Nenda kwa yaliyomo

Khalilullah (Lakabu)

Kutoka wikishia

Khalilullah (Kiarabu: خلیل‌ الله (لقب)) ni ibara ya Kiarabu iliojengeka kupitia maneno mawili Khalilu na Allah. Katika lugha ya Kiarabu neno Khalilu humaaanisha rafiki kipenzi, na neno Allah lina maana ya Mungu. Kwa hiyo neno Khalilullah lina maana ya “rafiki kipenzi wa Mwenye Ezi Mungu”,[1] nalo ni lakabu maalum ya Nabii Ibrahim (a.s).[2] Imeelezwa ya kwamba; nafasi ya kuwa Khalilullah ni nafasi na sifa kubwa mno, na ni makhususi kwa Nabii Ibrahim (a.s),[3] ambayo ni nafasi ya juu zaidi kuliko hata nafasi ya unabii na utume.[4] Katika moja ya Hadithi kutoka kwa Imam Swadiq (a.s), imeelezwa kuwa; kwanza kabisa Mwenyezi Mungu alimchagua Ibrahim kama mja (abd) wake, kisha kama nabii, baadae kama mtume, na hatimaye kama rafiki (khalil).[5]

Aya ya 125 ya Suratu An-Nisa inasema: «واتَّخَذَ اللَّهُ إِبْراهیمَ خَلیلاً» Na Allah alimchagua Ibrahim kuwa ni rafiki yake (kipenzi)".[6] Neno «واتَّخَذَ» wattakadha" limetafsiriwa kwa maana ya kuchagua au kuteua.[7] Mwanzoni mwa aya hii, Mwenye Ezi Mungu amewataka watu kufuata dini ya Ibrahim,[8] kisha ili kuwashawishi wengine kumfuata Ibrahim, Aya hii mwishoni mwake inamalizi kwa kusema; Na Mwenye Ezi Mungu alimchagua Ibrahim kama rafiki kipenzi.[9] Zamakhshari, mwanazuoni na mfasiri wa Kisunni, amelifasiri neno rafiki kama ni fumbo linalomaanisha kuchaguliwa pamoja na kule Ibrahim kuwa na sifa maalum zipatikanazo kati ya marafiki wawili.[10]

Pia Hadithi zimemtaja Ibrahim kama ni Khalilullah.[11] Hata Nabii Ibrahim (a.s) naye pia alijitaja kama Khalilullah.[12] Waislamu wa mji wa Al-Khalil ulioko Palestina iliyokaliwa kimabavu, ambayo ndio nchi aliyokuwa akiishi Ibrahim (a.s),[13] waliuita mji huo kwa jina la Al-Khalil, jina ambalo limetokana na Aya ya 125 ya Suratu An-Nisa.[14] Ingawa lakabu hii imekuwa ni sifa maalum kwa Nabii Ibrahim, ila pia kuna baadhi ya Hadithi na dua zilizotumia wasifu huo katika kumsifu bwana Mtume (s.a.w.w),[15] Imam Ali (a.s) pamoja[16] na Imamu Hussein (a.s) [17].

Pia katika fasihi ya Kiajemi, Nabii Ibrahim (a.s) anajulikana kama ni Khalil. Mulla Ahmad Naraqi katika Mathnawi Ta'qdis aliandika:

Allah Mwingi wa Utukufu alimteua na kumuita kuwa Khalil wake.
Hadhi ya urafiki ilimfikia kutoka kwa Mola, na hivyo akapewa lakabu ya Khalilullah.[17]

Mshairi mwingine aliandika akisema:

Msingi wa Nyumba ya Kaaba uliwekwa na Khalilullah (Ibrahim),
Lakini Ali alizaliwa ndani ya Kaaba, na mwenye nyumba akawa amejitokeza.[18]

Hadithi zimeelezea sababu mbalimbali zilizo mfanya Mwenye Ezi Mungu amchague Ibrahim na kumweka kwenye nafasi hii.[19] Katika kitabu cha Al-‘Ilalu Al-Sharaa’i'i, kuna sehemu yenye kichwa cha habari kisemacho Sababu zilizomfanya Mwenye Ezi Mungu amchague Ibrahim kuwa ni rafiki yake kipenzi.[20] Kuna Hadithi nyingi zilizotajwa juu ya Nabii Ibrahim (a.s) katika sehemu hiyo.[21] Kwa mujibu wa Hadithi, nafasi ya Khalilullah kwa Ibrahim inatokana na kusujudu sana, kuwapa chakula wahitaji, kusali usiku, kutowakataa masikini, ukarimu kwa wageni,[22] na kutoomba chochote kutoka kwa yeyote yule isipokuwa kutoka kwa Mwenye Ezi Mungu mwenyewe.[23] Wafasiri wengine wamesema; kuacha kuabudu sanamu na kumwabudu Mungu ndio msingi wa yeye kupata sifa hiyo.[24]

