Tahniki kwa mtoto mchanga
Tahniki kwa Mtoto Mchanga (Kiarabu: تحنيك المولود) ni mila maalumu ya Kiislamu inayotekelezwa kwa kuweka kiasi kidogo cha maji au chakula kwenye kinywa cha mtoto mchanga punde tu baada ya kuzaliwa kwake. Kwa mujibu wa mafundisho ya wanazuoni wa Kishia, tahniki inapaswa kufanywa kwa kutumia maji ya Mto Furati pamoja na udongo mtakatifu wa Imamu Hussein (a.s) (udungo wa Karbala), kwa mujibu wa maoni yao, kufanya hivyo ni miongoni mwa amali za mustahabu. Kuna Riwaya kadhaa zinabainisha kwamba; mtu aliyefanyiwa tahniki kwa kupitia maji ya Mto Furati atapata hatima njema ya kuwa mfuasi wa madhehebu ya Kishia na kuwa mpenzi wa Ahlul-Bayt (a.s).
Ufahamu wa Dhana ya Tahniki
Tahniki ni desturi inayohusisha zoezi la upakaji au uwekaji wa kiasi kidogo cha chakula chepesi kwenye kinywa cha mtoto mchanga kiwango ncha ya kidole, kisha kudidimiza kidole hicho kwenye sehemu ya juu ya kinywa cha mtoto huyo.[1] Kawaida, zoezi hili hufanywa na mkunga au mtu mwengine asiyekuwa yeye.[2] Katika tamaduni za jamii mbalimbali, desturi hii inajulikana kwa majina tofauti, ikiwa ni pamoja na; tahniki, kuondoa kinywa,[3] sunna ya kufungua au kupanua kinywa.[4]
Katika muktadha wa imani za kidini na kijamii, zoezi la kufanya tahniki linaaminika kuwa na manufaa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na; kuimarisha afya ya mtoto, kurahisisha unyonyaji au ufyonzaji wa maziwa ya mama, kuzuia matatizo ya kusema (ulimi), kama vile kigugumizi, pamoja na kuweka msingi wa malezi ya kidini katika maisha ya baadae.[5] Kulingana na mafundisho ya wanazuoni wa Fiqhi wa Kishia, yaliofafanuliwa katika fiqhi ya ndoa, tahniki ni amali inayofa nyiwa mtoto mchanga mara tu baada ya kuzaliwa.[6]
Umuhimu wa Tahniki
Katika Wasa’il al-Shi‘a, ambacho ni mojawapo ya vitabu maarufu vya Hadithi za Kishia, kuna sehemu mahususi iliotengwa kwa ajili ya kufafanua umuhimu wa tahniki kwa watoto wachanga, pamoja na hukumu zake za kisharia kuhusiana na zoezi hilo.[7] Pia kuna Hadithi kadhaa zinathibitisha kwamba; mtoto anayefanyiwa tahniki kupitia maji ya Mto Furati atapata hatima ya kuwa Mshia na mwenye mapenzi thabiti kwa Ahlul-Bayt (a.s).[8]
Hata hivyo, zoezi la kuwanyia watoto tahniki, si desturi iliyobuniwa ndani ya Uislamu; bali mila hiyo ilikuwepo miongoni mwa mataifa mbalimbali hata kabla ya kuja kwa Uislamu.[9] Baadhi ya tafsiri za Kisunni katika kufasiri Aya ya 25 ya Surat Maryam, zimeeleza kwamba; desturi ya tahniki kupitia tende ilianzishwa kutokana kule Bibi Maryam kula tende wakati wa kumzaa Nabii Isa (a.s).[10] Katika zama za mwanzoni mwa Uislamu, Masahaba walikuwa na ada ya kumchukua mtoto mchanga na kumpeleka kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) mara tu baada ya kuzaliwa kwake, naye bwana Mtume (s.a.w.w) alikuwa akimpokea mtoto huyo na kumfanyia tahniki kwa kutumia tende, kisha kuhitimisha amali hiyo kwa kumwombea dua.[11] Desturi hii ilipata msisitizo wa kipekee katika enzi za Maimamu wa Kishia, ambapo ilihimizwa kufanya tahniki kupitia maji ya Mto Furati. Baada ya kuuawa kwa Imamu Hussein (a.s), Mashia walisisitizwa kutumia turbah (udongo mtakatifu wa Karbala) katika zoezi hilo la tahniki, jambo ambalo lilisisizwa na kupewa kipau mbele na Maimamu hao.[12]
