Al-Hassan wa Al-Hussein Sayyidaa Shabaabi Ahlu al-Jannah

Kutoka wikishia
Al-Hassan wal-Hussein Sayyidaa Shabaabi Ahlul-Jannah

Al-Hassan wal-Hussein Sayyidaa Shabaabi Ahlul-Jannah (اَلْحَسَنُ واَلْحُسَينُ سَيِّدَا شَبَابِ أَهْلِ الْجَنَّة) ni Hadithi ya bwana Mtume (s.a.w.w) kuhusiana na ubora na hadhi ya Imamu Hassan na Imamu Hussein (a.s) juu ya watu wa Peponi. Baadhi ya wanazuoni wa Kishia, waielewa na kuifasiri dhana ya Hadithi hii kwa maana ya kwamba; Maimamu wawili hawa pia ni bora zaidi kuliko watu wengine waliomo duniani humu na ni wajibu kwa umma kushikamana nao kuwafwata. Kulingana na baadhi ya wanazuoni wa Kisunni, wakizingatia Riwaya zinazosema kuwa watu wa Peponi wote ni vijana, wameifasiri hadithi hii kwa maana ya kwamba; Hassan na Hussein (a.s) ni mabwana wa watu wote wa Peponi; ingawaje ubora wao huo hautaweza kupindukia ubora wa Mtume (s.a.w.w) na Imam Ali (a.s).

Hadithi hii inapatikana katika vyanzo kadhaa, kama vile Amali ya Sheikh Tusi, Man La Yahduruhu al-Faqih, na Sunan at-Tirmidhi. Pia imeripotiwa kutoka kwa watu 25 miongoni mwa Masahaba wa bwana Mtume (s.a.w.w) kama vile Imamu Ali (a.s), Abu Bakar, na Omar bin Khattab. Hidithi imepewa hadhi ya mutawaatir (yenye wingi wa mapokezi kupitia matabaka ya wapokezi tofauti) kutoka kwa wanazuoni wa madhehebu ya pande zote mbili za Sunni na Shia, na wakaihisabu Hadithi hiyo kuwa ni sahihi. Pia kuna Riwaya inayofanana na Hadithi hii kutoka katika baadhi ya vyanzo vya Sunni, ambayo imewatambulisha Abu Bakar na Omar kama vikongwe wa wazee wa Peponi; lakini baadhi ya wataalamu wa Hadithi wa upande wa Kisunni wanaihisabu Hadithi hii kuwa ni Hadithi dhaifu na bandia.

Utambulisho na Hadhi Yake

Hadithi ya Sayyidaa al-Shabab Ahlu al-Jannah: ni Riwaya maarufu kutoka kwa bwana Mtume (s.a.w.w),[1] ambayo imekuwa ikitumiwa kama ni uthibitisho wa ubora wa Imamu Hassan na Imamu Hussein (a.s) juu ya watu wengine wa Peponi.[2] Katika kitabu cha Bihar al-Anwar kuna maelezo yasemayo kuwa; Katika tukio la Karbala, Imamu Hussein (a.s) alitumia hadithi hii kuitetea na kuthibitisha uhalali wake wa kustahiki nafasi ya Ukhalifa mbele ya maadui zake.[3]

Matini na maelezo ya Hadithi hii ni kama ifuatavyo: «اَلْحَسَنُ واَلْحُسَينُ سَيِّدَا شَبَابِ أَهْلِ الْجَنَّة» “Al-Hasan na Al-Hussein ni mabwana wa vijana wa watu wa Peponi”.[4] Pia Hadithi hii inapatikana vyanzo vya Hadithi vya Shia na Sunni kwa ibara nyengine isiokuwa hiyo, kama vile: «الْحَسَنُ وَ الْحُسَینُ سَیدَا شَبَابِ أَهْلِ الْجَنَّةِ وَ أَبُوهُمَا خَیرٌ مِنْهُمَا». Ambayo maana yake ni kwamba; “Al-Hassan na Al-Hussein ni mabwana wa vijana wa watu wa Peponi, na baba yao ni mbora zaidi kuliko wao”.[5] Pia imekuja kwa ibara isemayo;«الْحَسَنَ وَ الْحُسَینَ سَیدَا شَبَابِ أَهْلِ الْجَنَّةِ وَ أَنَّ فَاطِمَةَ سَیدَةُ نِسَاءِ أَهْلِ الْجَنَّة». Yaani “Al-Hassan na Al-Hussein ni mabwana wa vijana wa watu wa Peponi, na Fatima ni mbora wa wanawake wa Peponi.”[6]

