi, negaargari wa felezkaarii), ukurasa 48, Abbas Zaadeh, (Barrasi naqshe madh'hab shiie bar honar wa mi'imaari imam zadegaan iran).

VYANZO

  • Afruugh, Muhammad, (Madhaamiin wa anaasir shii'i dar Honar asri swafawiy boo negaahi be honar qaali boofi), negaargariy wa felezkaarii), Mutwala aati Iraaniy, namba 20, Paaiiz 1390sh.
  • Shekhe Swadouq, Muhammad bin Ali, Manlaa yahdhuruhul-faqihi, Qom, Daftar Intishaarat waabaste be Jaamiatul-mudarrisiin Hawzeye ilmiye qom, cha mwaka 1413q.
  • Shekhe Tousiy, Muhammad bin Hasan, Misbahul-mutahajjid wa silaahul-muta'abbid, Bairut, Muassase fiqhi shiie, cha mwaka 1411q.
  • Shekhe Tousiy, Muhammad bin Hasan, Misbahul-mutahajjid wa silaahul-muta'abbid, Bairut, Muassasatul- fiqhi shiie, cha mwaka 1411q.
  • Twabatwabai, Sayyid Muhammad Husein, Al-miizaan fii tafsiril-qur'an, Qom, Daftare intishaaraat islaamiy waabaste be Jaamiatul-mudarrisiin Hawzeye ilmiye qom, cha mwaka 1417q.
  • Abbas Zaadeh wa diigaraan, (Bar'rasi naqshe madh'habe shiie bar honar wa miimaari imam zaadegaan iran), Intishare 2 mehri 1395sh, mushaahadeh 30 day mwaka 1398sh.
  • Najafiy, Jaafar bin Khudhri, Kashful-ghitwaa an mubhamaatis-shariatil-ghar-raa, qom, Daftar Tablighaat islaamiy Hawzeye ilmiye qom, mwaka 1422q.
  • Najafiy, Muhammad Hasan, Jawaahirul-kalaam fii sharhi sharaai'il-islaam, Bairut, Darul-ihyaait-turaathil-arabiy, cha mwaka 1404q.
  • Yazdiy Twabatwabaiy, Sayyid Muhammd Kaadhim, Al-urwatul-wuthqaa fiima taummu bihil-bal'waa, Bairut, Muassasatul-aalamiy lilmatbuuaat, cha mwaka 1409q.