Nenda kwa yaliyomo

Saumu ya kuukaribisha mwezi wa Ramadhani

Kutoka wikishia

Saumu ya kuukaribisha mwezi wa Ramadhani ni zoezi la kufunga siku moja au zaidi kabla ya kuingia kwa mwezi wa Ramadhani.[1] Ingawa istilahi hii haihisabiwi kuwa ni miongoni mwa istilahi zenye nafasi katika vyanzo vya kifiqhi, ila ni istilahi mashuhuri iliozoeleka kijamii na kiutamaduni. Istilahi hii inahusishwa na saumu zinazofungwa katika siku za mwisho za mwezi wa Shaaban kama maandalizi ya kuukaribisha mwezi wa Ramadhani.[2] Kulingana na moja ya Riwaya kutoka kwa Imamu Sadiq (a.s), ni kwamba; Thawabu za kufunga ya siku tatu za mwisho za mwezi wa Shaaban ni sawa na thawabu za kufunga miezi miwili mfululizo.[3] Vile vile, kwa mujibu wa Hadithi ya Imamu Ridha (a.s) ni kwamba; kufunga siku ya mwisho ya Shaaban ni amali inayompelekea mja kupata maghfira ya dhambi kutoka kwa Mola wake.[4] Pia katika vyanzo vya Hadithi vya upande wa madhehebu ya Kisunni, kuna Hadithi zisemazo kwamba; bwana Mtume (s.a.w.w) aliitaja funga ya mwezi wa Shaaban kama moja ya saumu zenye thamani zaidi mingoni mwa funga mbali mbali, na akaeleze kwamba, funga hii ni alama ya kuuheshimu mwezi wa Ramadhani.[5] Kulingana na Hadithi hizo, imethibiti kuwa; hata yeye alikuwa alikuwa na kawaida ya kufunga saumu hiyo ya mwezi wa Shaaban na kuiunganisha moja kwa moja na mwezi wa Ramadhani.[6]

Hata hivyo, wanazuoni wa madhehebu ya Kisunni, kwa kutegemea baadhi ya riwaya, hawaruhusu siku moja au mbili za mwisho wa mwezi wa Shaabani, kwani kwa mtazamo wa Kisunni, ni haramu kufunga siku ya Yaumu Al-Shakk,[7] ila si haramu kwa yule aliyeanza kufungu siku za nyuma yake hadi kumaliza mwezi mzima wa Shaabani. Pia si tatizo kwa yule mwenye kawaida ya kufunga siku moja na kuacha siku ya pili kwa muda wa mwaka mzima,[8] hata kama funga yake itaangukia ndani ya mwezi 28 au 29 Shaabani.[9] Sayyid Ibn Tawus anaamini kwamba; umarufuku huu unawahusu wale waliokamilisha saumu ya Shaabani mzima. Kwa umarufu huu umekuja kuwata wale angalau siku moja au mbili ili wapate nafasi ya kupumzika na kuimarika kimwili kabla ya kuingia mwezi wa Ramadhani.[10]

Makala Zinazo Fungamana

Rejea

  1. Fallah, «Maanaye Be Pishvaz Mahe Ramadhan Rafte Chist?», Tovuti ya Hamid-Ridha Fallah.
  2. Fallah, «Maanaye Be Pishvaz Mahe Ramadhan Rafte Chist?», Tovuti ya Hamid-Ridha Fallah.
  3. Sheikh Saduq, Man La Yahdhuruh al-Faqih, 1413 AH, juz. 2, uk. 49.
  4. Sheikh Saduq, Fadhail al-Ashhur al-Thalatha, 1396 AH, uk. 98.
  5. Ibn Abi Shaybah, Al-Masanif, 1436 AH, juz. 6, uk. 125; Ibn Battal, Sharh Sahih al-Bukhari, 1423 AH, juz. 4, uk. 115.
  6. Ibn Rahuyyah, Musnad Ishaq ibn Rahuyyah, 1412 AH, juz. 4, uk. 150, Ibn Abdul-Barr, Al-Tamhid, 1439 AH, juz. 2, uk. 46.
  7. Ibn Jauzi, Kashf al-Mushkil, Riyadh, juz. 1, uk. 475; Abu Ya'ali, Musnad Abi Ya'ali, 1434 AH, juz. 8, uk. 252.
  8. Saffarini, Kashf al-Littham, 1428 AH, juz. 3, uk. 486.
  9. Ibn Mulqin, al-Tawdhih, 1429 AH, juz. 13, uk. 103.
  10. Ibn Tawus, Iqbal al-Amal, 1409 AH, juz. 1, uk. 9.

Vyanzo

  • Abu Ya'ali, Ahmad bin Ali, Musnad Abi Ya'ali, Taaliqat: Said bin Muhammad Sanari, Cairo, Dar al-Hadith, Chapa ya Kwanza, 1434 AH.
  • Ibn Abi Shaybah, Abdullah bin Muhammad, Al-Musannaf, Tahqiq: Saad bin Nassir, Riyadh, Dar Kunuz Ashbilia Linashr wa Tauzii, Chapa ya Kwanza, 1436 AH.
  • Ibn Battal, Ali ibn Khalaf, Sharh Sahih al-Bukhari, Tahqiq: Abu Tamim Yasir ibn Ibrahim, Riyadh, Maktabat al-Rushd, Chapa ya Pili, 1423 AH.
  • Ibn Jauzi, Abdul-Rahman bin Ali, Kashf al-Mushkil Min Hadith al-Sahihein, Tahqiq: Ali Hussein Al-Bawab, Riyadh, Dar al-Watan, Beta.
  • Ibn Rahuyyah, Ishaq, Musnad Ishaq bin Rahuyyah, Madina, Maktaba'at al-Iman, chapa ya kwanza, 1412 AH.
  • Ibn Tawus, Ali ibn Musa, Iqbal al-Amal, Tehran, Dar al-Kutub al-Islamiyya, chapa ya pili, 1409 AH.
  • Ibn Abdul-Barr, Abu Omar, Al-Tamhid Lma Fi Al-Mu'ta' Min Ma'an Wa'n-Ananid Fi Hadith Rasulullah, Utafiti: Kundi la Watafiti, London, Al-Furqan Foundation for Islamic Heritage, Chapa ya Kwanza, 1439 AH.
  • Ibn Mulqan, Umar Ibn Ali, Al-Tawzih kwa matz ya al-Jame al-Sahih, Tawzih: Dar al-Falah, Damascus, Dar al-Nawader, chapa ya kwanza, 1429 AH.
  • Safarini, Muhammad bin Ahmad, Kashf al-Latham Sharh Umdat al-Ahkam, utafiti: Nur al-Din Talib, Damascus, Dar al-Wadr, chapa ya kwanza, 1428 AH.