Ubora wa Hassan na Hussein Juu ya Watu wa Peponi

Katika baadhi ya Hadithi, imeelezwa ya kwamba; watu wote watakaoingia Peponi, wataingia humo hali wakiwa ni vijana.[7] Baadhi ya wanazuoni wa Kisunni wakitegemea Hadithi kama hizo wameeleza kuwa; neno la “vijana” lililoko katika Hadithi hiyo, ni neno la ziada lenye nia ya kutoa tafsiri na ufafanuzi[8] ya kwamba; Hassan na Hussein (a.s) ndio mabwana wa watu wote wa Peponi.[9] Hata hivyo, Mtume (s.a.w.w) na Imam Ali (a.s) wako nje ya hukumu hiyo kwani wao ni wabora zaidi kuliko Hassan na Hussein (a.s).[10] Katika hadithi nyingine imeelezwa kwamba; Bwana Mtume (s.a.w.w) alimvua Nabii Isa na Yahya katika orodha hiyo.[11] Lakini Muhammad Hassan Madhaffar, mwanazuoni wa Shia, amekataa maneno hayo, na ameona kuwa; kuna uwezekano wa kwamba Haidithi hii imetiwa mkono, na shaka yake ni kwamba; Iweje Nabi Isa na Yahya (a.s) wavuliwe kutoka katika orodha hiyo, hali ya kwamba kuna mitume wenye hadhi na daraja kubwa zaidi kuliko wao, ambao hawakuvuliwa kutoka katika orodha hiyo! Akiwemo Ibrahim na Mussa (a.s), ambao ni bora kuliko Yahya, lakini hawakutajwa katika Hadithi hiyo.[12]

Vielelezo vya Kuthibitishia Uimamu wa Hassan na Hussein (a.s)

Ali Baharani (aliye fariki mwaka 1340 Hijiria) aliye kuwa mwanazuoni wa madhehebu ya Shia, anaamini na kusadiki kuwa; Hadithi inayothibitisha ubwana na utukufu wa Akhera, pia inathibitisha utukufu na ubora katika ulimwengu huu.[13] Hivyo basi yeye anaamini kwamba; kulingana na Hadithi isimayo Hassan na Hussein ni mabwana wa vijana wa Pepono, ni ithibati tosha ya haki ya Uimamu wa Hassan na Husain (a.s) dunianai humu, na kulingana na bora walionao ni lazima watiiwe kama ni viongozi.[14] Kwa kupitia msingi wa hoja hiyo, Hadithi hii inachukuliwa kuwa ni moja ya ushahidi wa Uimamu wa Maimamu hao wawili.[15]

Neno Sayyid ( سَید) lililoko katika ibara ya Hadithi hiyo, kikawaida hutumiwa kwa ajili ya mtu aliye na cheo cha; uongozi, ukubwa, au heshima na hadhi maalumu.[16] Pia mtu bora na mkamilifu aliye kamilika kwa sifa zote njema kuliko wengine, naye huitwa Sayyid.[17]

Hadithi Kuwa na Hadhi ya Mutawatiru

Alamaah Mujlisi, ambaye mtaalamu wa Hadithi wa Shia; akizingatia hali ya mmiminiko wa nukuu juu ya Hadithi ya “Sayyidaa Shababu Ahlu al-Jannah”, ameichukulia Hadithi hiyo kuwa ni miongoni mwa Hadithi mutawatiru mbele ya wanazuoni wa pande zote mbili, Shia pamoja na Sunni.[18] Baadhi ya wanazuoni wa Ahl al-Sunna kama Suyuti na Nasir ad-Din al-Albani pia wamethibitisha “utawatiru” wa Hadithi hii.[19] Abu Nu’aim Isfahani, mtaalamu wa Hadithi wa Ahl as-Sunna, ametoa ishara fulani inayo ashiria uzito na usahihi wa nukuu ya Hadithi hii, akimnukuu Ahmad ibn Hanbal amesema kwamba: Ikiwa Riwaya hii atasomewa mwendawazimu, basi mwendawazimu ataondokewa na wendawazimu wake.[20]