Katika jamii ya Wairani, desturi hii imeingatiwa kwa kina katika imani na mila zao za kijamii, ikichuwa nafasi maalumu katika uwanja wa fasihi na tamaduni zao.[13] Kuna imani ya jadi isemayo kwamba: tahniki inastahili kufanywa na mtu mwenye uadilifu na nafasi maalumu na inayohimidiwa katika jamii, kwa kuwa inadhaniwa kuwa jambo hilo lina ushawishi wa moja kwa moja katika malezi na mustakabali wa mtoto mchanga.[14]
Adabu na Hukumu za Kifiqhi Kuhusu Tahniki
Kuna Hadithi mbalimbali zinaonyesha jinsi tahniki ilivyotekelezwa na Mtume Muhammad (s.a.w.w) pamoja na Maimamu wa kutoka upande wa Ahlul-Bayt (a.s). Kulingana na moja ya Riwaya kutoka kwa Imamu Ali (a.s), ni kwamba; bwana Mtume (s.a.w.w) alimfanyia tahniki Imamu Hassan (a.s) na Imamu Hussein (a.s) kwa kutumia tende mara tu baada ya kuzaliwa kwao.[15] Vile vile, kuna Hadithi iliyomepokewa kutoka kwa Imamu Musa al-Kadhim (a.s), ya kwamba; Baada ya kuzaliwa kwa Imamu Ridha (a.s), Imamu Musa al-Kadhim (a.s) ndiye aliyemfanyia tahniki mwanawe huyo, kwa kutuia maji ya Mto Furati..[16]
Kulingana na mafundisho mafaqihi wa upande wa madhehebu ya Kishia, tahniki ni sunna inayopendekezwa kufanywa mara tu baada ya kuzaliwa kwa mtoto na kabla ya kumpatia jina rasmi.[17] Sunna hii inastahili zaidi kufanywa kwa maji ya Mto Furati pamoja na turbah ya Imamu Hussein (a.s) (udongo mtakatifu wa Karbala).[18] Iwapo maji ya Furati hayapatikani, basi maji matamu (maji safi) ndiyo yanayopendekezwa kutumika badala yake. Endapo maji yaliyopo yatakuwa ni maji yenye chumvi nyingi, basi inashauriwa yachanganywe na kiasi kidogo cha tende au asali ili kupunguza athari zake.[19]
Pia Katika madhehebu ya Kisunni, tahniki inachukuliwa kuwa ni sunna inayostahili kufanywa mara tu baada ya kuzaliwa kwa mtoto. Ibn Qayyim al-Jawziyya, mmoja wa wanazuoni maarufu wa Kisunni, ameitaja tahniki kama ni moja ya amali zinazopendekezwa wakati wa kuzaliwa kwa mtoto, akizingatia mafundisho ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) pamoja na Masahaba zake katika suala hilo.[20]
Rejea
- ↑ Karimi, Saq Bardoshtane «Saq Bardoshtane», Tovuti ya Markaz Dairat al-Maarif Buzurge Islami.
- ↑ Karimi, Saq Bardoshtane «Saq Bardoshtane», Tovuti ya Markaz Dairat al-Maarif Buzurge Islami.
- ↑ Dahkhuda، Lughatname Dahkhuda, Dhail vizhe «Kam-bordoshtane».
- ↑ Wahidi، «Kam-bardory Nuzad», Tovuti ya Shirika la Habari la Mizan.
- ↑ Karimi, Bardoshtane «Saq Bardoshtane»، Tovuti ya Markaz Dairat al-Maarif Buzurge Islami. ؛ Wahidi, «Kam-bardory Nuzad», Tovuti ya Shirika la Habari la Mizan.
- ↑ Tazama: Muhaqiq Hilli, Sharai' al-Islam, 1408 AH, juz. 2, uk. 287; Bahrani, Al-Hadaiq al-Nadhirah, 1405 AH, juz. 25, uk. 37.
- ↑ Hurr Amili, Wasa'il al-Shi'a, 1409 AH, juz. 21, uk. 407.
- ↑ Ibn Qoluyah, Kamil al-Ziyarat, 1356, uk. 49; Majlisi, Rawdat al-Muttaqeen, 1406 AH, juz. 8, uk. 622.
- ↑ Wahidi، «Kam-bardory Nuzad», Tovuti ya Shirika la Habari la Mizan.
- ↑ Zamakhshari, Kashaf, 1407 AH, juz. 3, uk. 13; Haqi Brusawa, Ruh al-Bayan, Dar al-Fikr, Juz. 5, uk. 327.
- ↑ Subhani, Wahabiyat, 1388 S, juz. 1, uk. 337.
