Eda

Kutoka wikishia

Eda (Kiarabu: العِدَّة) Ni muda au idadi ya masiku na ni kipindi maalumu ambacho mwanamke baada ya talaka au kifo cha mume wake hawezi kuolewa kisheria. Kuna aina mbalimbali za Eda ambazo hutafautiana katika kipindi cha masiku ambayo mwanamke hutakiwa kujizuia na ndoa. Sharti la lazima la katika suala la mwanamke kuwajibikiwa na Eda, ni kutendeka kwa tendo la ndoa, baada kuolewa kwake, isipokuwa Eda ya mwanamke kufiwa na mume wake.

Eda ya talaka ni sawa na mzunguko wa hedhi tatu; ingawa ikiwa mwanamke ni mjamzito, muda wa Eda yake utakuwa ni hadi baada ya kujifungua. Muda wa talaka kwa mwanamke ambaye amefikia umri wa hedhi lakini akawa haoni hedhi, ni miezi mitatu ya Qamaria (ya mwezi mwandamo). Muda wa Eda ya kufiliwa na mume, ni miezi minne na siku kumi, na ikiwa mwanamke ni mjamzito, ima muda Eda yake utakuwa n miezi minne na siku kumi, baada ya kujifungua. Ufafanuzi wake ni kwamba; Iwapo yeye atakuwa kwenye Eda ya miezi mine na siku kumi, kisha akajifungua kabla ya kumalizika kwa Eda hiyo, basi itambidi aitimize Eda hiyo, na kama atakuwa amekaa Eda hiyo na wake (miezi mine na siku kumi) ukawa umamalizika ila akawa bado hajajifungua, basi itambidi aendelee na Eda hiyo hadi ajifungue, na kujifungua kwake ndio kutakuwa hitimisho la Eda hiyo. Muda wa Eda ya ndoa ya muda mfupi (mutaa), ni mzunguko wa hedhi mbili, na ikiwa mwanamke atakuwa na tatizo la kuto ona hedhi, basi Eda yake itakuwa ni siku 45.

Miongoni mwa hukumu za fiqhi zinazo ambatana na Eda, ni kwamba; ni haramu mwanamme kumuoa mwanamke ambaye yuko ndani ya Eda. Ikiwa mwanaume atamuoa mwanamke ambaye yuko ndani ya muhula wa Eda, basi mwanamke huyo atakuwa haramu kwake milele; yaani ndoa yao itakuwa batili na kamwe hawataweza kuoana. Pia, ni haramu kumposa mwanamke ambaye yuko katika kipindi cha Eda ya talaka rejea. Ni haramu pia kujipamba kwa mwanamke aliyeko ndani ya Eda ya kufiliwa na mumewe.

Ufafanuzi na utambulisho wa Kifiqhi

Muda wa Eda ni kipindi maalum ambapo mwanamke baada ya talaka au kifo cha mume wake au baada ya kujamiiana kimakosa na mtu mwingine, anakuwa hana haki ya kuolewa mume mwengine, mpaka kipindi hicho kimalizike. [1]

Aina za 'Iddah

Kuna aina tofauti za Eda kama vile; Eda ya talaka, Eda ya kifo, 'Iddah ya ndoa ya muda (mutaa), Eda ya kujamiiana kimakosa, na Eda ya kupotea na kutoweka kwa mume. Muda wa Eda kwa kila moja kati ya aina hizi kwa kawaida huwa ni tofauti. Kulingana na fat'wa za wanazuoni, katika aina zote za Eda isipokuwa Eda ya kifo, sharti la wajibu linalomfanya mwanamke kukabiliwa na Eda, ni kupita tendo la kujamiiana. [2]

Eda ya talaka

Mwanamke ambaye ameachwa na mumewe kwa njia ya talaka au ametengana na mumewe kutokana na kuvunjwa kwa ndoa, Eda yake huwa ni miezi mitatu, ambayo ni mzunguko wa mitakasiko mitatu (muda wa kuwa safi kutokana na damu ya hedhi). [3] Hukumu hii imethibitishwa katika Aya ya 228 ya Surat al-Baqarah isemayo: ((وَالْمُطَلَّقَاتُ يَتَرَبَّصْنَ بِأَنفُسِهِنَّ ثَلَاثَةَ قُرُوءٍ…; Na wanawake walioachwa wangoje na wajizuie binanfsi yao kwa muda wa miezi mitatu)). [4]

Hata hivyo, kulingana na maoni maarufu miongoni mwa wanazuoni ni kwamb; Eda ya talaka kwa mwanamke mjamzito ni muda wa kujifungua kwake. [5] Hukumu hii ya sheria imeelezwa katika Aya ya 4 ya Surat Talaq isemayo: ((وَ أُوْلَاتُ الْأَحْمَالِ أَجَلُهُنَّ أَن يَضَعْنَ حَمْلَهُن ; Na kwa wajawazito hitimisho la muda wa Eda yao ni kujifungua)).

