Kadhim (Lakabu)

Kutoka wikishia
Makala hii inahusu jina la Imam Kadhimu (a.s.). Ili kujifunza kuhusu shkhsia ya Imam (a.s.), tazama utangulizi wa Imamu Kazim (a.s.).

Makala hii inahusiana na utafiti juu ya jina la Imam Kadhimu (a.s). Ili kuelewa uhalisia na ujhakika wa Imam Kadhim (a.s), rejea utangulizi juu ya Imamu Kadhim (a.s) Jina Kadhim ni mojawapo ya majina mashuhuri ya Imam Musa bin Ja'afar (a.s). [1] Imeelezwa katika vitabu vya maadili (akhlaq) ya kwamba; jina Kadhim limaana ya mtu anayedhibiti hasira zake. Imam Musa bin Jafar (a.s) alikuwa ni mpole, mvumilivu, na mwenye kudhibiti hasira zake, pia katu hakujionyesha kwa alichokijua. [3] Sabti bin Jauz (aliyefariki mwaka 654 Hijiria) katika kitabu chake kiitwacho Tadhkiratul Al-Khawas ameeleza ya kwamba: “Imam Musa Al-Kadhimu (a.s) alikuwa ni mvumilivu mwenye kusamehe, na hiyo ndiyo sababu hasa ya yeye kuitwa Kadhim kwa ajili hiyo, kwamba kila jambo linapomjia kutoka kwa mtu fulani. atamtumia pesa”. [4] Sayyid Hashim maarufu Al-Hasani, katika kitabu "Siratul A-immatul Ithna'ashariyyah" anasema kwamba, kulingana na riwaya ya iliyonukuliwa katika kitabu Tazkira al-Khuwwaas, Imam Kadhim (a.s) alikuwa akiitwa Kadhimu. Alijulikana kwa jina hilo sababu kila alipoona kitu kibaya kutoka kwa mtu fulani, alikuwa akimtumia mali mtu huyo ambazo zingetosheleza mahitaji ya mtu huyo [5]


REJEA

VYANZO

  • Arbali, Ali Ibn Isa, Kashfu al-Ghumma fi Ma’rifati al-umma, Qom, Razi, 1421 AH.
  • Al-Hasani, Sayyid Hashim, Sira al-Aimmah al-Athnai'ashr, Najaf, Al-Maktab Al-Haydariyya, 1382 AH.
  • Sibtu bin Juzi, Yusuf bin Ghazaughli, Tadhkiratu al-Khuwwas minal umma fi dhikr manaqibil al-Aimma, Qom, Manshurat al-Sharif al-Radhi, 1418 AH.
  • Tabarsi, Fadhlu bin Hasan, Al-Alam al-Wori ba'alam al-Hadi, Qom, Taasisi ya Al-Al-Bayt, 1417 AH.
  • Ghazali, Muhammad bin Muhammad, Ihyau Ulum al-Din, Beirut, Daru al-Maarif, Bita.
  • Majlisi, Muhammad Baqir, Bihar Al-Anwar, Tehran, Islamia, 1363.
  • Naraqi, Muhammad Mahdi, Al-Saadat Jami’, Beirut, Al-Alami Institute of Press, BTA.