Dua ya ‘Arafa ya Imamu Sajjad

Kutoka wikishia

Dua ya ‘Arafa ya Imam Sajjad (a.s) (Kiarabu: دعاء الإمام السجاد يوم عرفة), Dua ya arubaini na saba ilioko kwenye kitabu Sahifa Sajjadiyyah, ni mojawapo ya dua maarufu za Imam Sajjad (a.s), dua hii ndio dua maalumu na makhususi isomwayo siku ya Arafa. Dua ya ‘Arafa ndiyo dua ndefu zaidi katika kitabu Sahifatu Sajjadiyya. Ndani yake kuna muna maudhui kadhaa, kama vile; uchambuzi wa majina na sifa za Mwenyezi Mungu, dua na sala na salamu kwa bwana Mtume wa (s.a.w.w), Ahlul-Bayt (a.s) na Mashia, pamoja na ufafanuza wa mafunzo ya baadhi ya masuala ya kimaadili na vikwazo vya nafsi. Katika dua hii, Imam Sajjad (a.s) akielezea sifa za Mashia, mamesema miongoni mwa wasifu wa Mashia ni; kwa kukiri nafasi ya Ahlu al-Bayt, kutoa ahadi juu ya kufuata amri zao, kushikamana na kubaki chini ya taa yao, pamoja na kusubiri utawala wa Ahlu al-Bayt.

Mafundisho ya dua hii yamegawanywa katika sekta kadhaa za kitheolojia, pia imezungumzia maudhui nyengine tofauti, kama vile; Sala na salamu kwa bwana Mtume na Ahlul Bayt zake (a.s), welewa na utambuzi wa Imamu, kukiri makosa, na maombi ya mahitaji.

Dua ya arubaini na saba imeoroshwa katika vitabu kadhaa, miongoni mwavyo ni: "Najwaye Aarifaan" na "Irfane Arafe". Pia, dua hii imefafanuliwa na kupewa maelezo ya uchambuzi katika vitabu mbali mbali vilivyo fanya kazi ya uchambuzi wa Dua ya ‘Arafa, kama vile; Diyaru Aashiqan cha Hussein Ansarian na Shuhud wa Shenakht cha Hassan Mamduhi Kirmanshahi, vitabu vimeandikwa kwa lugha ya Kiajemi, isipokuwa kitabu kiitwacho Riyadh al-Salikin ambacho kimeandikwa kwa lugha Kiarabu.

Mafundisho

Dua ya arobaini na saba, inayojulikana kama Dua ya Arafa ya Imam Sajjad (a.s) ni moja ya dua zilizomo katika Sahifa Sajjadiya ambayo husomwa siku ya Arafa. Kwa maoni ya Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, dua hii ya Imam Sajjad ni kama vile ufafanuzi na maelezo ya uchambuzi wa Dua ya Arafa ya Imam Hussein (a.s). [1] Katika dua hii, Imam Zainul Abidin (a.s) amezungumzia masuala kadhaa ndani yake:

  1. Tawhidi, majina na Sifa za Mwenyezi Mungu.
  2. Dua kwa ajili ya bwana Mtume Muhammad (s.a.w.w).
  3. Dua kwa ajili ya Imamu Ma'sum (a.s)
  4. Dua kwa wafuasi wa Ma'sum.
  5. Dhambi na uovu.
  6. Kuomba msamaha na maghfira kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
  7. Kuelezea njia za toba.
  8. Shetani na hadaa zake.
  9. Kifo na dalili za Qiyama.
  10. Maadili mema na maovu ya nafsi ya mwanadamu. [2]
  11. Kwa mujibu wa maelezo ya Mamduhi Kermanshahi, Dua ya Arafa ndio dua refu zaidi ya Imam Sajjad (a.s) iliomo katika Sahifa Sajjadiya, na inazingatia zaidi uhusiano fungamani la kiroho kati ya mja mwema na Mwenye Ezi Mungu. [3]

Mafundisho ya Dua ya Arafa yamegawanywa katika makundi kadhaa ya msingi:

Maarifa ya Mungu

  • Shukrani na sifa njema ni zenye kumstahikia Mwenye Ezi Mungu peke yake, ambaye ni mmiliki, msimamizi na muumba wa ulimwengu.
  • Uwezo na elimu ya Mungu imetawala kila kilichomo kwenye ulimwengu wa uwepo.
  • Kukiri Umoja, Ukarimu na Utkufu wa Mungu.
  • Ukali wa kisasi cha Mungu.
  • Kuzingatia na kutilia mkazo juu ya Upendo, Uadilifu na Ujuzi wa Mungu.
  • Usikivu na kuona kwa Mwenyezi mungu.
  • Utangu na uwepo endelevu wa Mungu usio na mwanzo na mwisho.
  • Utukufu wa Mungu.
  • Kumtambua Mungu kuwa ni muumba wa viumbe vyote.
  • Uumbaji wa ulimwengu katika hali bora zaidi.
  • Mungu kuto kuwa na washirika.
  • Kumtakasa Mungu na kwamba hana anaye fafana Naye wala asiye fanana Naye
  • Unyenyekevu, heshima, utii na kujisalimisha kwa kila kiumbe mbele ya Mwenyezi Mungu.
  • Kutambua kwamba Hukumu za Mungu ni kulingana na uadilifu na haki.
  • Utaratibu wa ajabu wa mfumo wa uumbaji.
  • Ukosefu wa uwezo wa akili ya binadamu kuelewa asili na dhati ya Mungu.
  • Kutambua kwamba Mungu hana mwenza na hakuna nguvu dhidi yake.
  • Uwazi wa viwango vya kimungu katika kutenganisha haki na batili.
  • Rehema na hekima ya Mungu.
  • Ukunjufu wa Mungu katika kuwapa msamaha viumbe wake.
  • Kutambua kwamba uongofu wa binadamu uko mikononi mwa Mungu.
  • Unyenyekevu wa viumbe vyote mbele ya Mungu.
  • Kuto kuwepo nguvu dhidi ya Mungu kutoka kwa viumbe vyote ziwezazo kumshinda Mwenye Ezi Mungu.
  • Neno na matakwa thabiti ya Kiungu.
  • Kuthabitika bila ya pingamizi kwa matakwa ya Mungu.
  • Tofauti kati ya sifa na shukrani za Mungu na sifa za wasiokuwa Yeye.
  • Kujikurubisha kwa Mungu kwa kumshukuru Mungu.
  • Sifa za milele na enevu za Mungu, sifa na shukurani zinayolingana na ufalme wake wa enzi, sifa ziendazo sambamba na radhi na kuridhika kwake, sifa na shukurani ziendazo sambamba na neema, sifa na shukurani ziendazo sambamba na nia safi na ...[4]

Dua kwa Muhammad Aali zake (a.s)

Katika sehemu ya pili ya dua ya Arafah ya Imam Sajjad (a.s), maudhui ya dua imeelekea upande wa kumtakia bwana Mtume na Aali zake (a.s).

  • Sala na salamu kwa Muhammad na watu wa nyumba yake (a.s).
  • Falsafa ya sala ya Mtume na familia yake (a.s), Shukrani na kuthamini uwepo wa Mtume na Aali zake (a.s), kuendeleza kumbukumbu na kutukuza jina la Mtume (s.a.w.w) na kumfanya yeye kuwa mfano na kigezo.
  • Kukitambulisha cheo cha bwana Mtume (s.a.w.w).
  • Sala na salamu kwa watu wa nyumba ya bwana Mtume (s.a.w.w), kwa kuwa wao ndio walinzi wa dini na wawakilishi wa Mungu duniani na hoja na ithibati za Kiungu kwa waja wake.
  • Kukitambulisha kizazi cha Mtume (s.a.w.w) ni njia ya kumfikia Mungu na njia ya kuifikia Pepo.
  • Ombi la sala na salamu isiyokuwa na mwanzo wala mwisho kwa Mtume na familia yake.
  • Sala na salamu kwa bwana Mtume (s.a.w.w): Sala na salamu endelevu, inayopekea radhi na furaha, sala na salamu za milele, sala na salamu adhimu na enevu, zisiyohesabika. [5]

Utambulisho wa hadhi ya Imamu

Imamu Sajjad (a.s.) katika sehemu ya tatu ya Dua ya ‘Arafah anaelezea hadhi ya Ahlul Bayt (a.s) na pia anawaombea dua Mashia na kueleza sifa zao. Maelezo juu ya hadhi ya Ahlul Bayt ya Mtume (s.a.w.w):

  • Watekelezaji wa amri za Mungu.
  • Hazina ya elimu ya Mungu.
  • Wahifadhi wa dini.
  • Wawakilishi wa Mungu kwenye ardhi yake.
  • Ushahidi na hoja za wazi kwa waja.
  • Njia ya kuwongoza waja kwa Mungu, na watoharifu kutokana na dhambi na uchafu.
  • Kimbilio la watu na waumini.
  • Akisiko la uzuri wa Kiungu
  • Ukubwa na uadhimu wa elimu ya Ahlul Bayt (a.s)
  • Sala salamu kwa Mtume na Ahlul Bayt (a.s), iliyo endelevu isio na kikomo ilinganayo na uadhimu wa kiti cha enzi cha Allah.

Utambulisho wa hadhi ya Ahlul Bayt (a.s)

  • Taa inayowaka kwa ajili ya kumulika haki na ukweli, wao ndio jia ya kufikia radhi ya Mungu na kimbilio la wakimbizi.
  • Ulazima wa kufuata maagizo ya Ahlul Bayt (a.s) [6]
  • Imamu ndio lengo na kusudio asili la uumbaji.
  • Ulazima na wajibu wa uwepo wa Imamu Maasumu katika kila zama.
  • Uthibitisho na upasishaji wa dini ya Mungu katika kila wakati kupitia Imamu.
  • Ulinzi wa malaika kwa Maimamu na majeshi ya Kiungu.
  • Shukrani kwa Mungu kwa sababu ya uwepo wa neema ya Imamu Maasumu (a.s).
  • Ulazima wa kujenga nguvu na kuanzisha utawala kwa Imamu Maasumu (a.s).
  • Dua na ombi la kusimamishwa sheria kupitia Kitabu (Qur’ani) na kutoa maamuzi kupitia sheria za Kiungu na Sunna za bwana Mtume (s.a.w.w) chini ya usimamizia wa Imamu Maasumu (a.s).
  • Ombi la kuhuisha upya sheria za dini ambazo watawala waovu wamezitokomeza.
  • Nyenzo tofauti za Imamu katika kuongoza watu kwa Mungu.
  • Ombi la kuwataka watu kumtii Imamu (a.s), na kujisalimisha kwake na kufanya juhudi katika kutafuta radhi zake.
  • Ombi la sala na salamu kwa wapenzi na wafuasi wa Imamu (a.s).
  • Utii wa kujisalimisha kwa Maasumu na kumsaidia, njia ya Kujikurubisha Kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake (s.a.w.w).
  • Salamu kwa marafiki na wafuasi wa Ahlul Bayt (a.s): Sifa za Mashia wa Ahlul Bayt (a.s): Kukiri hadhi ya Ahlul Bayt (a.s), Kufuata maagizo yao, Kushikamana na uongozi wao, Kusubiri na kuwa na hamu ya utawala wa Ahlul Bayt (a.s).
  • Dua kwa Mashia wa Ahlul Bayt (a.s): Kuwa miongoni mwa watu wenye takuwa, Mwenye Ezi Mungu kupokea kwa toba zao na kuwekwa mahala salama. [7]

Ukiri wa makosa

Katika sehemu hii, Imamu Sajjad (a.s) anazungumza juu ya udhaifu wa nafsi ya mwanadamu na kuomba msamaha kutoka kwa Mungu.

  • Alama za rehema na hadhi ya siku ya Arafa (siku adhimu na yenye heshima na meza ya rehema za Mungu inayo wapambazukia waja wake
  • Kulalamika juu ya hali yake binafsi ili kujikaribisha kwenye rehema za Mungu.
  • Kuomba kuwekwa chini ya uongofu na mwongozo wa Kiungu
  • Kujielewa ni mojawapo ya nguzo muhimu za mfumo wa elimu.
  • Kuto tii waja katika kutekeleza kwa amri za Mungu.
  • Kukimbilia kwenye rehema za Mungu kutokana na adhabu
  • Kuomba msamaha wa Mungu.
  • Omba malipo adhimu ya Mungu katika siku ya Arafa.
  • Kukiri Upweke wa Mungu ili kujikurubisha kwake.
  • Kuwa na dhana njema na kuomba ukuruba wa Mwenyezi Mungu.
  • Kukiri umaskini wa unyonge wa kibinadamu mbele ya Mungu.
  • Kutenda hisani na kutaka msamaha wa Mungu kwa wenye chuki nawe na kutokuwa na haraka katika kuwaadhibu.
  • Aina za kukiri dhambi, makosa na mitelezo, (dhambi za siri na za makusudi)
  • Matokeo ya kumwelekea Mungu na kusahau kumkumbuka Mungu ni;

kuenea kwa unafiki, ujinga na kudhoofika kwa uhusiano baina ya mja na Mungu wake.