Nukuu mashuhuri za Hadithi zinapatikana kutoka kwa Sheikh Tusi ndani ya kitabu chake cha Amali[21] na kutoka kwa Sheikh Saduq katika kitabu chake cha Man La Yahduruhu al-Faqih.[22] Tirmidhi na Ibnu Abi Shaybah pia ni miongoni mwa wanazuoni wa Ahlu al-Sunna walioinukuu Riwaya hii.[23] Kulingana na baadhi ya watafiti, ni kwamba; Hadithi ya Sayyidaa Shabab Ahl al-Jannah - pamoja na Riwaya zinazofanana nayo - zimeripotiwa na watu 25 miongoni mwa Masahaba wa bwana Mtume (s.a.w.w), ikiwemo Imam Ali (a.s), Abu Bakr, na Omar.[24]

Uwekwaji wa Hadithi Bandia Juu ya Hadhi ya Omar na Abu Bakar Sambamba na Riwaya Hiyo

Katika vyanzo vya Ahl al-Sunnah, kuna ripoti zinazoripoti Hadith zinazo fanana na Hadithi ya “Sayyidaa Shabab Ahl al-Jannah”, Hadithi ambazo zimenukuliwa kuhusiana na hadi ya Omar na Abu Bakar. Ndani ya ripoti ya Hadithi hizo, Omar na Abu Bakar wamesifiwa kuwa wao ni mabwana wa wazee wenye hadhi za kupindia juu ya watu wengine wa Peponi.[25] Mwandishi aitwaye Haythami akiambatana na Ibn Jawzi, ambao ni wanazuoni wa upande wa Ahl al-Sunna, wamezihisabu Riwaya hizo kuwa ni dhaifu na za uongo.[26]

Bwana Tabarsi amenukuu katika kitabu kiitwacho “Al-Ihtijaaj” ya kwamba; katika mjadala kati ya Yahya bin Aktham na Imamu Jawad (a.s), Yahya alimuuliza Imamu kuhusu Hadithi hiyo isemayo kwamba; “Abu Bakar na Omar ni viongozi au ni mambwana wa wazee wa Peponi.” Imamu akimjibu juu ya swali lake; alimwambia kuwa ni jambo geni na lisilowezekana kwamba maneno hayo yawe yametoka kwa bwana Mtume (s.a.w.w), na akasema kamba, Hadithi hiyo ni Hadithi iliyo tungwa na Bani Umayya dhidi ya ile Hadith isemayo kuwa ‘Hassan na Husayn ni mabwana wa watu wa Peponi.[27]