Wanawake ambao wameshafikia umri wa hedhi lakini wakawa hawana hedhi, wanapaswa kukaa Eda kwa muda wa miezi mitatu ya Qamaria (kulingana na mwezi Mwandamo). [6] Fat'wa hii pia imeelezwa kwenye Aya ya 4 ya Surat Talaq inasemayo: ((وَاللَّائِي يَئِسْنَ مِنَ الْمَحِيضِ مِن نِّسَائِكُمْ إِنِ ارْتَبْتُمْ فَعِدَّتُهُنَّ ثَلَاثَةُ أَشْهُرٍ وَاللَّائِي لَمْ يَحِضْنَ ; Na wale ambao wamekoma hedhi (wameshakatikiwa na hedhi) miongoni mwa wanawake wenu, ikiwa mnashaka (juu ya hali zao za uja uzito), basi Eda yao ni miezi mitatu)). [7]

Eda ya kufiliwa na mume

Kipindi cha Eda ya mwanamke aliye filiwa na mumewe ni miezi minne na siku kumi. [8] Uamuzi huu wa Shari'a umetajwa katika Aya ijulikanayo kwa jina la Aya ya Tarabbus, [9] kiwango cha masiku ya Eda hii ni kiwango sawa katika aina zote mbili za ndoa, yaani ndoa ya kudumu au ndoa ya muda mfupi (mutaa), Eda hii ni wajibu bila ya kujali kwamba kulipita tendo la ndoa baina yao au la. [10]

Yaani iwapo mwanamke atakuwa ameolewa kwa ndoa ya daima au kwa ndoa ya muda, iwapo mume atafariki hali akiwa yupo katinda hiyo, mwanamke huyo atawajibika kukaa Eda ya miezi mine na siku kumi. Kama mwanamke atakuwa ni mjamzito, basi atawajibika kukaa Eda ilio refu zaidi baina ya Eda ya miezi minne na siku 10 na Eda ya kujifungua. [11] Yaani iwapo atafiliwa na mumewe hali akiwa katika masiku ya mwishoni mwa mimba yake, kisha atajifungua kabla ya kutimiza Eda yake ya muda wa miezi minne na siku kumi, basi atawajibika aendelee na Eda yake mpaka atimize miezi mine na siku kumi, kwa hiyo kujifungua kwake hakutahitimisha Eda hiyo. Na iwapo atakuwa amekaa Eda hali akiwa mwanzoni mwa mimba yake, kisha muda wa miezi mine na masiku kumi ukamalizika kabla ya yeye kujifungua, basi pia atatakiwa kubakia katika Eda hiyo hadi ajifungue.

Eda ya ndoa muda maalumu (muta)

Eda ya ndoa ya muda maalumu, huanza baada ya kumalizika kwa kipindi cha mkataba wa ndoa hiyo, kupita msamaha kutoka kwa mume, yaani iwapo mume ataona kuwa hana haja ya kuendelea na ndoa hiyo ila masiku ya mkataba wa ndoa hiyo yakawa hayajamalizika, basi mume anaweza kusamehe masiku yaliobakia na kumfanya mke huyo kuwa huru. Muda wa masiku ya Eda katika ndoa ya muda ni mizungungo miwili ya hedhi, hii ni kwa mwanamke mwenye kupata hedhi katika hali ya kawaida. Ama kwa mwanamke aliye fikia umri wa kuona hedhi na akawa haoni hedhi kutokana na jambo au tatizo fulani, basi Eda yake itakuwa ni siku arubaini na tano. [14]

Ni vyema ieleweke ya kwamba kuna aina nne za wanawake ambao wanawezekana kukabiliwa na masuala ya kindoa kwa sababu tofauti. Aina tatu za wanawake ni:

  1. Mwanamke aliye fikia baleghe na akawa anaona hedhi katika hali ya kawaida.
  2. Mwamke baleghe ambaye ima ni tasa au haoni hedhi kutokana na sababu fulani.
  3. Mwanamke mwenye umri mdogo wa kabla ya kubaleghe (kigori).
  4. Mwanamke mtu mzima ambaye ameshakonga, na hedhi yake imekatika kutokana na uzee wake.

Mwanamke anayekabiliwa na Eda kati ya wanawake hawa ni mwanamke aliyeko katika kundi namba 1 na namba mbili 2. Kwa hiyo kigori na mtumzi aliypindukia zama za kuona hedhi, wao hawana Eda.

Eda ya kujamiiana kimakosa

Kulingana na fat'wa za wanazuoni, ikiwa mwanaume ikiwa atajamiiana na mwanamke kimakosa akifikiria kuwa yeye ni mkewe, mwanamke huyo atalazimika kukaa Eada sawa na Eda ya talaka, yaani kiwango cha mizunguko mitatu ya hedhi (atoharike mara tatu), iwe manamke amefanya tendo hilo kwa kujua au bila kujua. Lakini kuna tofauti za maoni katika hali ya mwanamme kutenda tendo hilo hali akijua kuwa mwanamke huyo si mkewe, huku mwanamke akiwa hajui. Baadhi wanazuoni wanasema kwamba; katika hali kama hii, mwanamke atalazimika kukaa Eda, ila kwa fatwa za kikundi jengine ni kwamba; katika hali hiyo mwanamke huyo hatawabikiwa na Eda. [15]

Eda ya mume aliyepotea au kutoweka

Kwa mujibu wa maoni maarufu, ni kwamba; mwanamke ambaye mumewe amepotea anapewa talaka na mlezi wa mume au hakimu wa kidini, na talaka hiyo ni talaka rejea. [16] Hata hivyo, baadhi ya wanazuoni, kama vile Sheikh Tusi katika kitabu chake al-Khilaf [17] na al-Mabsut, [18] Sheikh Mufid katika al-Muqni'ah, [19] na Ibn Idris al-Hilli katika al-Sara'iru, [20] wanaamini kwamba; hakuna haja ya kutamka ibara na maneno yapitishayo talaka, na kwamba hukumu ya hakimu inatosha katika kukamilika kwa talaka hiyo, na ndiyo sharti ya kuwatenganisha wawili hao.

Wanazuoni wengi mashuhuri wanaamini kwamba; aina ya Eda kiwango cha masiku ya Eda katika kesi hii, ni sawa na Eda ya kufiwa na mume. [21]

Eda ya mwanamke mzinzi

Wanazuoni wanasema kwamba; hakuna Eda kwa mwanamke aliye fanya uzinzi na kupata mimba, ila kuna tofauti ya maoni kuhusu mwanamke mzinzi aliye fanya tendo hilo bila ya kushika mimba. Fat'wa za wengi wao ni kwamba; mwanamke huyo pia hana Eda; lakini baadhi yao wamechukua hadhari katika fatwa zao, kwa hiyo kwa mtazamo wao ni kwamba; yeye anapaswa ya kukaa Eda kwa kiasi cha kuona damu ya hedhi mara moja, yaani Eda yake ni mzunguko wa hedhi moja. [22]

Eda ya kuritadi

Kulingana na fatwa za maulamaa, ni kwamba; ikiwa mmoja wa wanandoa, mwanamke au mwanaume, ataritadi baada ya ndoa, ndoa hiyo inavunjika. [23] Ikiwa mwanamume ni mritadi fitri (aliyezaliwa na wazazi Waislamu kisha baada ya kubaleghe akaritadi), talaka yao itakuwa ya moja kwa moja, na mwanamke lazima akae Eda sawa na Eda ya mwanamke aliye filiwa na mumewe. Lakini ikiwa murtadi huyu atakuwa ni mritadi milliy, basi mwanamke atalazimika kukaa Eda sawa na Eda ya ya talaka. Na ikiwa katika kipindi hicho cha Eda mwanamume atakuwa tena Mwislamu, ndoa yao inaendelea tena. [24]

Lakini ikiwa mwanamke ataritadi, awe ni mritadi fitri au mritadi milliy, ni lazima mwanamke huyo akae Eda ya talaka. [25]

Sheria na hukumu za Eda

Baadhi ya hukumu za kisheria za Eda, kulingana na fat'wa kutoka kwa wanazuoni wenye mamlaka ya kisheria ya kutoa fatwa, ni kama ifuatavyo:

  • Ni haramu Kuoa mwanamke ambaye yuko katika Eda; iwe yuko katika Eda ya ndoa ya kudumu au ya muda (mutaa) au Eda ya kufiliwa na mume.[26]
  • Ikiwa mwanamme atamuoa mwanamke ambaye yuko katika Eda ya talaka rejea na mume wake wa mwanzo, kisha akafanya naye tendo la ndoa, basi mwanamke huyo atakuwa ni haramu kwake milele. hata kama alikuwa hajui hukumu ya kumuoa mwanamke aliyeko katika Eda, au alikuwa hajui kuwa mwanamke huyo yuko katika Eda. [27]
  • Ikiwa mwanamme, atamuoa mwanamke aliyeko katika kipindi cha Eda, na licha ya kujua kuwa ni haramu kumuoa mwanamke aliyeko katika Eda na akifahamu vyema kwamba mwanamke yuko katika 'Iddah, anaoa naye, mwanamke huyo anakuwa haramu kwake milele; hata kama hawajafanya naye tendo la ndoa. [28]
  • Si halali wala haijuzu kumposa mwanamke ambaye yuko katika Eda ya talaka rejea. [29] Lakini hakuna tatizo kumposa mwanamke aliye katika talaka bayyin (talaka isiyokuwa rejea), kwa kupitia njia ya fumbo na ishara isiyo ya wazi kutoka kwa. [30]
  • Mahitaji ya mwanamke ambaye yuko katika Eda ya talaka rejea, yako juu ya shingo ya mumewe; lakini Eda ya talaka ya bayyin, mume atapaswa kutoa mahitaji hayo iwapo tu mwanamke atakuwa ni mjamzito, wakati wa ujauzito. [31]
  • Si halali Kwa mwanamme kumtoa mwanamke ambaye yuko katika Eda ya talaka rejea kutoka katika nyumbani ambayo alikuwa akiishi wakati wa kupewa talaka hiyo. Pia, mwanamke huyo hawezi kutoka nje ya nyumba yake, bila idhini ya mumewe. [32]
  • Ni haramu kwa mwanamke aliyeko katika kipindi cha Eda ya kufiliwa na mume, kufanya kitendo ambacho kinachukuliwa kuwa mapambo, kama vile wanja na kuvaa nguo za mapambo. [33]
  • Kuzini na mwanamke ambaye yuko katika Eda ya talaka rejea hupelekea mwanamke huyo kuwa ni haramu milele kwa mwanamme aliye fanya kitendo hicho. [34]

Wasiowajibikiwa na Eda

Kwa mujibu wa maoni ya fiqhi, baadhi ya wanawake hawahitaji kukaa Eda baada ya kutengana waume wao. Baadhi yao ni wasichana wadogo ambao bado hawajabaleghe na wanawake waliokoma hedhi ambao ni wanawake waliozeeka. [35] Pia, mwanamke ambaye ameachika hali akiwa hajawahi kufanya tendo la ndoa na mumewe, naye pia hawajibikiwi na Eda, isipokuwa kama sababu ya kumalizika kwa ndoa yake itakuwa ni kifo cha mumewe, kwani katika kesi hiyo anapaswa kukaa Eda kifo (Eda ya kifiwa kwa mumewe). [36] Mwanamke mzinifu pia hana Eda ikiwa atakuwa ni mjamzito, na ikiwa si mjamzito, kwa mujibu wa maoni ya wanazuoni wengi, si lazima (wajibu) kuweka kukaa Eda. [37]

Hekima na falsafa ya Eda

Katika baadhi ya vitabu vya Hadithi, tafsiri na fiqhi, ndani yake mmeelezwa sababu za sheria ya Eda katika Uislamu. Katika tafsiri ya "Tafsiri ya al-Amthal", hekima ya Eda ya kifo imeelezwa kuwa; ni heshima kwa mume; kwa hoja ya kwamba ndoa mara tu baada ya kifo cha mume, haiendani na heshima yake na husababisha kutonesha hisia za jamaa zake pia. [38] Pia, hekima juu ya Eda ya talaka, imetajwa kuwa; ni kumpa mume fursa ya kurekebisha na kufikiria zaidi juu ya suala la kutengana. [39]

Kulingana na Hadithi ilioko katika kitabu Ilal al-Sharaai'i, ni kwamba; sababu ya Eda ya kifo kuwa miezi minne na siku kumi, ni kutokana uwezo wa stahamala ya mwanamke, kwani kiwango cha juu cha stahamala ya mwanamke juu ya mahitajio ya tendo la ndoa ni miezi minne; hii ni kwa kuzingatia sheria ya fiqhi, ya kwamba ni wajibu kwa mume kufanya tendo la ndoa na mkewe angalau mara moja kila baada ya miezi minne. [40]

Pia moja ya hekima zilizotajwa kuhusiana na falsafa ya Eda; ni kwa ajili ya kusafisha njia ya uzazi [41] na kuzuia mchanganyiko wa nasaba (kutokuwezekana kutambua baba wa mtoto anayezaliwa. [42]

Sheria na kanuni za uraiani

Hukumu za Eda zimejumuishwa katika Vifungu 1150-1158 vya Kanuni ya Kiraia ya Iran, ambazo zinategemea sheria ya Imamiya. [44] Kulingana na kifungu cha 1150 cha kanuni ya kiraia ya Iran, ni kwamba; Eda ni kipindi maalumu amabacho ndoa huwa imesha katika, ila mwanamke katika kipindi hicho, huwa bado hana haki ya kuolewa na mume mwengine. [45]

Inasemekana kwamba; katika nchi nyengine, ingawa hakuna sharia ya Eda, ila huwa kuna hatua maalumu zinazo chukuliwa, ili kuzuia mchanganyiko wa nasaba, kama vile; kurefusha kesi za talaka na kuzuia wanandoa kuoa tena kwa muda fulani. [46]

Mada zinazo husiana