  • Kukiri dhulma ya mja juu ya nafsi ya yake.
  • Kuwa mbali na Mungu na matokeo ya kudharau amri za Mwenye Ezi Mungu.
  • Kuangamia ni matokeo ya hakika ya kujitenga na njia ya Mungu.
  • Uhalisia wa kwamba; Mwanadamu ni kiumbe anayezongwa na mabalaa na muda mrefu wa mateso na dhiki za kidunia.
  • Hatari ya mwanadamu kuwacha pekee, yeye na nafsi yake.
  • Mipango mbalimbali ya Shetani ya kumdanganya mwanadamu. [8]

Maombi ya mahitaji mbali mbali

Imam Sajjad (a.s) katika sehemu ya mwisho ya dua yake, anamwomba Mwenye Ezi Mungu kwa jaha ya waja wake wa karibu (kupitia waja wake wa karibu) huku akielezea mahitaji yake mbele ya Mola wake. Sehemu ya maombi haya ni kama ifuatavyo:

  • Dua ya maombi ya kuwekwa chini ya utawala maalum wa Mwenyezi Mungu.
  • Dua ya maombi ya kumsihi Mwenye Ezi Mungu kuto muadhibu kwa sababu ya kuto tekeleza majukumu.
  • Dua ya maombi ya kuto puzwa na kuto puruziwa kamba na Mwenyezi Mungu, kutokana na makosa.
  • Dua ya maombi ya kuamka kutoka katika usingizini wa ghafla.
  • Dua ya maombi ya kujipendekeza kwa Mwenyezi Mungu, Mhuisha nyoyo.
  • Dua ya maombi kwa Mwenyezi Mungu kwa nijia ya hofu na unyenyekevu.
  • Dua ya maombi ya msamaha kupitia uombezi wa Mtume (s.a.w.w) na Ahlul Bayt zake (a.s), kama ni waombezi mbele ya Allah.
  • Dua ya maombi ya kuwekwa chini ya himaya na uongozi wa Mwenyezi Mungu.
  • Dua ya maombi ya malipo kwa wale wanaotimiza ahadi zao.
  • Dua ya maombi ya kuokolewa kutokana na madhara ya kuvuka mipaka ya Mungu.
  • Dua inayo onesha kwamba; kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu ndio jambo lenye ladha kuliko mambo mengine yote.
  • Dua ya maombi ya kupata maisha yenye heshima na kifo cha furaha.
  • Dua ya maombi ya kuamka kutoka usingizini wa kuojua uhakika wa mambo.
  • Dua ya maombi ya kufuata njia za kuelekea kwenye mambo ya kheri.
  • Dua ya maombi ya kuokolewa kutokana na kubatilika kwa matendo na kupotea kwa Baraka.
  • Dua ya maombi ya kuelewa na kuhisi ubaya na hatari za dhambi kupitia moyo.
  • Dua ya maombi kwa Mwenye Ezi Mungu kwa ajili ya kupata taufiki ya usiku na mchana katika kumwomba Mungu, pamoja kuomba kupata pambo la nuru Yake.
  • Dua ya maombi ya utakaso kutokana na uchafu wa dhambi
  • Dua ya maombi ya kuepuka na hasira za Mungu.
  • Dua ya maombi ya kuokolewa kutokana majaribu, fitna na misiba.
  • Dua ya maombi ya kupata ulinzi wa kuto kabiliwa na usugu wa moyo chini ya kivuli cha umri mrefu.
  • Dua ya maombi ya kulindwa na shari za maadui zake kutokana na kuwakemea kwake maadui hao.
  • Dua ya maombi ya kuepusha na shetani na nafsi iamrishayo maovo.
  • Dua ya maombi ya kuokolewa kutokana na shida na mashaka.
  • Dua ya maombi ya kuto kata tamaa kutokana na rehema ya Mwenye Ezi Mungu.
  • Dua ya maombi ya kufichiwa kasoro na kuto fedheheshwa
  • Dua ya maombi ya afya na ustawi wa mwili.
  • Dua ya maombi ya yanayo onesha kwa; nia njema ndio kigezo cha matendo mema.
  • Dua ya maombi ya riziki na kipato.
  • Dua ya maombi ya kuondoa na kufuta upendo wa dunia kutoka moyoni mwa mtu.
  • Dua ya maombi ya cheo cha utakaso wa Mungu.
  • Dua ya maombi ya kunufaika na nia njema na maneno yanayopendeza na tabia njema.
  • Dua ya maombi ya mafanikio katika kufanya matendo mema.
  • Dua ya Shukrani kwa Mwenyezi Mungu kutokana na kuongezeka kwa neema.
  • Dua ya maombi kupata maisha mazuri.
  • Dua ya maombi ya kupata heshima mbele ya watu na kuwa na unyenyekevu mbele ya Mwenye Ezi Mungu.
  • Dua ya maombi ya kwa ajili ya kuokolewa kutokana na fitna na maovu.
  • Dua ya maombi ya neema na kuepukana na ujinga wa kujisahau.
  • Dua ya maombi ya kufikia cheo cha watu wenye hofu na matumaini (خوف و رجا).
  • Dua ya maombi ya kupata taufiki ya kukesha usiku.
  • Dua ya maombi ya kujikinga kwa Mwenye Ezi Mungu kutokana na uasi na adhabu.
  • Dua ya maombi ya yanayo onesha kwamba; Toba ni biashara yenye manufaa na faida kubwa mbele ya Mwenye Ezi Mungu.
  • Dua ya maombi ya kunufaika na msamaha na rehema za Mwenye Ezi Mungu na neema za Peponi.
  • Dua ya maombi ya kuwa karibu na watakatifu wa Mwenyezi Mungu Peponi.
  • Dua ya maombi yanayo onesha ulazima na umuhimu wa kuepuka uadui kwa wengine.
  • Dua ya maombi ya kupata neema kamilifu.
  • Dua ya maombi ya kuepukana na shaka na wasiwasi.
  • Dua ya maombi ya kupata moyo wenye amani usio na shaka na wasiwasi.
  • Dua ya maombi ya usafi kutokana na dhambi kupata utulivu wa akili, na kusalimika katika nyanja zote.
  • Dua ya maombi ya kuomba hifadhi ya heshima kwa kuto omba mahitaji kwa wengine.
  • Dua ya maombi ya kuto kuwa pamoja na madhalimu.
  • Dua ya maombi yanayo onesha kwamba; kufanya ibada hija na umra ni mojawapo ya sababu za kumridhisha Mwenye Ezi Mungu.
  • Kumtegemea Mwenyezi Mungu na kukimbilia kwake tu, ndiyo njia pekee ya kupata amani na utulivu katika maisha. [9]

Tafsiri na uchambuzi wa Dua ya ‘Arafa

Kuna maandishi kadhaa yaliokuja kufasiri na kutoa maelezo juu ya kitabu Sahifa Sajjadiyya, vimeifasiri na kuifafanua Dua ya 47 ilioko katika kitabu hicho. Miongoni mwa vitabu hivi ni kama vile: Kitabu Diyaru Aashiqaan cha Hussein Ansarian. [10] "Shuhudi wa Shenaakht" cha Muhammad hassan Mamduhi Kirmanshahi [11] na "Sherhe wa Tarjume Sahife Sajjadiyya" cha Sayyid Ahmad Fahri [12]. Vitabu hivi vimechambua na kufafanua dua hii kwa lugha ya Kiajemi.

Pia kuna vitabu kadhaa, ambavyo vimeshughulikia uchambuzi wa dua hii tu, bila ya kuingiza ndani yake dua nyengine. Miongoni mwa vitabu hivyo ni; "Najwaa ‘Aarifaan: ambacho ni maelezo juu ya Dua ya 47 ya Sahifa ya Sajda (Dua ya Siku ya Arafa)" cha Sayyid Ahmad Sajjadi [13] na "Irfaane Arafe: ambacho ni Tafsiri, Maelezo na uchambuzi juu ya mada za Dua ya Arafa ya Imam Hussein (a.s) na Imam Sajjad (a.s)" kilicho andikwa na Qadeer Faadhili [14] kwa lugha ya Kiajemi (Kifarsi).

Dua ya 47 ya Sahifa Sajjadiyya pia imetolewa maelezo yake na kuchambuliwa kwa lugha ya Kiarabu kupitia vitabu tofauti, miongoni mwavyo ni Riyadhi as-Salikin cha Sayyid Alikhan Madani. [15] Fi Dhilali as-Sahifah as-Sajjadiyyah cha Muhammad Jawad Maghniyyah. [16] Riyadhi al-Arifiina cha Muhammad bin Muhammad Darabi [17] na Afaaqi ar-Ruuh cha Sayyid Muhammad Hussein Fadlullah. [18 Maana ya maneno ya dua hii pia yametolewa maelezo yake katika vitabu vya lugha, kama vile Ta'liqaat ala as-Sahifah as-Sajjadiyyah cha Faidhu Kashani [19] na "Sharhu as-Sahifah as-Sajjadiyyah" cha Izzuddin Jazairi. [20]

Andiko la dua na tafsiri

Na miongoni mwa dua za Imamu huyu ni Dua hii ya Arafah isemayo:

Dua ya ‘Arafa ya Imamu Sajjad

Tarjuma Dua
  1. Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu.
  2. Ee Mwenyezi Mungu, sifa zote njema ni zako, Muumbaji wa mbingu na ardhi, Mwenye utukufu na heshima, Mola wa mabwana, Mungu wa kila kiumbe, Muumbaji wa kila kilichoumbwa, Mrithi wa kila kitu. Hakuna kitu chochote kinachofanana Naye, na hakuna kitu kinachomoka na kukaa nje ya ujuzi wake. Yeye ndiye anayemiliki kila kitu, na anasimamia kila kitu.
  3. Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe, Mmoja Mpwekekaji Mpekee wa pekee.
  4. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe tu, Mwenye heshima, Mheshimika, Muadhamu, Mwadhimika, Mtukufu Mwenye kutukuka.
  5. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe tu, Aliye juu, Mtukukaji, Mwenye nguvu za juu.
  6. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe, Mwenye kurehemu, Mwenye huruma, Mjuzi, Mwenye hikima.
  7. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe, Mwenye kusikia, Mwenye kuona, Mtangu, Mjuzi wa khabari zote.
  8. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe, Mkarimu, Asiye na mipaka katika ukarimu, Mwenye kudumu, Asiye na mipaka katika dawama yake.
  9. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe, wa Awali kabla ya kila mtu, Na Mwisho baada ya kila hesabu na idadi.
  10. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe, Aliye katika ukuu wake, Na Mwenye ukuu katika ukaribu wake.
  11. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe, Mwenye uzuri, Mwenye uadhimu, Mwenye utukufu, na Mwenye sifa njema.
  12. Na Wewe Ndiye Mwenye Ezi Mungu, hakuna Mungu ila Wewe, Ambaye umeumba vitu bila ya kuhitaji mifano, Na ukaumba umbile la sura bila kukopi kutoka kwenye mfano wowote, Na ukabuni vitu vipya bila kuhitaji vigezo na vipimo kutoka mahala fulani.
  13. Wewe Ndiye Ambaye ulipanga kila kitu kwa mpangilio, Na ukarahisisha kila kitu kwa urahisi, Na ukadhibiti kile kilichoko chini yako kwa mpangilio.
  14. Wewe Ndiye Ambaye hakuna mshirika aliye kusaidia katika uumbaji wako, Na hakuna waziri aliyekusaidia katika jambo lako, Na wala hakuwa na shahidi aliye kuwa akikushuhudia, wala aliye kuwa na mfano wako.
  15. Wewe Ndiye Ambaye uliye taka, basi kwa lazima kikawa kile ulichokitaka, Na ukapitisha amri yako, basi ikakamilika amri ulio ipitisha, Na ukahukumu, basi ikawa ni haki kile ulicho hukumu.
  16. Wewe Ndiye Ambaye hakuna mahali penye uwezo kukuingiza ndani ya mipaka yake, Na hakuna mamlaka yoyote yenye uwezo wa kusimama, kujidhatiti na kuhimili mamlaka yako, Na hakuna maelezo ya hoja au ufafanuzi wenye uwezu wa kukufafanua na kukudiriki.
  17. Wewe Ndiye Ambaye uliye hisabu kila kitu kwa idadi maalumu, Na mipaka kwa kila kitu ukakiwekea mipaka na muda maalumu, Na ukakipanga kila kitu kwa mpangilio maalumu.
  18. Wewe Ndiye Ambaye mawazo hayawezi kufikia asili ya dhati yako, Na akili haziwezi kuelewa jinsi yako, na macho hayawezi kuelewa mahali pa uwepo wako.
  19. Wewe Ndiye Ambaye huwezi kuzungukwa kiasi ya kwamba uwe na mipaka, Na wala hukufananisha na chochote kile, kiasi ya kwamba iweze kusemwa; ulikuwa haupo kisha ukawepo, Na haujazaa ili iwe ni kigezo cha kusema kwamba kwamba Nawe umezaliwa.
  20. Wewe Ndiye Ambaye huna mpinzani wa kukupinga aliye simama nawe, na wala huna aliye sawa Nawe kiasi ya kwamba uweze kuwa wa pili sambaba nawe, na wala huna mpinzani wa kupingana Nawe.
  21. Wewe Ndiye Ambaye uliye anza, na ukaanzisha, na ukavumbua ambayo hayakuwepo, na ukabuni, na ukaunda vyema kile ulicho umba.
  22. Utukufu ni wako! Imetukuka mno hadhi na nafasi yake, Na mahali pako ni mahala bora zaidi kuliko sehemu zote, na msikiko wa sauti ya ubambanuzi wako wa haki na batili ni mkubwa ni mkubwa na wa wazi ulioje!
  23. Utukufu ni wako! Upole wako ni upole ulioje, Wewe ni Mwenye huruma zilioje, na Wewe ni Mwenye hikima Mjuzi ulioje!
  24. Utukufu ni wako! Wewe ni Mfalme mwenye ufalme ulioje na hakuna wa kukuwekea mipaka katika ufalme wako, na Wewe ni Mkarimu mwenye ukarimu ulioje, na Wewe ni Mtukufu mwenye utukufu ulioje! Mwenye uzuru na utukufu, aliye juu ya kila kitu (mutakabbir) mwenye sifa njema.
  25. Utukufu ni wako! Umenyosha mkono wako katika kila aina ya kheri kwa viumbe wako, Na uongofu umetambulika kutoka kwako, Basi yeyote anayekuomba kwa ajili ya dini au dunia atakukupata (atakukuta Wewe ndiye mtoaji)!
  26. Umetukuka! Amenyenyekea kwako kila aliyeko katika mkondi wa elimu yako, na kimenyenyekea kwenye ukuu wako kila kilichopo chini ya kiti cha ufalme wako, na kila mja amesalimu amri kwenye mamlaka yako.
  27. Wewe Umetakasika! huhisiwi kupitia viungo vya hisi, wala hudirikiwi kupitia mawazo na akili, huchokozeki, hudanganywi, huzozwi, hupinduliwi, hubishwi, na wala huhadaliwi.
  28. Umetukuka! Njia yako iko wazi na haina mazonge, na hukumu yako ni uongofu, na Wawe upo hai Mwenye kujitosheleza.
  29. Umetukuka! Kauli yako ni hukumu thabiti, na maamuzi yako ni ya lazima, na matakwa yako ni maazimio.
  30. Umetakasika! Hakuna wa kuyarejesha nyuma matakawa yako, wala wa kubadili maneno yako (amri zako).
  31. Umetukuka! Wewe ni Mwenye dalili zilizo wazi, Muumba wa mbingu, Muumba viumbe.
  32. Shukurani ni za kwako, shukurani zinazo dumu kwa dawama yako.
  33. Na shukurani ni zako, zenye kudumu milele kupitia neema zako.
  34. Na shukurani ni za kwako, shukurani zilinganazo na kwenda sambamba na uumbaji wako.
  35. Na shukurani ni za kwako, shukurani zinazo pindukia radhi zako.
  36. Na shukurani ni za kwako, shukurani zinazo shikamana na shukurani za kila mwenye kukushukuru, na shukurani pungufu ya kila mwenye kushukuru (shukurani ambayo haijafikiwa na wenye kushukuru).
  37. Shukrani ambazo hamstahikii mwengine yeyote ila Wewe tu, shukurani ambayo haina lengo la kujikurubisha kwa mwengine yeyote ila kwako Wewe tu.
  38. Shukrani zinazodumisha ya shukurani ya kwanza, na inayo pelekea kudumu kwa kwa shukurani ya mwisho.
  39. Shukrani zinazo ongezeka kwa mzunguko wa nyakati, na kwa maengezeko yake yawe yanaengezeke mara kwa mara.
  40. Shukurani ambazo zinazo pindukia uwezo wa makarani (malaika) kuzihesabu, na ambazo zinazidi kile ambacho waandishi wamehesabu katika Kitabu Chako.
  41. Shukurani ambazo zinalingana na kiti Chako cha enzi kitukufu, na zinalingana na nafasi ya kiti Chako cha juu.
  42. Shukurani ambazo thawabu yake ni kamilifu mbele yako, na ambazo thawabu zake zinashinda kila thawabu.
  43. Shukurani ambazo dhahiri yake inalingana na batini yake, na batini yake inalingana na ukweli wa nia.
  44. Shukurani ambazo hakuna kiumbe aliyewahi kukuru kwa shukurani kama hizo, na hakuna anayejua hadhi yake isipokuwa Wewe peke yako.
  45. Shukurani ambazo husababisha kusaidiwa yule anayejitahidi kuzihesabu, na zinamuunga mkono yule anayejitahidi kuzitimiza kwa ushupavu wa moyo wote.
  46. Shukurani ambazo zinakusanya kila aina ya shukurani uliyoiumba, na zinaingia kwenye kila kile ambacho utakiumba baadae.
  47. Shukurani ambazo hakuna shukurani nyingine kuliko hizo zinayokaribia zaidi na maneneo yako, na wala hakuna anayekushuru zaidi kupitia shukurani shizo.
  48. Shukurani ambazo kwa ukarimu Wako zinalazimisha umiminikaji wa ziada katika ongezeko la wingi wake, na kwa ungezeko lake endelevu lipate baraka hadi liweze kufikia kwenye ukarimu Wako.
  49. Shukurani ambazo zinawajibisha kwa ukarimu wa (uso wako) cheo chako, na zinalingana na uadhimu wa utukufu Wako.
  50. Ee Mola wangu Mlezi, mfikishia sala na salamu zako zilizo bora zaidi Muhammad na Aali zake, mchaguliwa, mteuliwa aliye fadhilishwa na aliye kurubishwa (mbele ya Allah), na mbarikie kwa baraka zako zilizo kamilifu kuliko zote, na umrehemu kupitia rehema zako zenye utulivu wa hali ya juu kuliko zote.
  51. Ee Mola wangu Mlezi, mshushia rehema (sala) rehema na amani takatifu kuliko zote Muhammad na Aali zake, na umshushie rehema endelevu kuliko zote, na umshushie rehema zilizojaa ridhaa, rehema ambazo zisizo na kifani.
  52. Ee Mola wangu Mlezi, mshushie rehema Muhammad na Aali zake, zitakazo mridhisha na zitazovuka radhi ridhaa yake, na umrehemu kwa kiwango cha ridhaa zako na zitakazo pindukia ridhaa zako juu yake, na umrehemu kwa rehema ambazo hutaridhiki naye ila kwazo na wala hutamuona mwenye kustahiki nazo katu isipokuwa yeye.
  53. Ee Mola wangu Mlezi, mshushie rehema Muhammad na Aali zake, rehema zinazopindukia radhi zako, rehema ambazo zinazofungamana na dawama yako, na wala hazikomi kama yasivyo koma maneno yako.
  54. Ee Mola wangu Mlezi, mpe rehema baraka Muhammad na Ahlul Bayt wake, baraka zinazojumuisha baraka za malaika zako, manabii wako, mitume wako, na watu walioko katika taa yako, na zinayojumuisha baraka za waja wako miongoni mwa majini wako na watu wako, na wale watu wenye kujibu wito wako, na zitakazo jumuisha ndani yake baraka za kila kiumbe uliye muumba na kuwaleta kwenye ulumwengu wa uwepo miongoni mwa viumbe vyako.
  55. Ee Mola wangu Mlezi, mshushie rehema Yeye na Ahlul Bayt wake, rehema ambayo inakusanya ndani yake rehema zilizotangulia na zinazoanza kudhihidri kati uwepo wake, na umshushie rehema yeye na Ahlul Bayt wake, rehema zinazokubalika mbele yako na mbele ya walio chini yako, na zinazo anzisha na kusababisha rehema nyengine juu yake, na ziwe ni rehema zinazo ongezeka siku baada ya siku kwa kwa jinsi ya ongezeko la masiku, rehema ambazo haziwezi kuhesabiwa na mtu mwingine yeyote isipokuwa Wewe.
  56. Ee Mola wangu Mlezi, wabariki watu wema ambao ni Ahlul Bayt wake, wema ambao umewachagua kwa amri yako, na umewafanya kuwa hazina ya elimu yako, na walinzi wa dini yako, na Makhalifa wako katika ardhi yako, na hoja zako kwa waja wako, na ukawatakasa kwa mtakaso kutokana na uchafu kwa mapenzi yako, na ukawafanya kuwa ndio njia ya kukufikia wewe, na njia ya kuingia katika bustani yako (Pepo yako).
  57. Ee Mola, mswalie Muhammad na Aali bayti zake, sala ambayo itawazidishia malipo na ukarimu wako, sala ambayo itakamilisha mambo yao kutoka katika neema zako na kuwakamilishia ibada zako, na itawapa bahati nema kutoka katika faida na baraka zako.
  58. Ewe Mola wangu Mlezi, mshishie rehema yeye pamoja nao, rehema ambayo haina mwanzo katika fuwepo wake, na wala haina mipaka katka mwisho, na haina kikomo katika hatima yake.
  59. Ewe Mola wangu Mlezi, washushie rehema, kwa uzito wa wa kiti chako cha enzi na kwa kila kinachokuzunguka, na kwa kiwango cha kujaa mbingu zako na kilichoko juu yake, na kwa idadi ya ardhi zako na kilichoko chini yake na kilicho kati yake, rehema itakayo wakaribisha Nawe, na zitakazo pelekea ridhaa kwako na kwao, na isikatizwe kamwe bali ziendelee na zishikamane na rehema zinazo fanana nazo.
  60. Ewe Mwenyezi Mungu, hakika Wewe umekuewa ukiisaidia na kudhatiti dini Yako katika kila wakati kupitia Imamu ambaye Umemsimamisha kama kiongozi kwa waja Wako kwa ajili taa Yako, na ukawafanya ni minara ya miji yako, baada ya kuunganisha kamba yake na kamba Yako, na Ukamfanya kuwa ndie njia ya kufikia radhi Zako, na Ukafaradhisha kumtii, na Ukatoa onya juu ya kumuasi, na Ukaamrisha kufuata amri zake, na kukoma pindi anapotoa katazo, na kwamba asitokee mtu yeyote wa kumutangulia, na asiweze kubaki nyuma yake mtu yeyote, kwani yeye ni kinga ya wale wanaoomba hifadhi, na ndio maficho ya waumini, na ni kamba ya wale wanao tafuta mashiko, na ni pambo na fahari ya walimwengu.
  61. Ewe Mwenyezi Mungu, basi mpa walii wako mwamko wa shukrani kwa yale Uliyompa, na tupe sisi pia mfano wake katika hilo, na Mpe kutoka kwako mamlaka ya ushindi, na Mfungulie ushindi rahisi, na Msaidie kwa nguzo Yako yenye nguvu, na Uimarishe uti wa mgongo wake, na Nguvusha bega lake, na Mlinde kwa macho Yako, na Mpe himaya kwa ulinzi Wako, na Msaidie kwa Malaika Wako, na Mpe nguvu kwa jeshi lako lenye nguvu.
  62. Na kupitia yeye; Simamisha Kitabu Chako, mipaka Yako, na sheria Zako, na sunna za Mtume Wako. Baraka zako Ewe Mwenyezi Mungu zimwendee yeye na kizazi chake, na Uyafufua kupitia yeye yale ambayo madhalimu wameyaua miongoni mwa misingi ya dini Yako, na Uondoe kutu ya dhuluma kutoka katika njia Yako, na Uondoe mipindo katika njia Yako, na Waondoe wapotofu katika njia Yako, na Uangamize wapinzani wa lengo la kupotoa dini Yako.
  63. Na lainisha moyo wake kwa upande wa marafiki zako (waumini), na Nyosha mkono wake dhidi ya maadui Zako, na Tupe sisi huruma yake, rehema zake, upole wake, na huruma yake, na Utujaalie tuwe wasikivu na watiifu kwake, na tuwe katika jitihada ya kutafuta radhi zake, na tuwe tayari kwa ajili ya nusura yake na kutoa ulinzi kwa ajili yake. Ewe Mwenye Ezi Mungu baraka zako zimwendee yeye na Aali zake. Sisi tujikaribishe kwako na kwa Mtume wako kupitia hilo.
  64. Ee Mwenyezi Mungu, washushie rehema na amani vipenzi vyao, wale wanaokiri vyeo vyao, wanaofuata njia yao, wanaofuata nyayo zao, wanaoshikamana kisawasawa na nyayo zao, wanaoshikamana na uongozi wao, wanaokaa chini ya kivuli cha Uimamu wao, wanaojisalimisha chini ya amri zao, wanaojitahidi katika kuwatii, wanaomngojea za uongozi wao, wanaoelekeza macho yao kwao, basi wahsushie rehema na amani zilizobarikiwa, safi, endelevu, asubuhi na jioni.
  65. Na washushi rerhema na amani, na uyajumuishe mambo katika taqwa, na urekebishe (uyanyoshe) mambo yao, na uwasamehe makosa yao, hakika Wewe ndiye Mwenye kusamehe na Mwenye rehema, na Mbora wa kutoa maghufira, na utuweka pamoja nao katika nyumba ya amani kwa rehema zako, Ee Mrehemevu wa warehemevu.
  66. Ee Mwenyezi Mungu, hii ni siku ya Arafa, siku ambayo umeitukuza, na ukaiadhimu, umeeneza rehema zako ndani yake, ukazawadia ndani yake msamaha wako, ukajaalia ukarimu wako ndani yake, na ukawafadhili waja wako kupitia siku hii.
  67. Ee Mwenyezi Mungu, na mimi ni mja wako ambaye umemneemesha kabla ya kuumbwa kwake na baada ya kuumbwa kwake, kisha ukamfanya kuwa miongoni mwa wale ambao umewaongoza kupia dini yako, na ukamfanikisha kwenye haki yako, na ukamshikiza kamba yako, na umemwingiza katika chama (kundi) chako, na ukamwongoza kwa kuwafuata vipenzi vyako, na kuwachukia maadui zako.
  68. Kisha ukamwamuru, lakini hakutii, na ukamwonya, lakini hakuonyeka, na ukamkataza kuto pingana nawe, akavunja amri zako juu ya makatazo yako, si kwa ajili ya kukupinga, wala kwa ajili ya kukuasi, bali matamanio yake ilimwita kwenye kile ambacho umemwonya na kweney kile ambacho umemkataza, na adui yako na adui yake alikamsaidia katika hilo, kwa hiyo alifanya hivyo akijua ahadi yako ya adhabu, akitumaini msamaha wako, akiwa na yakini na msamaha wako, na alifanya hivyo hali ya kwamba yeye alikuwa na haki zaidi ya kutofanya hivyo, kutokana na mapenzi uliompa kwa ajili yake.
  69. Na hapa niko mbele yako nikiwa ni; mdogo, dhalili, mnyenyekevu, mwoga, mwenye hofu, nikikiri dhambi kubwa nilizo jitwika nazo, na makosa makubwa niliyoyafanya, nikiomba msamaha wako, nikikimbia kweny rehema zako, nikiwa na uhakika kwamba hakuna anaye weza kuniokoa kutokana ghadhabu zako, na hakuna anayeweza kunilinda nawe.
  70. Basi nirudie (urudishe uso wako kwangu) na unisamehe kwa msamaha wako kupitia kile kinachopelekea kurudi (kurudisha uso wako) kwa yule aliye fanya dhambi, na unikirimu kupitia kile kinachofanya uwakirimu wale walio nyosha mikono yao kwako wakitaraji msamaha wako, na uniruzuku toba yako kwani si jambo kubwa kumsamehe yule mwenye matumaini ya msamaha wako.
  71. Ee Mwenyezi Mungu, nijaalie katika siku hii fungu maalumu ambalo kwalo nitaweza kupata bahati ya kufikia radhi zako, na usinirudishe mikono mitupu kutoka miongoni mwa waja wako wanaokuabudu.
  72. Na ingawa sikutenda mema kama walivyoyafanya, ila nime utanguliza mbele upweke wako, na kukutakasa kutokana na wapinzani, na wenza, na kukutakasa kutokana na kukufananisha. Nimekuja kwako kupitia milango uliyoamrisha kuja kwako kupitia kwayo, na nime kukaribia kwa kile ambacho hakuna mtu anaye weza kukukaribia isipokuwa kupitia hicho.
  73. Kisha nikafuatilisha mambo hayo; kurudi kwako, unyenyekevu, kujisalimisha kwako, kudhania dhana njema juu yako, na imani kwa kile kilichoko kwako (rehema zako). Nikataka shufaa kwa kukutumainia Wewe (kwa kutumainia matumani Yako), matumaini ambayo ni mara chache hufeli wanaokutumainia.