- ↑ Wahidi، «Kam-bardory Nuzad», Tovuti ya Shirika la Habari la Mizan.
- ↑ Tazama: Karimi, Saq Bardoshtane «Saq Bardoshtane», Tovuti ya Markaz Dairat al-Maarif Buzurge Islami.
- ↑ Tazama: Karimi, Saq Bardoshtane «Saq Bardoshtane», Tovuti ya Markaz Dairat al-Maarif Buzurge Islami.
- ↑ Hurr Amili, Wasa'il al-Shi'a, 1409 AH, juz. 21, uk. 407.
- ↑ Hurr Amili, Wasa'il al-Shi'a, 1409 AH, juz. 21, uk. 408.
- ↑ Tazama: Muhaqiq Hilli, Sharai' al-Islam, 1408 AH, juz. 2, uk. 287; Najafi, Jawahir al-Kalam, 1404 AH, juz. 31, uk. 252.
- ↑ Muhaqiq Hilli, Sharai' al-Islam, 1408 AH, juz. 2, uk. 287; Fakhr al-Muhaqiqiin, Idhahu al-Fawaid, 1387 A.H., juz. 3, uk. 258; Allamah Hilli, Qawa'id al-Ahkam, 1413 AH, juz. 3, uk. 97.
- ↑ Muhaqiq Hilli, Sharai' al-Islam, 1408 AH, juz. 2, uk. 287; Fakhr al-Muhaqiqiin, Idhahu al-Fawaid, 1387 A.H., juz. 3, uk. 258
- ↑ Ibn Qayyim Jauziyeh, Tohfa Al-Mawuud Biahkam Al-Mawlud, Maktabat Al-Qur'an, uk. 30.
Vyanzo
- Ibn Quluyeh, Ja'far ibn Muhammad, Kamili Ziyara, Najaf, Dar al-Murtadhaweih, Chapa ya Kwanza, 1356 S.
- Ibn Qayyim Jauziyeh, Muhammad Ibn Abi Bakr, Tohfa Al-Mawuud Biahkam Al-Mawlid, Misr, Maktabat Al-Qur'an, Bita.
- Bahrani, Yusuf, al-Hadaiq al-Nadhirah Fi Ahkam al-Itrah al-Tahirah, Qom, Daftar Intisharat Islami, 1405 AH.
- Hurr Amili, Muhammad ibn Hassan, Wasa’il al-Shi’ah, Qom, Muasase Ahlul-Bayt (a.s), Chapa ya Kwanza, 1409 AH.
- Haqi Brosuwa, Ismail bin Mustafa, Tafsir Ruh al-Bayan, Beirut, Dar al-Fikr, Beta.
- Dahkhoda, Ali Akbar, Lughatname Dahkhoda, Zire Nazar Muhammad Muin wa Sayyid Jafar Shahidi, Tehran, Muasase Intisharat wa Chap Danashghah Tehran, 1377 S.
- Zamakhshari, Mahmoud, Al-Kashaf An Haqaiq Ghawamidh al-Tanzil, Beirut, Dar al-Kitab al-Arabi, Chapa ya Tatu, 1407 AH.
- Allamah Hilli, Hassan bin Yusuf, Qawa'aid al-Ahkam Fi Maarifat al-Halal wa al-Haram, Qom, Daftar Intisharat Islami, 1413 AH.
- Fakhr al-Muhaqqiqin, Muhammad ibn Hassan, Idhahu al-Fawa'aid Fi Sherh Mushkilat al-Qawa'aid, Qom, Muasase Ismaili, Chapa ya Kwanza, 1387 AH.
- Karimi, Asghar, "Saq bardoshtan", Tovuti ya Markaz Dairat al-Maarif Buzurge Islami, Akhir Beruzeresani: 1 Azar 1400, Tarikh Bazdid: 20 Azar 1403.
- Majlisi, Muhammad Taqi, Rawdhat al-Mutaqeen Fi Sharh Man La Yahdhuruh al-Faqih, Qom,Muasase Farhange Islami Kushanbur,Toleo la Pili, 1406 AH.
- Muhaqiq Hilli, Ja'far ibn Hassan, Sharai' al-Islami Fi Masail al-Halal wa al-Haram, Qom, Muasase Ismailiyan,Chapa ya Pili, 1408 AH.
- Najafi, Muhammad Hassan, Jawahir al-Kalam Fi Sherh Sharai' al-Islamiyyah, Beirut, Dar Ihya al-Turat al-Arab, Chapa ya Saba, 1404 AH.