Dua ya Arobaini na Moja ya Sahifa Sajjadiyya
Dua ya Arobaini na Moja ya Sahifa Sajjadiyya, (Kiarabu: الدعاء الواحد والأربعون من الصحيفة السجادية) ni mojawapo ya dua zilizonukulia kutoka kwa Imamu Sajjad (a.s). Nayo ni ile dua inayomwomba Mwenye Ezi Mungu stara na ulinzi dhidi ya kutenda dhambi. Katika maombi ya dua hii, Imamu anaomba rehema za Mwenye Ezi Mungu ili asiangamie kwenye la kisasi na adhabu ya Mwenye Ezi Mungu.
Dua ya Arobaini na Moja, imefafanuliwa kwa kina katika tafsiri za Sahifa Sajjadiyya. Miongoni mwa vitabu vilivyofasiri dua hii, ni kitabu kiitwacho Shuhud wa Shinakht (Mwangazo na Utambuzi) kilichoandikwa na Hassan Mamduhi Kermanshahi kwa lugha ya Kiajemi, pamoja na Riyadh al-Salikin ambayo ni kazi ya Sayyid Ali-Khan Madani, ilioandikwa kwa lugha ya Kiarabu.
Mafundisho ya Dua
Dua ya Arobaini na Moja, ni mojawapo ya nyiradi tukufu zilizomo katika kitabu kiitwacho Sahifa Sajjadiyya, na ni ombi maalumu la kumnyenyekea Mwenye Ezi Mungu ili alete stara ya kufunika madhambi na ampe mja wake kinga dhidi ya dhambi na makossa mbali mbali.[1] Kwa mujibu wa ufafanuzi wa Kermanshahi ni kwamba; kuanikwa hadharani kwa makossa ya mwanadamu, katika maisha haya pamoja na huko Akhera, ni moja ya maumivu makubwa yanayomsibu binadamu. Kwa hivyo, Imam Sajjad (a.s), kupitia dua hii, anamtaka Mwenye Ezi Mungu afiche na kustiri dhambi za waja Wake na asiwadhalilishe mbele ya viumbe wengine.[2]
Mafundisho muhimu yanayopatikana katika dua hii ni kama yafuatayo:
- Kuomba heshima na fadhila za Mwenye Ezi Mungu ili mja asikataliwe mbele ya Mola wake.
- Maombi ya kuepushwa na kutumbukia katika uwanja kisasi na adhabu ya Mwenye Ezi Mungu kwa sababu ya dhambi.
- Kuomba stara ya madhambi na kuepushwa na fedheha.
- Maombi ya kuingizwa miongoni mwa waja waliobarikiwa kwa Pepo.
- Madhara ya kufichua siri za watu na athari zake kwa maisha ya mtu binafsi.
- Kukamilika kwa heshima na hadhi ya mwanadabu kupitia radhi na msamaha wa Mwenye Ezi Mungu.
- Kuomba kupata daraja za watu wa daraja tukufu na wenye taqwa.
- Dua ya kuwafakishwa na kuwa miongoni mwa watu wa kulia (As-hab al-Yamin).[3]
Tafsiri Mbali Mbali
Dua ya Arobaini na Moja ya Sahifa Sajjadiyya imetathminiwa na kufasiriwa kwa kina kupitia waandishi mbalimbali. Katika muktadha wa maandiko ya Kifarsi, dua hii imefasiriwa katika vitabu vifuatavyo: Shohood wa Shenaakht: cha Muhammad Hassan Mamdouhi Kermanshahi,[4] Sharhe wa Tarjume Sahifa Sajjadiya, cha Sayyid Ahmad Fahri.[5]
Kwa upande wa lugha ya Kiarabu, ufafanuzi na tafsiri ya dua hii unapatikana katika kazi zifuatazo: Riyadh al-Salikeen: cha Sayyid Ali Khan Madani,[6] Fi Dhilaal al-Sahifa al-Sajjadiyya cha Muhammad Jawad Mughniyeh,[7] Riyadhu al-Arifiin kilichoandikwa na Muhammad bin Muhammad Darabi,[8] Afaaqu al-Rouh cha Sayyid Muhammad Hussein Fadhlullah.[9] Vilevile, istilahi na maneno yaliyotumika katika dua hii yamfasiriwa na kufafanuliwa wa kitaalamu kupitia mfumo wa lugha fasihi, kama inavyoonyeshwa katika: Taliqaatu Ali al-Sahifa al-Sajjadiyya cha Fayz Kashani,[10] Sharhu al-Sahifa al-Sajjadiyya cha Ezzaldin Jazairi.[11]
Tafsiri ya Dua
وَ كَانَ مِنْ دُعَائِهِ عَلَيْهِ السَّلَامُ فِي طَلَبِ السِّتْرِ وَ الْوِقَايَةِ
اللَّهُمَّ صَلِّ عَلَى مُحَمَّدٍ وَ آلِهِ، وَ أَفْرِشْنِي مِهَادَ كَرَامَتِكَ، وَ أَوْرِدْنِي مَشَارِعَ رَحْمَتِكَ، وَ أَحْلِلْنِي بُحْبُوحَةَ جَنَّتِكَ، وَ لَا تَسُمْنِي بِالرَّدِّ عَنْكَ، وَ لَا تَحْرِمْنِي بِالْخَيْبَةِ مِنْكَ.