  74. Nikakuomba kwa maombi ya mnyonge, dhalili, mwenye taabu, maskini, mwenye hofu, na mwenye kuomba hifadhi. Maombi ambayo yameshikamana na; hofu, unyenyekevu, maombi ya hifadhi, na kujitupa kwako, bila kujidai kwa kiburi cha wenye kiburi, au kujikweza na kujipa daraja ya wachamungu, au kujidhania ni miongoni mwa wenye daraja ya kustahiki kupata shufaa.
  75. Na bado mimi ni mdogo kuliko wadogo, na mwenye unyonge kuliko wanyonge, na mfano wangu ni kama chembe tu au chini yake. Basi Ee Mwenye Ezi Mungu ambaye hufanyi haraka hauwaadhibu waovu, wala kuwasumbua wenye kuneemeka kwa starehe zao, Ee Mwenyezi Mungu ambaye huwasaidia watelezao, na huwafadhili watendao makosa kwa kuwapa muda (ili waweze kutubu).
  76. Mimi ni mbaya, mwenye kukiri, mwenye dhambi, na mteleza (aliye jikwaa).
  77. Mimi ndiye niliyekuja kwako kwa ujasiri (wa kukiri).
  78. Mimi ndiye niliye kuasi kwa makusudi.
  79. Mimi ndiye niliyejificha kwa waja wako na kujidhihirisha mbele yako.
  80. Mimi ndiye niliye waogopa waja wako na kukuamini Wewe (kwamba utanipa amani).
  81. Mimi ndiye yule ambaye hakuogopa mamlaka yako, wala hakukhofu nguvu zako.
  82. Mimi ndiye yule mkosaji aliye tenda makossa dhidi yake mwenyewe.
  83. Mimi ndiye ambaye nimefungwa (niliyeko rehani) kupitia mitihani yake mwenyewe.
  84. Mimi ndiye yule mwenye haya chache.
  85. Mimi ndiye yule mwenye msiba wa muda mrefu.
  86. Kwa haki ya yule uliyemteua miongoni mwa viumbe vyako, na yule uliyemchagua kwa ajili yako wewe mwenyewe, kwa haki ya yule uliyemchagua kutoka katika viumbe vyako, na yule uliyemchagua kwa ajili ya mambo yako, kwa haki ya yule uliye iunganisha taa yake kwenye taa yako (yaa kumtii yeye ni sawa na kukutii wewe), na yule uliyemfanya kumuasi yeye ni sawa na kukuasi wewe, kwa haki ya yule uliyemfanya kuufuata uongozi wake ni sawa na kuufuata uongozi wako wewe, na yule uliyemfanya kuwa kumfanyia adui yeye ni sawa na kukufanyia wewe uadui, nifunike katika siku hii yaleo na kile unachomfunika nacho yule anayekimbilia kwako kwa unyenyekevu, na akajikinga kwa msamaha wako kwa kupitia toba.
  87. Na niongoze kwa kile unacho waongozea wale wanaotii na wale walio karibu nawe na ulio wapa hadhi yako.
  88. Na unipe umakhususi kwa kile kinachopelekea umakhususi kwa yule anaye timiza ahadi yako, na anayejitolea kwa ajili yako, na anaye jitahidi kwa ajili ya kupata radhi zako.
  89. Na usinichukulie na kuniadhibu kwa kuzembea kwangu katika kutekeleza haki Zako, na kuvuka mipaka Yako, na kukiuka amri zako.
  90. Na usiniachie nikatokomea kwa kunipuruzia kamba kama mpuruzio wa yule aliye ninyima kheri alizo nazo (miongoni mwa matajiri) na wala hakukuunga mkono katika kunisaidia kwa kunineemesha kwa neema alizo nazo.
  91. Na nizindue kutoka katika usingizini wa wajinga, na unitoe katika usingizi wa wabadhirifu (watendao israfu), na unizindue kutokana na lepe la usingizi na ulegevu wa waliotelekezwa na kukandamizwa.
  92. Chukua moyo wangu na uuelekeze kuutumia kwenye kile ulichowaamuru kukitekeleza wale wenye kukutii, na kwenye ibada ambayo imewataka kuifanya wale wenye kukuabudu, na kwenye kile amabcho kimepelekea kuwaokoa waliopotea wenye kudharau.
  93. Nilinde na kile kinacho niweka mbali nawe, na kinachosimama kati yangu na fungu (nafasi) ulio niwekea kwako, na kinachonizuia nisifanye kile ninacho jaribu kufanya kwa ajili yako.
  94. Nisahilishie njia ya mema yenye kuelekea kwako, na n iwafikishe kushindana katika kufuata njia hiyo kwa vile ulivyo amuru, na niingie kwenye mashindano hayo kwa kile ulicho kitaka.
  95. Na usiniangamize pamoja na wale unao waangamiza kwa sababu ya kudharau kwao kile ulicho kitahadharisha.
  96. Na wala usinihilikishe pamoja na wale unaowaangamiza kwa sababu ya kujiweka katika ghadhabu Yako (walio jisababishia ghadhabu Yako).
  97. Na wala usiniponde (usinikunje) kunisonga pamoja na wale unao waangamiza kwa sababu ya kupotoka na kukaa nje ya njia zako.
  98. Na uniokoe kutokana na mawimbi ya fitina, na uniepushe kutokana na mvuto wa mambo yanayo fitinisha na kupotosha, na niokoe kutokana na maghafiliko ya kupuruziwa kamba.
  99. Tenganisha na uweke kizuizi kati yangu na adui anaye nipotosha, na tamaa ya nafsi inayo niangamiza, na kasoro inayo nilemea.
  100. Na wala usigeuze uso wako kutoka kwangu kama unavyogeuza uso wako kwa yule usiyeridhika naye baada ya kughadhibika naye.
  101. Na wala usikatishe matumaini yangu kwako, hadi kukata tamaa kukapindua matarajio ya kupata rehema zako.
  102. Na wala usinipe kile ambacho sina uwezo wa stahamala nacho (kilichopindukia uwezo wangu wa kukihimili), ili nisije kuporomoka kutokana wingi wa na uzito mapenzi yako juu yangu.
  103. Na wala usiniachia nikapuruzika kutoka mikononi mwako kama anavyopuruzika yule ambaye hana kheri wala manufaa, wala huna haja naye, wala hana njia ya kurudi kwako (njia ya kutubia).
  104. Na wala usinilembee mlembeo wa yule aliye anguka kutoka kwenye macho ya ulinzi (uchungaji) wako, na ambaye amevawa na fedheha Zako (kutokana na kutengana Nawe). Bali nishike mkono na univushe kutoka kwenye maanguko ya wanaorudi nyuma, na kutoka kwenye mshtuko wa wanaopotea, na mtelezo wa waliodanganywa (na Shetani au nafsi zao), na kutoka kwenye mtego wa walio potea.
  105. Na niokoe kutokana na kile ulichowajaribu nacho watu wa matabaka mbali mbali ya waja wako na wajakazi wako (waja wako wa kike), na nifikishe kwenye malengo ya yule uliye mjali, na ukamhifadhi, na ukaridhika naye, kwa hiyo maisha mema yenye kuhimidiwa, na ukamfisha hali akiwa ni mwenye kufuzu.
  106. Na nivishe shingoni mwangu mnyororo wa kunizuia na kuacha kile kinabatilisha matendo mema, na kinachoondoa baraka.
  107. Na uhisishe moyo wangu hisia ya kukata na kutengana na maovu, na usitiri na fedheha za makosa.
  108. Usinitie kwenye kazi ya kuzunguka kwa ajili ya kutafuta kile ambacho siwezi kukipata isipokuwa kupitia kwako Wewe tu, nikaachana na kile ambacho siwezi kupata radhi zako ila kwacho (yaani ibada yako).
  109. Na ondoa kutoka kwenye moyo wangu upendo wa dunia ambayo ni duni kiuhalisia, dunia ambayo ni kizuizi baina yangu na kile kilicho kwako (neema na radhi zako), na yenye kunizuia katika kutafuta njia ya kuelekea kwako, na inasababisha kughafilika na kusahau kujikurubisha kwako.
  110. Na unipambie tendo la kufaraghika Nawe usiku na mchana nikiwa katika hali ya zungumza, kukuomba na kukubembeleza.
  111. Na unipe ulinzi wa kunilinda na dhambi (isma) utakaonileta karibu na khofu yako, na utakao niachisha na kufanya kuyaendea makatazo yako, na utakao nitoa katika utumwa wa makosa adhimu.
  112. Na nipe utakaso kutokana na uchafu wa maasi, na uniondolee uchafu wa madhambi, na unifunike nguo ya ponyo Lako, na unifunike vazi la usamehevu Wako, na nifunike kwa ukarimu wa neema zako, dhihirisha kwangu fadhila zako na ukarimu wako.
  113. Na niunge mkono kwa taufiki yako na miongozo yako, na nisaidie kwenye kuielekea nia njema, na kauli zinazoridhisha, na matendo yenye kupendeza, na usiniachie nikategemea nguvu zangu na uwezo wangu bila ya kuniunga mkono kwa nguvu zako na uwezo wako.
  114. Na wala usinifedheheshe siku utakaponiamsha (utakapo nifufua) kukutana nawe, wala usinidhalilishe mbele ya wapenzi wako, wala usinisahaulishe kukutaja (kukudhukuri), wala usiniondolee neema ya kukushukuru, bali nifungamanishe na kuikumbuka shukurani yako hata katika hali ya uzembe na kusahau, wakati ambao wajinga husahau kuzishukuru neema zako, na niwezeshe kukumsifu (kukushukuru) kwa yale uliyonipa, na nikiri kwa yale mema uliyo nifanyia.
  115. Na ifanye shauku yangu kukuelekea Wewe, iwe ni kubwa kuliko shauku ya wote wenye hamu Nawe, na jaalia shukurani (sifa) zangu kwako ziwe ni kubwa zaidi kuliko shukurani za wote wanao kusifu (wanao kukushukuru).
  116. Na wala usinidhalilishe pale ninapokuhitajia (ninapokuwa na shida Nawe), wala usiniangamizwe kwa yale niliyokutendea, wala usinihukumu kama ulivyohukumu wapinzani wako (wenye usugu wa kutii amri zako). Kwa maana mimi ni mtii wako, na ninajua kwamba hoja haki ni yako Wewe, na ninaelewa ya kwamba Wewe ndiye mwenye kustahiki zaidi katika kuwafadhili na kuwasamehe waja wako, na kutendea hisani ndia ada na kawaida yako, na Wewe ndiye mwenye kustahiki taqwa, na Wewe ni mwenye kutanguliza na kuweka mbele usamehevu wako, na Wewe ni mbora kusamehe kuliko kuadhibu, na kusitiri mbele yako Wewe ni jambo la karibu zaidi kuliko kufedhehesha.
  117. Basi nihuishe maisha mazuri ambayo yanaendana na kile ninachotaka, na yanafikia kiwango chake na kile ninacho kipenda, ila isije kupelekea kutenda kile ambacho unachokichukia, na wala isipelekee kufanya kile ulichonikataza, na nifeshe kifo cha mtu ambaye nuru yake inatangulia mbeleni kwake na kuliani kwake.
  118. Na unifanye niwe mnyenyekevu (dhalili) mbele yako, na uniinue na kunifanya mtukufu mbele ya viumbe vyako, na unishushe chini pale ninapokuwa peke yangu ambapo ninafaraghika nawe, na uniinu juu mbele ya waja wako, na unifanye niwe ni mwenye kutosheka mbele ya yule mwenye mali (tajiri) kuliko mimi, na unizidishie unyonge na mahitajio yangu kwao Wewe.
  119. Na nihifadhi kutoka kwa dhihaka za maadui, na kutoka kwa majanga yanayotokea, na kutokana na unyonge na shida, nisamehe katika kile ulichokifahamu kutoka kwangu kupitia usamehevu ambao Muweza huutumia katika kusamehe waja wake, ambapo lau kama si usamehevu huo, basi angeliwaadhibu, na lau kama si kukimbilia kwako (kwa kukutaka toba), basi ungelimtia adabu.
  120. Na pale unapo kusudia kuwatia fitna au kuwaadhibu watu fulani, basi niokoe na fitna hiyo kutokana kimbilio lango kwako wewe, na kwa vile hukunifedhehesha duniani mwako, basi pia usinifedheheshe katika akhera yako.
  121. Na uniruzuku kwa neema zako za duniani na za Akhera, na unifidishe kwa faida zako za mwanzoni zenye kuoana na zile zinazo jitokeza kwa uendelevu wa zama. Usinipe umri mrefu, ili nisije tahinika kwa mtihani wa kupata usugu wa moyo wangu, wala usinitahini kwa mtihani ambao utapoteza hadhi yangu. Wala usinifanye mnyonge ikapelekea kuanguka kwa thamani yangu, wala usinipe mapungufu yasababishayo kusahaulika nu kupuzwa kwa nafasi yangu.
  122. Na usinifanye nihisi hofu ambayo itanifanya nikate tamaa, wala usinifanye nihisi woga ambao utanitia wasiwasi. Bali ijaalie hofu yangu kwenye matishio yako, na jaalia hadhari yangu iwe matahadharizho yako na onyo lako. Na jaalia woga wangu mkubwa uwe pale ninaposoma Aya zako.
  123. Na uimarishe usiku wangu kwa kunifanya niamke ndani yake kwa ajili ya kukuabudu, na kwa kujitenga (kufaraghika) kwangu kwa ajili ya kutahajudi (kusali sala za usiku) kwa ajili yako, na upweke wangu kwa kukunyeyekea ka ajili ya kufikia utulivu wa moyo wangu kupitia kwako, na kuomba haja zangu kwako, na kujipapatua mbele yako ili kukomboa shingo yangu kutokana minyororo ya moto wako, na kutafuta njia yako ya kuepukana na kile ambacho wakazi wa moto huo kimewapelekea kubaki katika adhabu yako.
  124. Na usiniache niendelee kubaki katika uasi na upofu wangu, wala katika upotevu wangu hali nikiwa nimejisahahu kwa kipindi fulani, wala usinifanya kuwa ni fundisho kwa yule aliyejifunza kupitia makossa ya wengine, wala kuwa ni ashirio la mazingatio kwa yule anayepata mazingatio kupitia wengine, wala niswe ni fitina ya kuwafitinisha wenye kuangali matendo ya wengine, wala usinite mikononi mwako ukanifanya miongoni mwa unaowatia mikononi mwako, wala usinibadilishe na ukamweka mwingine katika nafasi yangu, wala usibadilishe jina langu (hadhi yangu), wala usibadilishe mwili wangu (ukaupa umbile jengine), wala usinifanye kuwa ni kejeli kwa viumbe wako, wala dhihaka (mwenye kudharaulika) kwako, wala usinipe utumwa kutenda jambo isipokuwa kwa ajili ya radhi zako, na wala usinifanye kuwa ni mwenye kujitolea isipokuwa kwa kwa ajili ya kulipiza kisasi chako.
  125. Na unipatie ladha baridi ya msamaha wako, na unionjeshe utamu wa rehema zako na starehe yako, na harufu yako njema ya manukato ya Pepo yako, na bustani ya neema yako, na unipe ladha ya kufaraghika katika kutenda yale unayopenda mtu kujitahidi nayo, na nipe ladha ya juhudi katika kutenda yale yanayo kurubisha kwako na kupelekea kufikia hadhi maalumu mbele yako, na unitunuku kwa tunuko maalumu kati ya tunuko zako.
  126. Na ufanye biashara (amali) yangu iwe ni yenye faida, na mapambano yangu yasiwe na hasara (yasipotee bure), na unikhofishe juu ya ukuu wako na nafasi, na nipe shauku ya kukutana nawe, na unipe taufiki ya kuomba maghufira kwa kutubia toba ya kweli isio na mzaha, ambayo hataacha dhambi ndogo wala kubwa, wala haito acha dhambi ya dhahiri wala ya siri.
  127. Na uondoe fungo lililoko kifuani mwangu kwa ajili ya waaminifu (nililo wawekea waumini), na ulainishe moyo wangu kwa ajili ya wanyenyekevu wako, na niamili (usimame upande wangu) mimi kama unavyo waamili watenda wema, na unipambe kwa pambo la wachamungu, na unfanye utajo wangu utajwe kwa wema na wale watakao kuja baada yangu, na ufanye wangu huo uwe ni endelevu kwa watakao kuja baadae, na uniweke katika daraja ya wale wenye daraja za juu kabisa miongoni mwa waja wako.
  128. Na nitimizie utimilifu wa neema zako juu yangu, na unibainishie baraka zake (uadhimu wa neema hizo), jaza manufaa yako (neema zako) kwenye mikono yangu, na nimiminie fadhila za tunuko Zako kangu mimi (zitiririshe na uzielekeze fadhila za tunuko Zako kwangu mimi), na unijiranishe na watu wema (nizungushie majirani wema), miongoni mwa wapenzi wako huko Peponi, Pepo ambazo umezipamba kwa ajili ya wapenzi wako, na univishe vazi la neema zako kutoka katika nafasi zilizoandaliwa kwa ajili ya wapenzi wako.
  129. Na nijaalie nipate mahala pema kwako, mahala ambapo nitaweza kukimbilia na kupata utulivu ndani yake, na mashukio (marejeo) ambayo nitaweza kushuka na kubaki ndani yake, na kupata faraja ya macho yangu, wala usinilinganishe na ukubwa wa maovu (yangu), wala usiniangamize siku ambayo siri (za waja) zitafunuliwa na kuanikwa, na niondolee shaka na dhana tata, na ijaalie njia ya haki iwe ndio njia ya kufikia kila aina ya rehema zako, na unipe fungu maalumu la tunuko kutoka katika jaza zako, na nikithirishie (nipe kwa wingi) bahati ya hisani ya ukarimu wa fadhila zako.
  130. Na ufanye moyo wangu uwe na uhakika na kile kilichoko kwako (ili niwe na yakini na thawabu zako), na niachane na shughuli nyengine kwa ajili ya kufaraghika na shughuli zako (za kukuabudu wewe), na unitumie (kama ninyenzo yako) katika kile unachowatumia kwa ajili ya yake waja wako maalumu, na unywishe moyo wangu hahi uroane kwa ibada zako, jambo ambalo litapelekea kuendelea kukutii hata katika nyakati za kughafilika na kutokwa na akili, na nipe utajiri, na kutosheka na maisha ya wastani, na usahili wa maisha, niweke mbali na mabaya, nipe siha, wasaa, utulivu, na ustawi wa afya.
  131. Na wala usiyapoteze (usibatilishe) mema wangu kwa kutokana kuchanganyika kwa mema hayo na matendo ya uasi wangu dhidi yako, na wala usibatilishe faragha zangu kwa kile kinachonijia (mitikiso) miongoni mwa majaribu yako, na zilinde haya za uso wangu kwa kunizuia kuomba kutoka kwa yeyote yule miongoni mwa walimwengu, na niepushe na kukodolea macho (kutamani) kile kilichoko mikononi waovu (mapambo ya kidunia walio nayo waovu).
  132. Na wala usinifanya niwe msaidizi wa waovu, wala nisiwe ni mkono wao (nyenzo) wala msaidizi wao katika kufuta (kubutusha) kitabu chako (maamrisho yako), na nilinde kutokana na mabaya kwa ulinzi ambao sina habari nao (bila ya hata mimi mwenyewe kuelewa), na nifungulie milango ya toba yako, rehema zako, huruma zako, na riziki zako zenye wasaa. Hakika mimi ni miongoni mwa shauku Nawe, na nikamilishie neema zako, hakika wewe ndiye mbora wa waneemeshaji.
  133. Na yajaalie maisha yangu yaliyosalia katika ibada (hii) ya Hajj na Umra niyatumie katika kutafuta radhi zako, Ewe Mola wa walimwengu. Na mshishie rehema zako Muhammad na Aali zake watakatifu waliotoharika, na amani yako iwe juu yake (Muhammad) na juu yao (Aali zake) daima dawama.


