Kugusa maiti

Kutoka wikishia

Makala hii inahusiana na kugusa maiti. Ili kufahamu kuhusiana na ghusl (josho) angalia makala ya josho la kugusa maiti.


Mass al-Mayyit (Kiarabu: مَسّ المَیِّت) ina maana ya kugusa maiti (mtu aliyefariki) [1] Maudhui ya kugusa maiti huzungumziwa katika mlango wa hukumu za tohara katika vitabu vya Fiq’h.[2]

Hukumu za kugusa maiti

  • Fat'wa ya wanazuoni wa fikihi wa Kishia inasema: kugusa maiti (mwili wa mtu aliyekufa) hupelekea ghusl ya wajibu endapo mwili wa maiti huyo utakuwa umeshapoa. Katika hali hii mtu atalazimika kuoga josho linajulikana kama ghusl ya kugusa maiti.[3]
  • Kugusa mwili wa Maasumu, shahidi katika vita na mtu ambaye kabla ya kutekelezwa adhabu dhidi yake (kutokana na kufanya dhambi fulani) au kufanyiwa kisasi alifanya ghusli ya maiti, haipelekei kuoga josho la kugusa maiti.[4] Hata hivyo baadhi ya wanazuoni wa fikihi wamesema kuwa, huenda kugusa maiti ya shahidi kukapelekea kuwa wajibu ghusl ya kugusa maiti.[5]
  • Kwa mujibu wa mtazamo mashuhuri miongoni mwa wanazuoni wa fikihi ni kwamba, kugusa maiti hakubatilishi udhu. [6] Ingawa baadhi ya mafakihi wanaamini kwamba, kugusa maiti kunabatilisha udhu. [7]
  • Fat'wa ya Marajii taqlidi wengi ni kwamba, kugusa kiungo kilichotengana na mwili wa mwanadamu kama kitakuwa na mfupa hupelekea kuwa wajibu ghusli. [8] Mkabala na wanazuoni hao, Ayatullah Ali Sistani anaamini kwamba, kugusa kiungo kilichotengana na mwili hata kama kitakuwa na mfupa na nyama, hilo halipelekea mtu kutakiwa aoge ghusli ya kugusa maiti.[9]
  • Kwa mujibu wa baadhi ya mafakihi ni kwamba, kuoga josho la kugusa maiti kunahitajika tu kwa ajili ya kufanya mambo ya wajibu ambayo kimsingi yanahitajia kuwa na udhu; kama Swala na kugusa maandishi ya Qur’an. Baadhi wanatambua kitendo cha kugusa maiti kuwa ni hadathi kubwa. Kwa muktadha huo, wanaamini kwamba, ni lazima kuoga ghusl ya kugusa maiti ili kuweza kufanya amali ambazo zinahitajia kuwa na tohara kama Swala, kufanya tawafu na kadhalika.[10]

Rejea

  1. Fadhil al-nakaranii, Risale taudhihul-masail, 1426 Qamarii, kurasa ya 541
  2. Tazama: Tabatabai Yazdi, Al-uruwatul-uthqaa, 1419 Qamarii, juzuu ya 2, kurasa ya 12
  3. Tabatabai Yazdi, Al-uruwatul-uthqaa, 1419 Qamarii, juzuu ya 2,kurasa ya 3; Isfahanii, wasilatu al-najat, 1422 Qamarii, kurasa ya 60
  4. Najafii, Jawahirul-kalam, 1362 Shamsii, juzuu ya 5, kurasa ya 307
  5. Tabrizii Uruwii, Al-tankihu, 1411 Qamarii, juzuu ya 8, kurasa ya 294-298
  6. Tabatabai Yazdi, Al-uruwatul-uthqaa, 1419 Qamarii, juzuu ya 2,kurasa ya 9, Panuviis 5
  7. Tabatabai Yazdi, Al-uruwatul-uthqaa, 1419 Qamarii, juzuu ya 2,kurasa ya 9
  8. Tabatabai Yazdi, Al-uruwatul-uthqaa, 1419 Qamarii, juzuu ya 2,kurasa ya 5
  9. Sistani, Manahij-swalihiin, 1417 Qamarii, juzuu ya 1, kurasa ya 116
  10. Tazama: Tabatabai Yazdi, Al-uruwatul-uthqaa, 1419 Qamarii, juzuu ya 2,kurasa ya 11; Husseini Amulii, Mafatihul-karama, muasasatu nashri al-islam, juzuu ya 4, kurasa ya 314-317

Vyanzo

  • Fadhil Lankaroni, Muhamamd. Risalah Taudhih al-Masail. Qom: Tanpa penerbit, 1426 H.
  • Husaini Amili, Sayid Muhammad Jawad. Miftah al-Karamah fi Syarhi Qawaid al-Allamah. Riset: Muhammad Baqir Khalishi. Qom: Muassasah al-Nasyr al-Islami, tanpa tahun.
  • Isfahani, Sayid Abu al-Hasan. Washilah al-Najah. Qom: Syarh, Sayid Ruhullah Musawi Khomaini. Muassasah Tanzhim wa Nasyre Atstare Imam Khomaini, 1422 H.
  • Najafi, Muhammad Hasan. Jawahir al-Kalam fi Syarhi Syarai' al-Islam. Riset: Abbas Qauchani. Beirut: Dar Ihya' al-Turats al-Arabi, 1362 S.
  • Sistani, Sayid Ali. Minhaj al-Shalihin. Qom: kantor penerbitan Ayatullah Sistani, 1417 H.
  • Tabrizi Gharawi, Mirza Ali. Al-Tanqih fi Syarhi al-Urwah al-Wutsqa taqriran li Bahtsi Ayatillah al-Uzhma al-Sayid Abu al-Qasim al-Khui. Cet. Kedua, 1411 H.
  • Thabathabai Yazdi, Sayid Muhammad Kazhim. Al-Urwah al-Wutsqa. Qom: Muassasah al-Nasyr al-Islami, 1419 H.