Rejea

  1. Fat-ḥī, Ḥadīth sayyidā shabāb ahlul-janna wa masʾala-yi afḍhalīyyat Imam, uk. 61.
  2. Fat-ḥī, Ḥadīth sayyidā shabāb ahlul-janna wa masʾala-yi afḍhalīyyat Imam, uk. 82.
  3. Majlisī, Biḥār al-anwār, juz. 45, uk. 6.
  4. Ṭūsī, al-Amālī, uk. 312; Ṣadūq, Man lā yaḥḍuruh al-faqīh, juz. 4, uk. 179; Tirmidhī, Sunan al-Tirmidhī, juz. 5, uk. 656; Kūfī, al-Muṣannaf, juz. 6, uk. 378.
  5. Ḥimyarī, Qurb al-isnād, uk. 111; Ibn Māja, Sunan Ibn Māja, juz. 1, uk. 44.
  6. Mufīd, al-Amālī, uk. 23; Aḥmad b. Ḥanbal, Musnad al-Imām Aḥmad, juz. 38, uk. 353, Hadith 2329.
  7. Mufīd, al-Ikhtiṣāṣ, uk. 358; Tirmidhī, Sunan al-Tirmidhī, juz. 4, uk. 679; Majlisī, Biḥār al-anwār, juz. 43, uk. 292.
  8. Munāwī, Fayḍ al-qadīr, juz. 6, uk. 151.
  9. Sindī, Ḥāshiyat al-Sindī ʿalā Sunan Ibn Māja, juz. 1, uk. 57.
  10. Muẓaffar, Dalāʾil al-ṣidq, juz. 6, uk. 463; Fat-ḥī, Ḥadīth sayyidā shabāb ahl al-janna wa masʾala-yi afḍalīyyat-i imam, uk. 59.
  11. Majlisī, Biḥār al-anwār, juz. 43, uk. 316.
  12. Muẓaffar, Dalāʾil al-ṣidq, juz. 6, uk. 461-462.
  13. Ibn Abī l-Ḥadīd, Sharḥ Nahj al-balāgha, 1404 H, juz. 7, uk. 64.
  14. Baḥrānī, Manār al-hudā, 1405 H, uk. 582.
  15. Bāzwand, sanadī wa dilālī-yi ḥādīth-i sayyidā shabāb ahl al-janna», Markaz Haqaiq Islami.
  16. Baḥrānī, Manār al-hudā, uk. 582.
  17. Samʿānī, Tafsīr al-Qurʾān, juz. 1, uk. 316; Baghdādī, Lubāb al-taʾwīl, juz. 2, uk. 242.
  18. Majlisī, Ḥaqq al-yaqīn, uk. 287.
  19. Munāwī, al-Taysīr, juz. 1, uk. 507; Albānī, Silsilat al-aḥādīth al-ṣaḥīḥa, juz. 2, uk. 431.
  20. Iṣfahānī, Tārīkh Iṣfahān, uk. 73.
  21. Ṭūsī, al-Amālī, uk. 312.
  22. Ṣadūq, Man lā yaḥḍuruh al-faqīh, juz. 4, uk. 179.
  23. Tirmidhī, Sunan al-Tirmidhī, juz. 5, uk. 656; Kūfī, al-Muṣannaf, juz. 6, uk. 378, Hadith 32176.
  24. Fat-ḥī, Ḥadīth sayyidā shabāb ahlul-janna wa masʾala-yi afḍhalīyyat-i Imam, uk. 62.
  25. Tirmidhī, Sunan al-Tirmidhī, juz. 5, uk. 611; Aḥmad bin Ḥanbal, Musnad al-Imām Aḥmad, juz. 2, uk. 40, Hadith 602.
  26. Haythamī, Majmaʿ al-zawāʾid, juz. 9, uk. 53; Ibn al-Jawzī, al-Mawḍūʿāt, juz. 1, uk. 398.
  27. Ṭabrasī, al-Iḥtijāj, juz. 2, uk. 447.