وَ كَانَ مِنْ دُعَائِهِ عَلَیهِ السَّلَامُ فِی یوْمِ عَرَفَةَ

(1) الْحَمْدُ للهِ رَبِّ الْعالَمِینَ‏ (2) اللهُمَّ لَكَ الْحَمْدُ بَدِیعَ السَّمَاوَاتِ وَ الْأَرْضِ، ذَا الْجَلَالِ وَ الْإِكْرَامِ، رَبَّ الْأَرْبَابِ، وَ إِلَهَ كُلِّ مَأْلُوهٍ، وَ خَالِقَ كُلِّ مَخْلُوقٍ، وَ وَارِثَ كُلِّ شَی‏ءٍ، لَیسَ كَمِثْلِهِ شَی‏ءٌ، وَ لَا یعْزُبُ عَنْهُ عِلْمُ شَی‏ءٍ، وَ هُوَ بِكُلِّ شَی‏ءٍ مُحِیطٌ، وَ هُوَ عَلَی كُلِّ شَی‏ءٍ رَقِیبٌ.(3) أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، الْأَحَدُ الْمُتَوَحِّدُ الْفَرْدُ الْمُتَفَرِّدُ (۴) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، الْكَرِیمُ الْمُتَكَرِّمُ، الْعَظِیمُ الْمُتَعَظِّمُ، الْكَبِیرُ الْمُتَكَبِّرُ (۵) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، الْعَلِی الْمُتَعَالِ، الشَّدِیدُ الْمِحَالِ (۶) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، الرَّحْمَنُ الرَّحِیمُ، الْعَلِیمُ الْحَكِیمُ. (۷) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، السَّمِیعُ الْبَصِیرُ، الْقَدِیمُ الْخَبِیرُ (۸) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، الْكَرِیمُ الْأَكْرَمُ، الدَّائِمُ الْأَدْوَمُ، (۹) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، الْأَوَّلُ قَبْلَ كُلِّ أَحَدٍ، وَ الْآخِرُ بَعْدَ كُلِّ عَدَدٍ (۱۰) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، الدَّانِی فِی عُلُوِّهِ، وَ الْعَالِی فِی دُنُوِّهِ (۱۱) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، ذُو الْبَهَاءِ وَ الْمَجْدِ، وَ الْكِبْرِیاءِ وَ الْحَمْدِ (۱۲) وَ أَنْتَ اللهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، الَّذِی أَنْشَأْتَ الْأَشْیاءَ مِنْ غَیرِ سِنْخٍ، وَ صَوَّرْتَ مَا صَوَّرْتَ مِنْ غَیرِ مِثَالٍ، وَ ابْتَدَعْتَ الْمُبْتَدَعَاتِ بِلَا احْتِذَاءٍ. (۱۳) أَنْتَ الَّذِی قَدَّرْتَ كُلَّ شَی‏ءٍ تَقْدِیراً، وَ یسَّرْتَ كُلَّ شَی‏ءٍ تَیسِیراً، وَ دَبَّرْتَ مَا دُونَكَ تَدْبِیراً (۱۴) أَنْتَ الَّذِی لَمْ یُعِنْكَ عَلَی خَلْقِكَ شَرِیكٌ، وَ لَمْ یُوَازِرْكَ فِی أَمْرِكَ وَزِیرٌ، وَ لَمْ یكُنْ لَكَ مُشَاهِدٌ وَ لَا نَظِیرٌ. (۱۵) أَنْتَ الَّذِی أَرَدْتَ فَكَانَ حَتْماً مَا أَرَدْتَ، وَ قَضَیتَ فَكَانَ عَدْلًا مَا قَضَیتَ، وَ حَكَمْتَ فَكَانَ نِصْفاً مَا حَكَمْتَ. (۱۶) أَنْتَ الَّذِی لَا یحْوِیكَ مَكَانٌ، وَ لَمْ یقُمْ لِسُلْطَانِكَ سُلْطَانٌ، وَ لَمْ یعْیكَ بُرْهَانٌ وَ لَا بَیانٌ. (۱۷) أَنْتَ الَّذِی أَحْصَیتَ‏ كُلَّ شَی‏ءٍ عَدَداً، وَ جَعَلْتَ لِكُلِّ شَی‏ءٍ أَمَداً، وَ قَدَّرْتَ كُلَّ شَی‏ءٍ تَقْدِیراً. (۱۸) أَنْتَ الَّذِی قَصُرَتِ الْأَوْهَامُ عَنْ ذَاتِیتِكَ، وَ عَجَزَتِ الْأَفْهَامُ عَنْ كَیفِیتِكَ، وَ لَمْ تُدْرِكِ الْأَبْصَارُ مَوْضِعَ أَینِیتِكَ. (۱۹) أَنْتَ الَّذِی لَا تُحَدُّ فَتَكُونَ مَحْدُوداً، وَ لَمْ تُمَثَّلْ فَتَكُونَ مَوْجُوداً، وَ لَمْ تَلِدْ فَتَكُونَ مَوْلُوداً. (۲۰) أَنْتَ الَّذِی لَا ضِدَّ مَعَكَ فَیعَانِدَكَ، وَ لَا عِدْلَ لَكَ فَیكَاثِرَكَ، وَ لَا نِدَّ لَكَ فَیعَارِضَكَ. (۲۱) أَنْتَ الَّذِی ابْتَدَأَ، وَ اخْتَرَعَ، وَ اسْتَحْدَثَ، وَ ابْتَدَعَ، وَ أَحْسَنَ صُنْعَ مَا صَنَعَ. (۲۲) سُبْحَانَكَ! مَا أَجَلَّ شَأْنَكَ، وَ أَسْنَی فِی الْأَمَاكِنِ مَكَانَكَ، وَ أَصْدَعَ بِالْحَقِّ فُرْقَانَكَ! (۲۳) سُبْحَانَكَ! مِنْ لَطِیفٍ مَا أَلْطَفَكَ، وَ رَءُوفٍ مَا أَرْأَفَكَ، وَ حَكِیمٍ مَا أَعْرَفَكَ! (۲۴) سُبْحَانَكَ! مِنْ مَلِیكٍ مَا أَمْنَعَكَ، وَ جَوَادٍ مَا أَوْسَعَكَ، وَ رَفِیعٍ مَا أَرْفَعَكَ! ذُو الْبَهَاءِ وَ الْمَجْدِ وَ الْكِبْرِیاءِ وَ الْحَمْدِ. (۲۵) سُبْحَانَكَ! بَسَطْتَ بِالْخَیرَاتِ یدَكَ، وَ عُرِفَتِ الْهِدَایةُ مِنْ عِنْدِكَ، فَمَنِ الْتَمَسَكَ لِدِینٍ أَوْ دُنْیا وَجَدَكَ! (۲۶) سُبْحَانَكَ! خَضَعَ لَكَ مَنْ جَرَی فِی عِلْمِكَ، وَ خَشَعَ لِعَظَمَتِكَ مَا دُونَ عَرْشِكَ، وَ انْقَادَ لِلتَّسْلِیمِ لَكَ كُلُّ خَلْقِكَ! (۲۷) سُبْحَانَكَ! لَا تُحَسُّ وَ لَا تُجَسُّ وَ لَا تُمَسُّ وَ لَا تُكَادُ وَ لَا تُمَاطُ وَ لَا تُنَازَعُ وَ لَا تُجَارَی وَ لَا تُمَارَی وَ لَا تُخَادَعُ وَ لَا تُمَاكَرُ! (۲۸) سُبْحَانَكَ! سَبِیلُكَ جَدَدٌ. وَ أَمْرُكَ رَشَدٌ، وَ أَنْتَ حَی صَمَدٌ. (۲۹) سُبْحَانَكَ! قَولُكَ حُكْمٌ، وَ قَضَاؤُكَ حَتْمٌ، وَ إِرَادَتُكَ عَزْمٌ! (۳۰) سُبْحَانَكَ! لَا رَادَّ لِمَشِیتِكَ، وَ لَا مُبَدِّلَ لِكَلِمَاتِكَ!. (۳۱) سُبْحَانَكَ! بَاهِرَ الْآیاتِ، فَاطِرَ السَّمَاوَاتِ، بَارِئَ النَّسَمَاتِ! (۳۲) لَكَ الْحَمْدُ حَمْداً یدُومُ بِدَوَامِكَ (۳۳) وَ لَكَ الْحَمْدُ حَمْداً خَالِداً بِنِعْمَتِكَ. (۳۴) وَ لَكَ الْحَمْدُ حَمْداً یوَازِی صُنْعَكَ (۳۵) وَ لَكَ الْحَمْدُ حَمْداً یزِیدُ عَلَی رِضَاكَ. (۳۶) وَ لَكَ الْحَمْدُ حَمْداً مَعَ حَمْدِ كُلِّ حَامِدٍ، وَ شُكْراً یقْصُرُ عَنْهُ شُكْرُ كُلِّ شَاكِرٍ (۳۷) حَمْداً لَا ینْبَغِی إِلَّا لَكَ، وَ لَا یتَقَرَّبُ بِهِ إِلَّا إِلَیكَ (۳۸) حَمْداً یسْتَدَامُ بِهِ الْأَوَّلُ، وَ یسْتَدْعَی بِهِ دَوَامُ الْآخِرِ. (۳۹) حَمْداً یتَضَاعَفُ عَلَی كُرُورِ الْأَزْمِنَةِ، وَ یتَزَایدُ أَضْعَافاً مُتَرَادِفَةً. (۴۰) حَمْداً یعْجِزُ عَنْ إِحْصَائِهِ الْحَفَظَةُ، وَ یزِیدُ عَلَی مَا أَحْصَتْهُ فِی كِتَابِكَ الْكَتَبَةُ (۴۱) حَمْداً یوازِنُ عَرْشَكَ الْمَجِیدَ وَ یعَادِلُ كُرْسِیكَ الرَّفِیعَ. (۴۲) حَمْداً یكْمُلُ لَدَیكَ ثَوَابُهُ، وَ یسْتَغْرِقُ كُلَّ جَزَاءٍ جَزَاؤُهُ (۴۳) حَمْداً ظَاهِرُهُ وَفْقٌ لِبَاطِنِهِ، وَ بَاطِنُهُ وَفْقٌ لِصِدْقِ النِّیةِ (۴۴) حَمْداً لَمْ یحْمَدْكَ خَلْقٌ مِثْلَهُ، وَ لَا یعْرِفُ أَحَدٌ سِوَاكَ فَضْلَهُ (۴۵) حَمْداً یعَانُ مَنِ اجْتَهَدَ فِی تَعْدِیدِهِ، وَ یؤَیدُ مَنْ أَغْرَقَ نَزْعاً فِی تَوْفِیتِهِ. (۴۶) حَمْداً یجْمَعُ مَا خَلَقْتَ مِنَ الْحَمْدِ، وَ ینْتَظِمُ مَا أَنْتَ خَالِقُهُ مِنْ بَعْدُ. (۴۷) حَمْداً لَا حَمْدَ أَقْرَبُ إِلَی قَوْلِكَ مِنْهُ، وَ لَا أَحْمَدَ مِمَّنْ یحْمَدُكَ بِهِ. (۴۸) حَمْداً یوجِبُ بِكَرَمِكَ الْمَزِیدَ بِوُفُورِهِ، وَ تَصِلُهُ بِمَزِیدٍ بَعْدَ مَزِیدٍ طَوْلًا مِنْكَ‏ (۴۹) حَمْداً یجِبُ لِكَرَمِ وَجْهِكَ، وَ یقَابِلُ عِزَّ جَلَالِكَ. (۵۰) رَبِّ صَلِّ عَلَی مُحَمَّدٍ وَ آلِ مُحَمَّدٍ، الْمُنْتَجَبِ الْمُصْطَفَی الْمُكَرَّمِ الْمُقَرَّبِ، أَفْضَلَ صَلَوَاتِكَ، وَ بَارِكْ عَلَیهِ أَتَمَّ بَرَكَاتِكَ، وَ تَرَحَّمْ عَلَیهِ أَمْتَعَ رَحَمَاتِكَ. (۵۱) رَبِّ صَلِّ عَلَی مُحَمَّدٍ وَ آلِهِ، صَلَاةً زَاكِیةً لَا تَكُونُ صَلَاةٌ أَزْكَی مِنْهَا، وَ صَلِّ عَلَیهِ صَلَاةً نَامِیةً لَا تَكُونُ صَلَاةٌ أَنْمَی مِنْهَا، وَ صَلِّ عَلَیهِ صَلَاةً رَاضِیةً لَا تَكُونُ صَلَاةٌ فَوْقَهَا. (۵۲) رَبِّ صَلِّ عَلَی مُحَمَّدٍ وَ آلِهِ، صَلَاةً تُرْضِیهِ وَ تَزِیدُ عَلَی رِضَاهُ، وَ صَلِّ عَلَیهِ صَلَاةً تُرْضِیكَ و تَزِیدُ عَلَی رِضَاكَ لَهُ وَ صَلِّ عَلَیهِ صَلَاةً لَا تَرْضَی لَهُ إِلَّا بِهَا، وَ لَا تَرَی غَیرَهُ لَهَا أَهْلًا. (۵۳) رَبِّ صَلِّ عَلَی مُحَمَّدٍ وَ آلِهِ صَلَاةً تُجَاوِزُ رِضْوَانَكَ، وَ یتَّصِلُ اتِّصَالُهَا بِبَقَائِكَ، وَ لَا ینْفَدُ كَمَا لَا تَنْفَدُ كَلِمَاتُكَ. (۵۴) رَبِّ صَلِّ عَلَی مُحَمَّدٍ وَ آلِهِ، صَلَاةً تَنْتَظِمُ صَلَوَاتِ مَلَائِكَتِكَ وَ أَنْبِیائِكَ وَ رُسُلِكَ وَ أَهْلِ طَاعَتِكَ، وَ تَشْتَمِلُ عَلَی صَلَوَاتِ عِبَادِكَ مِنْ جِنِّكَ وَ إِنْسِكَ وَ أَهْلِ إِجَابَتِكَ، وَ تَجْتَمِعُ عَلَی صَلَاةِ كُلِّ مَنْ ذَرَأْتَ وَ بَرَأْتَ مِنْ أَصْنَافِ خَلْقِكَ. (۵۵) رَبِّ صَلِّ عَلَیهِ وَ آلِهِ، صَلَاةً تُحِیطُ بِكُلِّ صَلَاةٍ سَالِفَةٍ وَ مُسْتَأْنَفَةٍ، وَ صَلِّ عَلَیهِ وَ عَلَی آلِهِ، صَلَاةً مَرْضِیةً لَكَ وَ لِمَنْ دُونَكَ، وَ تُنْشِئُ مَعَ ذَلِكَ صَلَوَاتٍ تُضَاعِفُ مَعَهَا تِلْكَ الصَّلَوَاتِ عِنْدَهَا، وَ تَزِیدُهَا عَلَی كُرُورِ الْأَیامِ زِیادَةً فِی تَضَاعِیفَ لَا یعُدُّهَا غَیرُكَ. (۵۶) رَبِّ صَلِّ عَلَی أَطَایبِ أَهْلِ بَیتِهِ الَّذِینَ اخْتَرْتَهُمْ لِأَمْرِكَ، وَ جَعَلْتَهُمْ خَزَنَةَ عِلْمِكَ، وَ حَفَظَةَ دِینِكَ، وَ خُلَفَاءَكَ فِی أَرْضِكَ، وَ حُجَجَكَ عَلَی عِبَادِكَ، وَ طَهَّرْتَهُمْ مِنَ الرِّجْسِ وَ الدَّنَسِ تَطْهِیراً بِإِرَادَتِكَ، وَ جَعَلْتَهُمُ الْوَسِیلَةَ إِلَیكَ، وَ الْمَسْلَكَ إِلَی جَنَّتِكَ‏ (۵۷) رَبِّ صَلِّ عَلَی مُحَمَّدٍ وَ آلِهِ، صَلَاةً تُجْزِلُ لَهُمْ بِهَا مِنْ نِحَلِكَ وَ كَرَامَتِكَ، وَ تُكْمِلُ لَهُمُ الْأَشْیاءَ مِنْ عَطَایاكَ وَ نَوَافِلِكَ، وَ تُوَفِّرُ عَلَیهِمُ الْحَظَّ مِنْ عَوَائِدِكَ وَ فَوَائِدِكَ. (۵۸) رَبِّ صَلِّ عَلَیهِ وَ عَلَیهِمْ صَلَاةً لَا أَمَدَ فِی أَوَّلِهَا، وَ لَا غَایةَ لِأَمَدِهَا، وَ لَا نِهَایةَ لِآخِرِهَا. (۵۹) رَبِّ صَلِّ عَلَیهِمْ زِنَةَ عَرْشِكَ وَ مَا دُونَهُ، وَ مِلْ‏ءَ سَمَاوَاتِكَ وَ مَا فَوْقَهُنَّ، وَ عَدَدَ أَرَضِیكَ وَ مَا تَحْتَهُنَّ وَ مَا بَینَهُنَّ، صَلَاةً تُقَرِّبُهُمْ مِنْكَ زُلْفَی، وَ تَكُونُ لَكَ وَ لَهُمْ رِضًی، وَ مُتَّصِلَةً بِنَظَائِرِهِنَّ أَبَداً. (۶۰) اللهُمَّ إِنَّكَ أَیّدْتَ دِینَكَ فِی كُلِّ أَوَانٍ بِإِمَامٍ أَقَمْتَهُ عَلَماً لِعِبَادِكَ، وَ مَنَاراً فِی بِلَادِكَ بَعْدَ أَنْ وَصَلْتَ حَبْلَهُ بِحَبْلِكَ، وَ جَعَلْتَهُ الذَّرِیعَةَ إِلَی رِضْوَانِكَ، وَ افْتَرَضْتَ طَاعَتَهُ، وَ حَذَّرْتَ مَعْصِیتَهُ، وَ أَمَرْتَ بِامْتِثَالِ أَوَامِرِهِ، وَ الِانْتِهَاءِ عِنْدَ نَهْیهِ، وَ أَلَّا یتَقَدَّمَهُ مُتَقَدِّمٌ، وَ لَا یتَأَخَّرَ عَنْهُ مُتَأَخِّرٌ فَهُوَ عِصْمَةُ اللائِذِینَ، وَ كَهْفُ الْمُؤْمِنِینَ وَ عُرْوَةُ الْمُتَمَسِّكِینَ، وَ بَهَاءُ الْعَالَمِینَ. (۶۱) اللهُمَّ فَأَوْزِعْ لِوَلِیكَ شُكْرَ مَا أَنْعَمْتَ بِهِ عَلَیهِ، وَ أَوْزِعْنَا مِثْلَهُ فِیهِ، وَ آتِهِ‏ مِنْ لَدُنْكَ سُلْطاناً نَصِیراً، وَ افْتَحْ لَهُ فَتْحاً یسِیراً، وَ أَعِنْهُ بِرُكْنِكَ الْأَعَزِّ، وَ اشْدُدْ أَزْرَهُ، وَ قَوِّ عَضُدَهُ، وَ رَاعِهِ بِعَینِكَ، وَ احْمِهِ بِحِفْظِكَ وَ انْصُرْهُ بِمَلَائِكَتِكَ، وَ امْدُدْهُ بِجُنْدِكَ الْأَغْلَبِ. (۶۲) وَ أَقِمْ بِهِ كِتَابَكَ وَ حُدُودَكَ وَ شَرَائِعَكَ وَ سُنَنَ رَسُولِكَ،- صَلَوَاتُكَ اللهُمَّ عَلَیهِ وَ آلِهِ-، وَ أَحْی بِهِ مَا أَمَاتَهُ الظَّالِمُونَ مِنْ مَعَالِمِ دِینِكَ، وَ اجْلُ بِهِ صَدَاءَ الْجَوْرِ عَنْ طَرِیقَتِكَ، وَ أَبِنْ بِهِ الضَّرَّاءَ مِنْ سَبِیلِكَ، وَ أَزِلْ بِهِ النَّاكِبِینَ عَنْ صِرَاطِكَ، وَ امْحَقْ بِهِ بُغَاةَ قَصْدِكَ عِوَجاً (۶۳) وَ أَلِنْ جَانِبَهُ لِأَوْلِیائِكَ، وَ ابْسُطْ یدَهُ عَلَی أَعْدَائِكَ، وَ هَبْ لَنَا رَأْفَتَهُ، وَ رَحْمَتَهُ وَ تَعَطُّفَهُ وَ تَحَنُّنَهُ، وَ اجْعَلْنَا لَهُ سَامِعِینَ مُطِیعِینَ، وَ فِی رِضَاهُ سَاعِینَ، وَ إِلَی نُصْرَتِهِ وَ الْمُدَافَعَةِ عَنْهُ مُكْنِفِینَ، وَ إِلَیكَ وَ إِلَی رَسُولِكَ- صَلَوَاتُكَ اللهُمَّ عَلَیهِ وَ آلِهِ- بِذَلِكَ مُتَقَرِّبِینَ. (۶۴) اللهُمَّ وَ صَلِّ عَلَی أَوْلِیائِهِمُ الْمُعْتَرِفِینَ بِمَقَامِهِمُ، الْمُتَّبِعِینَ مَنْهَجَهُمُ، الْمُقْتَفِینَ آثَارَهُمُ، الْمُسْتَمْسِكِینَ بِعُرْوَتِهِمُ، الْمُتَمَسِّكِینَ بِوِلَایتِهِمُ، الْمُؤْتَمِّینَ بِإِمَامَتِهِمُ، الْمُسَلِّمِینَ لِأَمْرِهِمُ، الْمُجْتَهِدِینَ فِی طَاعَتِهِمُ، الْمُنْتَظِرِینَ أَیامَهُمُ، الْمَادِّینَ إِلَیهِمْ أَعْینَهُمُ، الصَّلَوَاتِ الْمُبَارَكَاتِ الزَّاكِیاتِ النَّامِیاتِ الْغَادِیاتِ الرَّائِحَاتِ. (۶۵) وَ سَلِّمْ عَلَیهِمْ وَ عَلَی أَرْوَاحِهِمْ، وَ اجْمَعْ عَلَی التَّقْوَی أَمْرَهُمْ، وَ أَصْلِحْ لَهُمْ شُئُونَهُمْ، وَ تُبْ عَلَیهِمْ، إِنَّكَ أَنْتَ التَّوَّابُ الرَّحِیمُ‏، وَ خَیرُ الْغافِرِینَ‏، وَ اجْعَلْنَا مَعَهُمْ فِی دَارِ السَّلَامِ بِرَحْمَتِكَ، یا أَرْحَمَ الرَّاحِمِینَ. (۶۶) اللهُمَّ هَذَا یوْمُ عَرَفَةَ یوْمٌ شَرَّفْتَهُ وَ كَرَّمْتَهُ وَ عَظَّمْتَهُ، نَشَرْتَ فِیهِ رَحْمَتَكَ، وَ مَنَنْتَ فِیهِ بِعَفْوِكَ، وَ أَجْزَلْتَ فِیهِ عَطِیتَكَ، وَ تَفَضَّلْتَ بِهِ عَلَی عِبَادِكَ. (۶۷) اللهُمَّ وَ أَنَا عَبْدُكَ الَّذِی أَنْعَمْتَ عَلَیهِ قَبْلَ خَلْقِكَ لَهُ وَ بَعْدَ خَلْقِكَ إِیاهُ، فَجَعَلْتَهُ مِمَّنْ هَدَیتَهُ لِدِینِكَ، وَ وَفَّقْتَهُ لِحَقِّكَ، وَ عَصَمْتَهُ بِحَبْلِكَ، وَ أَدْخَلْتَهُ فِی حِزْبِكَ، وَ أَرْشَدْتَهُ لِمُوَالاةِ أَوْلِیائِكَ، وَ مُعَادَاةِ أَعْدَائِكَ. (۶۸) ثُمَّ أَمَرْتَهُ فَلَمْ یأْتَمِرْ، وَ زَجَرْتَهُ فَلَمْ ینْزَجِرْ، وَ نَهَیتَهُ عَنْ مَعْصِیتِكَ، فَخَالَفَ أَمْرَكَ إِلَی نَهْیكَ، لَا مُعَانَدَةً لَكَ، وَ لَا اسْتِكْبَاراً عَلَیكَ، بَلْ دَعَاهُ هَوَاهُ إِلَی مَا زَیلْتَهُ وَ إِلَی مَا حَذَّرْتَهُ، وَ أَعَانَهُ عَلَی ذَلِكَ عَدُوُّكَ وَ عَدُوُّهُ، فَأَقْدَمَ عَلَیهِ عَارِفاً بِوَعِیدِكَ، رَاجِیاً لِعَفْوِكَ، وَاثِقاً بِتَجَاوُزِكَ، وَ كَانَ أَحَقَّ عِبَادِكَ مَعَ مَا مَنَنْتَ عَلَیهِ أَلَّا یفْعَلَ. (۶۹) وَ هَا أَنَا ذَا بَینَ یدَیكَ صَاغِراً ذَلِیلًا خَاضِعاً خَاشِعاً خَائِفاً، مُعْتَرِفاً بِعَظِیمٍ مِنَ الذُّنُوبِ تَحَمَّلْتُهُ، وَ جَلِیلٍ مِنَ الْخَطَایا اجْتَرَمْتُهُ، مُسْتَجِیراً بِصَفْحِكَ، لَائِذاً بِرَحْمَتِكَ، مُوقِناً أَنَّهُ لَا یجِیرُنِی مِنْكَ مُجِیرٌ، وَ لَا یمْنَعُنِی مِنْكَ مَانِعٌ. (۷۰) فَعُدْ عَلَی بِمَا تَعُودُ بِهِ عَلَی مَنِ اقْتَرَفَ مِنْ تَغَمُّدِكَ، وَ جُدْ عَلَی بِمَا تَجُودُ بِهِ عَلَی مَنْ أَلْقَی بِیدِهِ إِلَیكَ مِنْ عَفْوِكَ، وَ امْنُنْ عَلَیَّ بِمَا لَا یَتَعَاظَمُكَ أَنْ تَمُنَّ بِهِ عَلَی مَنْ أَمَّلَكَ مِنْ غُفْرَانِكَ، (۷۱) وَ اجْعَلْ لِی فِی هَذَا الْیوْمِ نَصِیباً أَنَالُ بِهِ حَظّاً مِنْ رِضْوَانِكَ، وَ لَا تَرُدَّنِی صِفْراً مِمَّا ینْقَلِبُ بِهِ الْمُتَعَبِّدُونَ لَكَ مِنْ عِبَادِكَ (۷۲) وَ إِنِّی وَ إِنْ لَمْ أُقَدِّمْ مَا قَدَّمُوهُ مِنَ الصَّالِحَاتِ فَقَدْ قَدَّمْتُ تَوْحِیدَكَ وَ نَفْی الْأَضْدَادِ وَ الْأَنْدَادِ وَ الْأَشْبَاهِ عَنْكَ، وَ أَتَیتُكَ مِنَ الْأَبْوَابِ الَّتِی أَمَرْتَ أَنْ تُؤْتَی مِنْهَا، وَ تَقَرَّبْتُ إِلَیكَ بِمَا لَا یقْرُبُ أَحَدٌ مِنْكَ إِلَّا بالتَّقَرُّبِ بِهِ. (۷۳) ثُمَّ أَتْبَعْتُ ذَلِكَ بِالْإِنَابَةِ إِلَیكَ، وَ التَّذَلُّلِ وَ الِاسْتِكَانَةِ لَكَ، وَ حُسْنِ الظَّنِّ بِكَ، وَ الثِّقَةِ بِمَا عِنْدَكَ، وَ شَفَعْتُهُ بِرَجَائِكَ الَّذِی قَلَّ مَا یخِیبُ عَلَیهِ رَاجِیكَ. (۷۴) وَ سَأَلْتُكَ مَسْأَلَةَ الْحَقِیرِ الذَّلِیلِ الْبَائِسِ الْفَقِیرِ الْخَائِفِ الْمُسْتَجِیرِ، وَ مَعَ ذَلِكَ خِیفَةً وَ تَضَرُّعاً وَ تَعَوُّذاً وَ تَلَوُّذاً، لَا مُسْتَطِیلًا بِتَكَبُّرِ الْمُتَكَبِّرِینَ، وَ لَا مُتَعَالِیاً بِدَالَّةِ الْمُطِیعِینَ، وَ لَا مُسْتَطِیلًا بِشَفَاعَةِ الشَّافِعِینَ. (۷۵) وَ أَنَا بَعْدُ أَقَلُّ الْأَقَلِّینَ، وَ أَذَلُّ الْأَذَلِّینَ، وَ مِثْلُ الذَّرَّةِ أَوْ دُونَهَا، فَیا مَنْ لَمْ یعَاجِلِ الْمُسِیئِینَ، وَ لَا ینْدَهُ الْمُتْرَفِینَ، وَ یا مَنْ یمُنُّ بِإِقَالَةِ الْعَاثِرِینَ، وَ یتَفَضَّلُ بِإِنْظَارِ الْخَاطِئِینَ. (۷۶) أَنَا الْمُسِی‏ءُ الْمُعْتَرِفُ الْخَاطِئُ الْعَاثِرُ. (۷۷) أَنَا الَّذِی أَقْدَمَ عَلَیكَ مُجْتَرِئاً. (۷۸) أَنَا الَّذِی عَصَاكَ مُتَعَمِّداً. (۷۹) أَنَا الَّذِی اسْتَخْفَی مِنْ عِبَادِكَ وَ بَارَزَكَ. (۸۰) أَنَا الَّذِی هَابَ عِبَادَكَ وَ أَمِنَكَ. (۸۱) أَنَا الَّذِی لَمْ یرْهَبْ سَطْوَتَكَ، وَ لَمْ یخَفْ بَأْسَكَ. (۸۲) أَنَا الْجَانِی عَلَی نَفْسِهِ (۸۳) أَنَا الْمُرْتَهَنُ بِبَلِیّتِهِ. (۸۴) أَنَا القَلِیلُ الْحَیاءِ. (۸۵) أَنَا الطَّوِیلُ الْعَنَاءِ. (۸۶) بِحَقِّ مَنِ انْتَجَبْتَ مِنْ خَلْقِكَ، وَ بِمَنِ اصْطَفَیتَهُ لِنَفْسِكَ، بِحَقِّ مَنِ اخْتَرْتَ مِنْ بَرِیتِكَ، وَ مَنِ اجْتَبَیتَ لِشَأْنِكَ، بِحَقِّ مَنْ وَصَلْتَ طَاعَتَهُ بِطَاعَتِكَ، وَ مَنْ جَعَلْتَ مَعْصِیتَهُ كَمَعْصِیتِكَ، بِحَقِّ مَنْ قَرَنْتَ مُوَالاتَهُ بِمُوَالاتِكَ، وَ مَنْ نُطْتَ مُعَادَاتَهُ بِمُعَادَاتِكَ، تَغَمَّدْنِی فِی یوْمِی هَذَا بِمَا تَتَغَمَّدُ بِهِ مَنْ جَارَ إِلَیكَ مُتَنَصِّلًا، وَ عَاذَ بِاسْتِغْفَارِكَ تَائِباً. (۸۷) وَ تَوَلَّنِی بِمَا تَتَوَلَّی بِهِ أَهْلَ طَاعَتِكَ وَ الزُّلْفَی لَدَیكَ وَ الْمَكَانَةِ مِنْكَ. (۸۸) وَ تَوَحَّدْنِی بِمَا تَتَوَحَّدُ بِهِ مَنْ وَفَی بِعَهْدِكَ، وَ أَتْعَبَ نَفْسَهُ فِی ذَاتِكَ، وَ أَجْهَدَهَا فِی مَرْضَاتِكَ. (۸۹) وَ لَا تُؤَاخِذْنِی بِتَفْرِیطِی فِی جَنْبِكَ، وَ تَعَدِّی طَوْرِی فِی حُدُودِكَ، وَ مُجَاوَزَةِ أَحْكَامِكَ. (۹۰) وَ لَا تَسْتَدْرِجْنِی بِإِمْلَائِكَ لِی اسْتِدْرَاجَ مَنْ مَنَعَنِی خَیرَ مَا عِنْدَهُ وَ لَمْ یشْرَكْكَ فِی حُلُولِ نِعْمَتِهِ بِی. (۹۱) وَ نَبِّهْنِی مِنْ رَقْدَةِ الْغَافِلِینَ، وَ سِنَةِ الْمُسْرِفِینَ، وَ نَعْسَةِ الْمَخْذُولِینَ (۹۲) وَ خُذْ بِقَلْبِی إِلَی مَا اسْتَعْمَلْتَ بِهِ الْقَانِتِینَ، وَ اسْتَعْبَدْتَ بِهِ الْمُتَعَبِّدِینَ، وَ اسْتَنْقَذْتَ بِهِ الْمُتَهَاوِنِینَ. (۹۳) وَ أَعِذْنِی مِمَّا یُبَاعِدُنِی عَنْكَ، وَ یَحُولُ بَینِی وَ بَینَ حَظِّی مِنْكَ، وَ یصُدُّنِی عَمَّا أُحَاوِلُ لَدَیكَ (۹۴) وَ سَهِّلْ لِی مَسْلَكَ الْخَیرَاتِ إِلَیكَ، وَ الْمُسَابَقَةَ إِلَیهَا مِنْ حَیثُ أَمَرْتَ، وَ الْمُشَاحَّةَ فِیهَا عَلَی مَا أَرَدْتَ. (۹۵) وَ لَا تَمْحَقْنِی فِیمَن تَمْحَقُ مِنَ الْمُسْتَخِفِّینَ بِمَا أَوْعَدْتَ (۹۶) وَ لَا تُهْلِكْنِی مَعَ مَنْ تُهْلِكُ مِنَ الْمُتَعَرِّضِینَ لِمَقْتِكَ (۹۷) وَ لَا تُتَبِّرْنِی فِیمَنْ تُتَبِّرُ مِنَ الْمُنْحَرِفِینَ عَنْ سُبُلِكَ‏ (۹۸) وَ نَجِّنِی مِنْ غَمَرَاتِ الْفِتْنَةِ، وَ خَلِّصْنِی مِنْ لَهَوَاتِ الْبَلْوَی، وَ أَجِرْنِی مِنْ أَخْذِ الْإِمْلَاءِ. (۹۹) وَ حُلْ بَینِی وَ بَینَ عَدُوٍّ یضِلُّنِی، وَ هَوًی یوبِقُنِی، وَ مَنْقَصَةٍ تَرْهَقُنِی (۱۰۰) وَ لَا تُعْرِضْ عَنِّی إِعْرَاضَ مَنْ لَا تَرْضَی عَنْهُ بَعْدَ غَضَبِكَ (۱۰۱) وَ لَا تُؤْیسْنِی مِنَ الْأَمَلِ فِیكَ فَیغْلِبَ عَلَی الْقُنُوطُ مِنْ رَحْمَتِكَ (۱۰۲) وَ لَا تَمْنَحْنِی بِمَا لَا طَاقَةَ لِی بِهِ فَتَبْهَظَنِی مِمَّا تُحَمِّلُنِیهِ مِنْ فَضْلِ مَحَبَّتِكَ. (۱۰۳) وَ لَا تُرْسِلْنِی مِنْ یدِكَ إِرْسَالَ مَنْ لَا خَیرَ فِیهِ، وَ لَا حَاجَةَ بِكَ إِلَیهِ، وَ لَا إِنَابَةَ لَهُ (۱۰۴) وَ لَا تَرْمِ بِی رَمْی مَنْ سَقَطَ مِنْ عَینِ رِعَایتِكَ، وَ مَنِ اشْتَمَلَ عَلَیهِ الْخِزْی مِنْ عِنْدِكَ، بَلْ خُذْ بِیدِی مِنْ سَقْطَةِ الْمُتَرَدِّینَ، وَ وَهْلَةِ الْمُتَعَسِّفِینَ، وَ زَلَّةِ الْمَغْرُورِینَ، وَ وَرْطَةِ الْهَالِكِینَ. (۱۰۵) وَ عَافِنِی مِمَّا ابْتَلَیتَ بِهِ طَبَقَاتِ عَبِیدِكَ وَ إِمَائِكَ، وَ بَلِّغْنِی مَبَالِغَ مَنْ عَنَیتَ بِهِ[یادداشت ۱]، وَ أَنْعَمْتَ عَلَیهِ، وَ رَضِیتَ عَنْهُ، فَأَعَشْتَهُ حَمِیداً، وَ تَوَفَّیتَهُ سَعِیداً (۱۰۶) وَ طَوِّقْنِی طَوْقَ الْإِقْلَاعِ عَمَّا یحْبِطُ الْحَسَنَاتِ، وَ یذْهَبُ بِالْبَرَكَاتِ (۱۰۷) وَ أَشْعِرْ قَلْبِی الِازْدِجَارَ عَنْ قَبَائِحِ السَّیئَاتِ، وَ فَوَاضِحِ الْحَوْبَاتِ. (۱۰۸) وَ لَا تَشْغَلْنِی بِمَا لَا أُدْرِكُهُ إِلَّا بِكَ عَمَّا لَا یرْضِیكَ عَنِّی غَیرُهُ (۱۰۹) وَ انْزِعْ مِنْ قَلْبِی حُبَّ دُنْیا دَنِیةٍ تَنْهَی عَمَّا عِنْدَكَ، وَ تَصُدُّ عَنِ ابْتِغَاءِ الْوَسِیلَةِ إِلَیكَ، وَ تُذْهِلُ عَنِ التَّقَرُّبِ مِنْكَ. (۱۱۰) وَ زَینْ لِی التَّفَرُّدَ بِمُنَاجَاتِكَ بِاللیلِ وَ النَّهَارِ (۱۱۱) وَ هَبْ لِی عِصْمَةً تُدْنِینِی مِنْ خَشْیتِكَ، وَ تَقْطَعُنِی عَنْ رُكُوبِ مَحَارِمِكَ، وَ تَفُكَّنِی مِنْ أَسْرِ الْعَظَائِمِ. (۱۱۲) وَ هَبْ لِی التَّطْهِیرَ مِنْ دَنَسِ الْعِصْیانِ، وَ أَذْهِبْ عَنِّی دَرَنَ الْخَطَایا، وَ سَرْبِلْنِی بِسِرْبَالِ عَافِیتِكَ، وَ رَدِّنِی رِدَاءَ مُعَافَاتِكَ، وَ جَلِّلْنِی سَوَابِغَ نَعْمَائِكَ، وَ ظَاهِرْ لَدَی فَضْلَكَ وَ طَوْلَكَ‏ (۱۱۳) وَ أَیدْنِی بِتَوْفِیقِكَ وَ تَسْدِیدِكَ، وَ أَعِنِّی عَلَی صَالِحِ النِّیةِ، وَ مَرْضِی الْقَوْلِ، وَ مُسْتَحْسَنِ الْعَمَلِ، وَ لَا تَكِلْنِی إِلَی حَوْلِی وَ قُوَّتِی دُونَ حَوْلِكَ وَ قُوَّتِكَ. (۱۱۴) وَ لَا تُخْزِنِی یوْمَ تَبْعَثُنِی لِلِقَائِكَ، وَ لَا تَفْضَحْنِی بَینَ یدَی أَوْلِیائِكَ، وَ لَا تُنْسِنِی ذِكْرَكَ، وَ لَا تُذْهِبْ عَنِّی شُكْرَكَ، بَلْ أَلْزِمْنِیهِ فِی أَحْوَالِ السَّهْوِ عِنْدَ غَفَلَاتِ الْجَاهِلِینَ لِآلْائِكَ، وَ أَوْزِعْنِی أَنْ أُثْنِی بِمَا أَوْلَیتَنِیهِ، وَ أَعْتَرِفَ بِمَا أَسْدَیتَهُ إِلَی. (۱۱۵) وَ اجْعَلْ رَغْبَتِی إِلَیكَ فَوْقَ رَغْبَةِ الرَّاغِبِینَ، وَ حَمْدِی إِیاكَ فَوْقَ حَمْدِ الْحَامِدِینَ (۱۱۶) وَ لَا تَخْذُلْنِی عِنْدَ فَاقَتِی إِلَیكَ، وَ لَا تُهْلِكْنِی بِمَا. أَسْدَیتُهُ إِلَیكَ، وَ لَا تَجْبَهْنِی بِمَا جَبَهْتَ بِهِ الْمُعَانِدِینَ لَكَ، فَإِنِّی لَكَ مُسَلِّمٌ، أَعْلَمُ أَنَّ الْحُجَّةَ لَكَ، وَ أَنَّكَ أَوْلَی بِالْفَضْلِ، وَ أَعْوَدُ بِالْإِحْسَانِ، وَ أَهْلُ التَّقْوی‏، وَ أَهْلُ الْمَغْفِرَةِ، وَ أَنَّكَ بِأَنْ تَعْفُوَ أَوْلَی مِنْكَ بِأَنْ تُعَاقِبَ، وَ أَنَّكَ بِأَنْ تَسْتُرَ أَقْرَبُ مِنْكَ إِلَی أَنْ تَشْهَرَ. (۱۱۷) فَأَحْینِی حَیاةً طَیبَةً تَنْتَظِمُ بِمَا أُرِیدُ، وَ تَبْلُغُ مَا أُحِبُّ مِنْ حَیثُ لَا آتِی مَا تَكْرَهُ، وَ لَا أَرْتَكِبُ مَا نَهَیتَ عَنْهُ، وَ أَمِتْنِی مِیتَةَ مَنْ یسْعَی نُورُهُ بَینَ یدَیهِ وَ عَنْ یمِینِهِ. (۱۱۸) وَ ذَلِّلْنِی بَینَ یدَیكَ، وَ أَعِزَّنِی عِنْدَ خَلْقِكَ، وَ ضَعْنِی إِذَا خَلَوْتُ بِكَ، وَ ارْفَعْنِی بَینَ عِبَادِكَ، وَ أَغْنِنِی عَمَّنْ هُوَ غَنِی عَنِّی، وَ زِدْنِی إِلَیكَ فَاقَةً وَ فَقْراً. (۱۱۹) وَ أَعِذْنِی مِنْ شَمَاتَةِ الْأَعْدَاءِ، وَ مِنْ حُلُولِ الْبَلَاءِ، وَ مِنَ الذُّلِّ وَ الْعَنَاءِ، تَغَمَّدْنِی فِیمَا اطَّلَعْتَ عَلَیهِ مِنِّی بِمَا یتَغَمَّدُ بِهِ الْقَادِرُ عَلَی الْبَطْشِ لَوْ لَا حِلْمُهُ، وَ الْآخِذُ عَلَی الْجَرِیرَةِ لَوْ لَا أَنَاتُهُ (۱۲۰) وَ إِذَا أَرَدْتَ بِقَوْمٍ فِتْنَةً أَوْ سُوءاً فَنَجِّنِی مِنْهَا لِوَاذاً بِكَ، وَ إِذْ لَمْ تُقِمْنِی مَقَامَ فَضِیحَةٍ فِی دُنْیاكَ فَلَا تُقِمْنِی مِثْلَهُ فِی آخِرَتِكَ‏ (۱۲۱) وَ اشْفَعْ لِی أَوَائِلَ مِنَنِكَ بِأَوَاخِرِهَا، وَ قَدِیمَ فَوَائِدِكَ بِحَوَادِثِهَا، وَ لَا تَمْدُدْ لِی مَدّاً یقْسُو مَعَهُ قَلْبِی، وَ لَا تَقْرَعْنِی قَارِعَةً یذْهَبُ لَهَا بَهَائِی، وَ لَا تَسُمْنِی خَسِیسَةً یصْغُرُ لَهَا قَدْرِی وَ لَا نَقِیصَةً یجْهَلُ مِنْ أَجْلِهَا مَكَانِی. (۱۲۲) وَ لَا تَرُعْنِی رَوْعَةً أُبْلِسُ بِهَا، وَ لَا خِیفَةً أُوجِسُ دُونَهَا، اجْعَلْ هَیبَتِی فِی وَعِیدِكَ، وَ حَذَرِی مِنْ إِعْذَارِكَ وَ إِنْذَارِكَ، وَ رَهْبَتِی عِنْد تِلَاوَةِ آیاتِكَ. (۱۲۳) وَ اعْمُرْ لَیلِی بِإِیقَاظِی فِیهِ لِعِبَادَتِكَ، وَ تَفَرُّدِی بِالتَّهَجُّدِ لَكَ، وَ تَجَرُّدِی بِسُكُونِی إِلَیكَ، وَ إِنْزَالِ حَوَائِجِی بِكَ، وَ مُنَازَلَتِی إِیاكَ فِی فَكَاكِ رَقَبَتِی مِنْ نَارِكَ، وَ إِجَارَتِی مِمَّا فِیهِ أَهْلُهَا مِنْ عَذَابِكَ. (۱۲۴) وَ لَا تَذَرْنِی فِی طُغْیانِی عَامِهاً، وَ لَا فِی غَمْرَتِی سَاهِیاً حَتَّی حِینٍ، وَ لَا تَجْعَلْنِی عِظَةً لِمَنِ اتَّعَظَ، وَ لَا نَكَالًا لِمَنِ اعْتَبَرَ، وَ لَا فِتْنَةً لِمَنْ نَظَرَ، وَ لَا تَمْكُرْ بِی فِیمَنْ تَمْكُرُ بِهِ، وَ لَا تَسْتَبْدِلْ بِی غَیرِی، وَ لَا تُغَیرْ لِی اسْماً، وَ لَا تُبَدِّلْ لِی جِسْماً، وَ لَا تَتَّخِذْنِی هُزُواً لِخَلْقِكَ، وَ لَا سُخْرِیاً لَكَ، وَ لَا تَبَعاً إِلَّا لِمَرْضَاتِكَ، وَ لَا مُمْتَهَناً إِلَّا بِالانْتِقَامِ لَكَ. (۱۲۵) وَ أَوْجِدْنِی بَرْدَ عَفْوِكَ، وَ حَلَاوَةَ رَحْمَتِكَ وَ رَوْحِكَ وَ رَیحَانِكَ، وَ جَنَّةِ نَعِیمِكَ، وَ أَذِقْنِی طَعْمَ الْفَرَاغِ لِمَا تُحِبُّ بِسَعَةٍ مِنْ سَعَتِكَ، وَ الِاجْتِهَادِ فِیمَا یزْلِفُ لَدَیكَ وَ عِنْدَكَ، وَ أَتْحِفْنِی بِتُحْفَةٍ مِنْ تُحَفَاتِكَ. (۱۲۶) وَ اجْعَلْ تِجَارَتِی رَابِحَةً، وَ كَرَّتِی غَیرَ خَاسِرَةٍ، وَ أَخِفْنِی مَقَامَكَ، وَ شَوِّقْنِی لِقَاءَكَ، وَ تُبْ عَلَی‏ تَوْبَةً نَصُوحاً لَا تُبْقِ مَعَهَا ذُنُوباً صَغِیرَةً وَ لَا كَبِیرَةً، وَ لَا تَذَرْ مَعَهَا عَلَانِیةً وَ لَا سَرِیرَةً. (۱۲۷) وَ انْزِعِ الْغِلَّ مِنْ صَدْرِی لِلْمُؤْمِنِینَ، وَ اعْطِفْ بِقَلْبِی عَلَی الْخَاشِعِینَ، وَ كُنْ لِی كَمَا تَكُونُ لِلصَّالِحِینَ، وَ حَلِّنِی حِلْیةَ الْمُتَّقِینَ، وَ اجْعَلْ لِی لِسانَ صِدْقٍ‏ فِی الْغَابِرِینَ، وَ ذِكْراً نَامِیاً فِی الْآخِرِینَ، وَ وَافِ بِی عَرْصَةَ الْأَوَّلِینَ. (۱۲۸) وَ تَمِّمْ سُبُوغَ نِعْمَتِكَ، عَلَی، وَ ظَاهِرْ كَرَامَاتِهَا لَدَی، امْلَأْ مِنْ فَوَائِدِكَ یدِی، وَ سُقْ كَرَائِمَ مَوَاهِبِكَ إِلَی، وَ جَاوِرْ بِی الْأَطْیبِینَ مِنْ أَوْلِیائِكَ فِی الْجِنَانِ الَّتِی زَینْتَهَا لِأَصْفِیائِكَ، وَ جَلِّلْنِی شَرَائِفَ نِحَلِكَ فِی الْمَقَامَاتِ الْمُعَدَّةِ لِأَحِبَّائِكَ. (۱۲۹) وَ اجْعَلْ لِی عِنْدَكَ مَقِیلًا آوِی إِلَیهِ مُطْمَئِنّاً، وَ مَثَابَةً أَتَبَوَّؤُهَا، وَ أَقَرُّ عَیناً، وَ لَا تُقَایسْنِی بِعَظِیمَاتِ الْجَرَائِرِ، وَ لَا تُهْلِكْنِی‏ یوْمَ تُبْلَی السَّرائِرُ، وَ أَزِلْ عَنِّی كُلَّ شَكٍّ وَ شُبْهَةٍ، وَ اجْعَلْ لِی فِی الْحَقِّ طَرِیقاً مِنْ كُلِّ رَحْمَةٍ، وَ أَجْزِلْ لِی قِسَمَ الْمَوَاهِبِ مِنْ نَوَالِكَ، وَ وَفِّرْ عَلَی حُظُوظَ الْإِحْسَانِ مِنْ إِفْضَالِكَ. (۱۳۰) وَ اجْعَلْ قَلْبِی وَاثِقاً بِمَا عِنْدَكَ، وَ هَمِّی مُسْتَفْرَغاً لِمَا هُوَ لَكَ، وَ اسْتَعْمِلْنِی بِمَا تَسْتَعْمِلُ بِهِ خَالِصَتَكَ، وَ أَشْرِبْ قَلْبِی عِنْدَ ذُهُولِ الْعُقُولِ طَاعَتَكَ، وَ اجْمَعْ لِی الْغِنَی وَ الْعَفَافَ وَ الدَّعَةَ وَ الْمُعَافَاةَ وَ الصِّحَّةَ وَ السَّعَةَ وَ الطُّمَأْنِینَةَ وَ الْعَافِیةَ. (۱۳۱) وَ لَا تُحْبِطْ حَسَنَاتِی بِمَا یشُوبُهَا مِنْ مَعْصِیتِكَ، وَ لَا خَلَوَاتِی بِمَا یعْرِضُ لِی مِنْ نَزَغَاتِ فِتْنَتِكَ، وَ صُنْ وَجْهِی عَنِ الطَّلَبِ إِلَی أَحَدٍ مِنَ الْعَالَمِینَ، وَ ذُبَّنِی عَنِ الْتِمَاسِ مَا عِنْدَ الْفَاسِقِینَ. (۱۳۲) وَ لَا تَجْعَلْنِی لِلظَّالِمِینَ ظَهِیراً، وَ لَا لَهُمْ عَلَی مَحْوِ كِتَابِكَ یداً وَ نَصِیراً، وَ حُطْنِی مِنْ حَیثُ لَا أَعْلَمُ حِیاطَةً تَقِینِی بِهَا، وَ افْتَحْ لِی أَبْوَابَ تَوْبَتِكَ وَ رَحْمَتِكَ وَ رَأْفَتِكَ وَ رِزْقِكَ الْوَاسِعِ، إِنِّی إِلَیكَ مِنَ الرَّاغِبِینَ، وَ أَتْمِمْ لِی إِنْعَامَكَ، إِنَّكَ خَیرُ الْمُنْعِمِینَ (۱۳۳) وَ اجْعَلْ بَاقِی عُمُرِی فِی الْحَجِّ وَ الْعُمْرَةِ ابْتِغَاءَ وَجْهِكَ، یا رَبَّ الْعَالَمِینَ، وَ صَلَّی اللهُ عَلَی مُحَمَّدٍ وَ آلِهِ الطَّیبِینَ الطَّاهِرِینَ، وَ السَّلَامُ عَلَیهِ وَ عَلَیهِمْ أَبَدَ الْآبِدِینَ.