وَ لَا تُقَاصَّنِي بِمَا اجْتَرَحْتُ وَ لَا تُنَاقِشْنِي بِمَا اكْتَسَبْتُ، وَ لَا تُبْرِزْ مَكْتُومِي، وَ لَا تَكْشِفْ مَسْتُورِي، وَ لَا تَحْمِلْ عَلَى مِيزَانِ الْإِنْصَافِ عَمَلِي، وَ لَا تُعْلِنْ عَلَى عُيُونِ الْمَلَإِ خَبَرِي
أَخْفِ عَنْهُمْ مَا يَكونُ نَشْرُهُ عَلَيَّ عَاراً، وَ اطْوِ عَنْهُمْ مَا يُلْحِقُنِي عِنْدَكَ شَنَاراً
شَرِّفْ دَرَجَتِي بِرِضْوَانِكَ، وَ أَكْمِلْ كَرَامَتِي بِغُفْرَانِكَ، وَ انْظِمْنِي فِي أَصْحَابِ الْيَمِينِ، وَ وَجِّهْنِي فِي مَسَالِكِ الْآمِنِينَ، وَ اجْعَلْنِي فِي فَوْجِ الْفَائِزِينَ، وَ اعْمُرْ بِي مَجَالِسَ الصَّالِحِينَ، آمِينَ رَبَّ الْعَالَمِينَ.
Na mojawapo ya dua zake (a.s), katika kuomba stara na ulinzi kutokana na dhambi, ni kama ifuatavyo:
Ee Mola wangu! Mpe amani (sala) Muhammad na Aali zake, na unitandikie zulia la heshima yako, unifikishe kwenye chemchemi za rehema zako, uniingiza katikati ya pepo yako, usinionjeshe adhabu ya kukataliwa kutoka kwako, wala usininyime kwa njia ya kukosa matumaini kutoka kwako. Ee Mola wangu!
Usinilipe (usiniadhibu na kuniangamiza) kwa dhambi nilizozitenda, wala usinipekue kwa yale niliyoyachuma. Usiyafichue niliyoyaficha rohoni, wala usiyadhihirishe niliyoyasitiri. Usiyapime matendo yangu kwa mizani yako adilifu, wala usizimwage habari zangu hadharani.
Sitiri na usiyaanike hadharani, yale ambayo kuukinitangazia yataniletea fedheha, na yaweke mbali na macho ya wanadamu, yakunje na uyaweke mbali na macho (ya watu) yale yanayonifedhehesha mbele yako.
Vinjari (tukuza) cheo changu kwa ridhaa yako, kamilisha utukufu wangu kwa msamaha wako, niunge kwenye kundi la mkono wa kulia (wenye kustahiki), uniongoze katika njia za waliokoka, nijaalie (niwe) miongoni mwa waliofaulu, yashughulishe (yajenge) maisha yangu na kazi ya kuhudhuria vikao vya watu wema. Amini, Ee Mola wa walimwengu wote!
Rejea
- ↑ Madani Shirazi, Riyadh al-Salihin, 1435 AH, juz. 5, uk. 365.
- ↑ Mamduhi Kermanshahi, Shuhud wa Shenakhti, 1388 S, juz. 3, uk. 297.
- ↑ Mamduhi, Shuhud wa Shenakhti, 1388 S, juz. 3, uk. 297-308.
- ↑ Mamduhi, Kitab Shuhud wa Shenakhti, 1388 S, juz. 3, uk. 295-308.
- ↑ Fahri, Sherh wa Tafsir Sahifa Sajjadiyah, 1388 S, juz. 3, uk. 157-160.
- ↑ Madani Shirazi, Riyadh al-Salihin, 1435 AH, juz. 5, uk. 363-382.
- ↑ Mughniyyah, Fi Dhilal al-Sahifa, 1428 AH, uk. 465-466.
- ↑ Darabi, Riyadh al-Arifin, 1379 S, uk. 493-496.
- ↑ Fadhlullah, Afaq al-Ruh, 1420 AH, juz. 2, uk.312-305.
- ↑ Faidh Kashani, Taaliqat Ala al-Sahaifa al-Sajadiyah, 1407 AH, uk. 77.
- ↑ Jazayiri, Sherh al-Sahifa al-Sajjadiyah, 1402, uk. 202-203.
Vyanzo
- Ansariyan, Ḥusayn. Dīyār-i Āshiqān: tafsīr-i jāmiʿ al-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya, Tehran: Payām-i Āzādī, 1372 Sh.
- Dārābī, Muḥammad bin Muḥammad. Rīyāḍ al-ʿārifīn fī sharḥ al-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya, Tahqiq: Ḥusayn Dargāhī. Tehran: Nashr-i Uswa, 1379 Sh.
- Faḍl Allāh, Sayyid Muḥammad Ḥussein. Āfāq al-rūḥ, Beirut: Dār al-Mālik, 1420 AH.
- Fihrī, Sayyid Aḥmad. Sharḥ wa tarjuma-yi Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya,Tehran: Nashr-i Uswa, 1388 Sh.
- Fayḍ al-Kāshānī, Muḥammad bin al-Murtaḍā al-Taʿlīqāt ʿalā l-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya, Tehran: Muʾassasat al-Buḥūth wa l-Taḥqīqāt al-Thiqāfīyya, 1407 AH.
- Jazāʾirī, ʿIzz al-Dīn, Sharḥ al-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya. Beirut: Dār al-Taʿāruf Lil-Maṭbūʿāt, 1402 AH.
- Madanī Shīrāzī, Sayyid ʿAlīkhān. Rīyāḍ al-sālikīn fī sharḥ al-Ṣaḥīfa Sayyid al-Sājjidīn, Qom: Muʾassisat al-Nashr al-Islāmī, 1435 AH.
- Mamdūḥī Kirmanshāhī, Shuhūd wa shinākht; tarjuma wa sharḥ Ṣaḥīfa-yi Sajjādīyya, Qom: Būstān-i Kitāb, 1388 Sh.
- Mughnīya, Muḥammad Jawād, Fī Dhilāl al-Ṣaḥīfa al-Sajjādīyya, Qom: Dār al-Kitāb al-Islāmī, 1428 AH.