Vyanzo

  • Aḥmad b. Ḥanbal, Abū ʿAbd Allāh. Musnad al-Imām Aḥmad b. Ḥanbal. Beirut: Muʾassisat al-Risāla, 1421 AH.
  • Albānī, Muḥammad Nāṣir al-Dīn. Silsilat al-aḥādīth al-ṣaḥīḥa wa shayʾ min fiqhihā wa fawaʾidihā. Riyadh: Maktabat al-Maʿārif li-l-Nashr wa al-Tawzīʿ, 1415 AH.
  • Baghdādī, ʿAlī b. Muḥammad al-. Lubāb al-taʾwīl fī maʿānī al-tanzīl. Beirut: Dar al-kutub al-ʿilmīyya, 1415 AH.
  • Baḥrānī, ʿAlī al-. Manār al-hudā fī l-naṣṣ ʿalā imāmat al-aʾimma al-ithnā ʿashar (a). Edited by ʿAbd al-Zahrāʾ Khaṭīb. Beirut: Dār al-Muntaẓar, 1405 AH.
  • Bāzwand, Riḍā. Bāzkhwānī-yi sanadī wa dilālī-yi ḥādīth-i sayyidā shabāb ahl al-janna. In Markaz-i Ḥaqāʾiq-i Islāmī.
  • Fatḥī, ʿAlī. Ḥadīth sayyidā shabāb ahl al-janna wa masʾala-yi afḍalīyyat-i imam. In Kalām-i Islāmī 21, 82 (1391 Sh).
  • Haythamī, ʿAlī b. Abūbakr. Majmaʿ al-zawāʾid wa manbaʿ al-fawāʾid. Edited by Hisam al-Din Qudsi. Cairo: Maktabat al-Qudsī, 1414 AH.
  • Ḥimyarī, ʿAbd Allāh b. Jaʿfar al-. Qurb al-isnād. Qom: Muʾassisat Āl al-Bayt, 1413 AH.
  • Ibn Abī l-Ḥadīd, ʿAbd al-Ḥamīd b. Hibat Allāh. Sharḥ Nahj al-balāgha. Qom: Maktabat Āyat Allāh al-Marʿashī, 1404 AH.
  • Ibn al-Jawzī, ʿAbd al-Raḥmān b. ʿAlī. Al-Mawḍūʿāt. Edited by ʿAbd al-Raḥmān Muḥammad ʿUthmān. Medina: Al-Maktabat al-Salafīyya, 1386 AH.
  • Ibn Māja, Muḥammad b. Yazīd . Sunan Ibn Māja. Edited by Muḥammad Fuʾād ʿAbd al-Bāqī . [n.p], Dār Iḥyāʾ al-Kutub al-ʿArabīyya, [n.d] .
  • Iṣfahānī, Abū Nuʿaym. Tārīkh Iṣfahān. Edited by Ḥasan Kasrawī. Beirut: Dār al-Kutub al-ʿIlmīyya, 1410 AH.
  • Kūfī, Ibn Abī Shayba al-. Al-Muṣannaf fī l-aḥādīth wa l-āthār. Edited by Kamāl Yūsuf al-Ḥūt. Riyadh: Maktabat al-Rushd, 1409 AH.
  • Majlisī, Muḥammad Bāqir al-. Biḥār al-anwār. Second edition. Beirut: Dār Iḥyāʾ al-Turāth al-ʿArabī, 1403 AH.
  • Majlisī, Muḥammad Bāqir al-. Ḥaqq al-yaqīn. Tehran: Intishārāt-i Islāmīyya, [n.d].
  • Mufīd, Muḥammad b. Muḥammad al-. Al-Ikhtiṣāṣ. Edited by ʿAlī Akbar Ghaffārī and Maḥmūd Muḥarramī Zarandī. Qom: al-Muʾtamar al-ʿĀlamī li-Alfīyat al-Shaykh al-Mufīd, 1413 AH.
  • Mufīd, Muḥammad b. Muḥammad al-. Kitāb al-amālī. Edited by Ḥusayn Ustād Walī and ʿAlī Akbar Ghaffārī. Qom: Kungira-yi Shaykh Mufīd, 1413 AH.
  • Munāwī, Muḥammad ʿAbd al-Raʾūf al-. Al-Taysīr. Riyadh: Maktabat al-Imām al-Shāfiʿī, 1408 AH.
  • Munāwī, Muḥammad ʿAbd al-Raʾūf al-. Fayḍ al-qadīr. Egypt: al-Maktabat al-Tijarīyya al-Kubrā, 1356 AH.
  • Muẓaffar, Muḥammad Ḥasan. Dalāʾil al-ṣidq li-nihaj al-ḥaqq. Qom: Muʾassisat Āl al-Bayt 1422 AH.
  • Ṣadūq, Muḥammad b. ʿAlī al-. Man lā yaḥḍuruh al-faqīh. Edited by ʿAlī Akbar Ghaffārī. Qom: Intishārāt-i Islāmī, 1413 AH.
  • Samʿānī, Manṣūr b. Muḥammad. Tafsīr al-Qurʾān. Edited by Yāsir b. Ibrāhīm. Riyadh: Dār al-Waṭan, 1418 AH.
  • Sindī, Nūr al-Dīn. Ḥāshiyat al-Sindī ʿalā Sunan Ibn Māja. Beirut: Dār al-Jīl, [n.d].
  • Ṭabrisī, Aḥmad b. ʿAlī al-. Al-Iḥtijāj ʿalā ahl al-lijāj. Edited by Muḥammad Bāqir Khirsān. Mashhad: Nashr-i Murtaḍā, 1403 AH.
  • Tirmidhī, Muḥammad ibn ʿĪsā al-. Sunan al-Tirmidhī. Edited by Aḥmad Muḥammad Shākir, Muḥammad fuʾād ʿAbd al-Bāqī and Ibrāhīm ʿUṭwa. Miṣr, Shirkat Maktabat wa Maṭbaʿat Muṣṭafā al-Bābī al-Ḥalabī, 1395 AH.
  • Ṭūsī, Muḥammad b. al-Ḥasan al-. Al-Amālī. Edited by Muʾassisat al-Biʿtha. Qom: Dār al-Thiqāfa li-ṭibaʿat wa al-Nashr wa al-Tawzīʿ, 1414 AH.