Maana ya Khalil

Kuna maana mbili zinazoweza kupatikana kuhusiana na neno Khalil: Khalil kwa maana ya rafiki kipenzi; Kiasilia neno Khalil linatokana na al-khullah lenye maana ya rafiki.[25] Maana hii inapatika katika tafsiri ya Tafsiri ya Majma'u al-Bayan ambayo ni tafsiri ya Kishia iliyoandikwa katika karne ya sita.[26] Mfasiri wa Kishia, aitwaye Makarem Shirazi, pia ameihisabu maana kuhusiana na Nabii Ibrahim hii kuwa ni sahihi.[27] Wafasiri wengine pia wanakubaliana na maana hii.[28]

Khalil kwa maana ya umaskini; Pia yawezekana kuwa neno Khalil linatokana na neno al-khallah lenye maana ya umaskini.[29] Baadhi pia wanaamini kuwa; Neno Khalil kwa Nabii Ibrahim lina maana ya kuwa maskini na mwenye uhitaji mbele ya Mungu.[30] Allama Tabatabai anaamini kuwa jina Khalil lina maana ya umaskini, hii ni kwa mujibu wa Hadithi isemayo kuwa; Ibrahimu aliitwa Khalil kwa sababu ya kutoomba chochote kutoka kwa yeyote yule isipokuwa Mungu pekee. Kwa maoni yake, maana sahihi ya Khalilullah ni kule mtu kutomlalamikia yeyote yule kuhusiana na mahitaji yake isipokuwa Mwenye Ezi Mungu peke yake na kuto omba msaada kutoka kwa mtu yeyote yule isipokuwa Mungu peke yake.[31]

Rejea

  1. Makarim Shirazi, Tafsir Nemune, 1374 S, juz. 4, uk. 145.
  2. Mughniyah, Tafsir al-Kashif, 1424 AH, juz. 2, uk. 448.
  3. Abu al-Futuh Razi, Rawdh al-Jinan, 1408 AH, juz. 6, uk. 129.
  4. Mughniyah, Tafsir al-Kashif, 1424 AH, juz. 2, uk. 448.
  5. Kulayni, al-Kafi, 1407 AH, juz. 1, uk. 175.
  6. Surat an-Nisa, Aya ya 125.
  7. Kashani, Zubdat al-Tafsir, 1423 AH, juz. 2, uk. 160.
  8. Husseini Shirazi, Tabi’in al-Qur'an, 1423 AH, uk. 109.
  9. Ibn Kathir Damascus, Tafsir al-Qur'an al-Adhim, 1419 AH, juz. 2, uk. 374.
  10. Zamakhshari, al-Kashaf, 1407 AH, juz. 1, uk. 569.
  11. Kulani, Al-Kafi, 1407 AH, juz. 1, uk. 473.
  12. Kulani, Al-Kafi, 1407 AH, juz. 4, uk. 205.
  13. Lahuti, «Al-Khalil», uk. 91.
  14. Lahuti, «Al-Khalil», uk. 92.
  15. Sheikh Saduq, «Man la Yadharah al-Faqih», 1413 AH, juz. 2, uk. 573.
  16. Ibn Qulawiyyah, Kamil al-Ziyarat, 1356 AH, al-Nas, uk. 44.
  17. Naraqi, Mathnawi Taqdis, Kipengele cha 135, «Subbuh Quddus Rabbi al-Malaikat wa al-Ruh», Tovuti ya Gonjur.
  18. Sighir Isfahan, Divan Ash'ar, Guftan Jibrail wa Bihush Shudan Ibrahim Khalil «Tahaniyyat Idi Maulud Mas;ud Amir al-Muuminin (a.s)»
  19. Makarim Shirazi, Tafsir Nemune, 1374 S, juz. 4, uk. 146.
  20. Sheikh Saduq, Ilal al-Shara’i, 1385 S, juz. 1, uk. 34.
  21. Sheikh Saduq, Ilal al-Shara’i, 1385 S, juz. 1, uk. 34-37.
  22. Qara'ati, Tafsir al-Nur, 1383 S, juz. 2, uk. 395.
  23. Tabataba’i, Al-Mizan, 1417 AH, juz. 5, uk. 96.
  24. Madrasa’i, Min Huda al-Quran, 1419 AH, juz. 2, uk. 201.
  25. Sheikh Tusi, Al-Tabyan, Beirut, juz. 3, uk. 340.
  26. Tabarsi, Majma’ al-Bayan, 1372 AH, juz. 3, uk. 178.
  27. Makarim Shirazi, Tafsir Nemune, 1374 AH, juz. 4, uk. 145.
  28. Taliqani, Partawi Az Qur’an, 1362 AH, juz. 6, uk. 195; Tayyib, Atib al-Bayan, 1378 AH, juz. 4, uk. 221.
  29. Sheikh Tusi, Al-Tabyan, Beirut, juz. 3, uk. 340.
  30. Najafi Khomeini, Tafsir A'san, 1398 AH, juz. 6, uk. 253.
  31. Tabataba’i, Al-Mizan, 1417 AH, juz. 5, uk. 96.