Maudhui zinazo fungamana

Vyanzo

  • Anṣārīyān, Ḥusayn. Dīyār-i Āshiqān: tafsīr-i jāmiʿ al-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya. Tehran: Payām-i Āzādī, 1373 Sh.
  • Ardshīrī Lājīmī, Nigāhī bi duʿā-yi ʿArafa Imām Sajjād (a). Ishārāt Journal. No 156. Fall 1393 AH.
  • Aʿrābī, Ghulām Ḥusayn. Chirā Imām Sajjād (a) bi mubārizāt-i siyāsī napardākht. Māhnāma Kawthar. No 34.
  • Dārābī, Muḥammad b. Muḥammad. Rīyāḍ al-ʿārifīn fī sharḥ al-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya. Edited by Ḥusayn Dargāhī. Tehran: Nashr-i Uswa, 1379 Sh.
  • Faḍl Allāh, Sayyid Muḥammad Ḥusayn. Āfāq al-rūḥ. Beirut: Dār al-Mālik, 1420 AH.
  • Fayḍ al-Kāshānī, Muḥammad b. al-Murtaḍā al-. Taʿlīqāt ʿalā l-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya. Tehran: Muʾassisat al-Buḥūth wa l-Taḥqīqāt al-Thiqāfīyya, 1407 AH.
  • Fihrī, Sayyid Aḥmad. Sharḥ wa tarjuma-yi Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya. Tehran: Nashr-i Uswa, 1388 Sh.
  • Jazāʾirī, ʿIzz al-Dīn. Sharḥ al-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya. Beirut: Dār al-Taʿāruf li-l-Maṭbūʿāt, 1402 AH.
  • Khalajī, Muḥammad Taqī. Asrār-i khāmūshān. Qom: Partuw Khurshīd, 1383 Sh.
  • Madanī Shīrāzī, Sayyid ʿAlīkhān. Rīyāḍ al-sālikīn fī sharḥ al-Ṣaḥīfa Sayyid al-Sājjidīn. Qom: Muʾassisat al-Nashr al-Islāmī, 1435 AH.
  • Mughnīya, Muḥammad Jawād al-. Fī zilāl al-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya. Qom: Dār al-Kitāb al-Islāmī, 1428 AH.
  • Mamdūḥī Kirmanshāhī, Ḥasan. Shuhūd wa shinākht; tarjuma wa sharḥ Ṣaḥīfa-yi Sajjādīyya. Qom: Būstān-i Kitāb, 1388 SH.