Vyanzo

  • Abū l-Futūḥ al-Rāzī, Ḥusayn b. ʿAlī. Rawḍ al-Jinān wa Rawḥ al-Janān fī Tafsīr al-Qurʾān. Edited by Muḥammad Jaʿfar Yāḥiqī and Muḥammad Mahdī Naṣiḥ . Mashhad: Āstān-i Quds-i Raḍawī, 1408 AH.
  • Ḥusaynī Shīrāzī, Sayyid Muḥammad. Tabyīn al-Qurʾān. Beirut: Dar al-'Ulum, 1423 AH.
  • Ibn Kathīr, Ismāʿīl b. ʿUmar. Tafsīr al-Qurʾān al-ʿaẓīm. Edited by Muḥammad Ḥusayn Shams al-Dīn. Beirut: Dār al-Kutub al-ʿIlmīyya, 1419 AH.
  • Ibn Qūlawayh, Jaʿfar b. Muḥammad. Kāmil al-zīyārāt. Edited by ʿAbd al-Ḥusayn Amīnī. Najaf: Dār al-Murtaḍawīyya, 1356 Sh.
  • Kāshānī, Mullā Fatḥ Allāh. Zubdat al-tafāsīr. Qom: Bunyād-i Maʿārif-i Islāmī, 1423 AH.
  • Kulaynī, Muḥammad b. Yaʿqūb al-. Al-Kāfī. Edited by ʿAlī Akbar Ghaffārī & Muḥammad Ākhūndī. Tehran: Dār al-Kutub al-Islāmīyya, 1407 AH.
  • Lāhūtī, Bihzād. Al-Khalīl. In Dānishnāmah-yi Jahān Islām. Tehran: Bunyād-i Dāʾirat al-Maʿārif-i Islāmī, 1390 Sh.
  • Makārim Shīrāzī, Nāṣir. Tafsīr-i nimūna. Tehran: Dār al-Kutub al-Islāmiyya, 1374 Sh.
  • Mudarrisī, Sayyid Muḥammad Taqī. Min huday al-Qurʾān. Tehran: Dār Muḥibbī al-Ḥusayn, 1419 AH.
  • Mughnīya, Muḥammad Jawād al-. Tafsīr al-Kāshif, Qom: Dār al-Kutub al-Islāmiyya, 1424 AH.
  • Najafī Khomeinī, Muḥammad Jawād. Tafsīr-i āsān. Tehran: Intishārāt-i Islāmiyya, 1398 AH.
  • Qirāʾatī, Muḥsin. Tafsīr-i nūr. Tehran: Markaz-i Farhangī-yi Dars-hā-yi az Qurʾān, 1388 Sh.
  • Ṣadūq, Muḥammad b. ʿAlī al-. ʿIlal al-sharāʾiʿ. Qom: Intishārāt-i Dāwarī, 1385 Sh.
  • Ṣadūq, Muḥammad b. ʿAlī al-. Man lā yaḥḍuruh al-faqīh. Edited by ʿAlī Akbar Ghaffārī. Qom: Intishārāt-i Islāmī, 1413 AH.
  • Ṭabāṭabāʾī, Sayyid Muḥammad Ḥusayn al-. Al-Mīzān fī tafsīr al-Qurʾān. Qom: Daftar-i Intishārāt-i Islāmī, 1417 AH.
  • Ṭabrisī, Faḍl b. al-Ḥasan al-. Majmaʿ al-bayān fī tafsīr al-Qurʾān. Tehran: Naṣir Khusruw, 1372 Sh.
  • Ṭaliqānī, Maḥmūd. Partuwī az Qurʾān. 4th edition. Tehran: Shirkat-i Sahāmī-yi Intishār, 1362 Sh.
  • Ṭayyib, ʿAbd al-Ḥusayn. Aṭyab al-bayān fī tafsīr al-Qurʾān. 2nd ed. Tehran: Intishārāt-i Islām, 1378 Sh.
  • Ṭūsī, Muḥammad b. al-Ḥasan al-. Al-Tibyān fī tafsīr al-Qurʾān. Edited by Aḥmad Qaṣīr al-ʿĀmilī. Beirut: Dār Iḥyāʾ al-Turāth al-ʿArabī, [n.d].
  • Ṭūsī, Muḥammad b. al-Ḥasan al-. Tahdhīb al-aḥkām. Tehran: Dār al-Kutub al-Islāmīyya, 1407 AH.
  • Zamakhsharī, Maḥmūd b. ʿUmar al-. Tafsīr al-kashshāf. Beirut: Dār al-Kutub al-ʿArabī, 1407 AH.