Operesheni ya Besharate Fath

Operesheni ya Besharate Fat-h (Kiarabu: عملية بشارة الفتح) (Bishara ya Ushindi) ni operesheni maalumu inayohusiana na shambulio la angani (kupitia makombora) lililofanywa na Vikosi vya Kijeshi la Iran dhidi ya kituo cha kijeshi cha Marekani cha Al Udeid kilichoko nchini Qatar. Tukio hilo la dhahania limewekwa tarehe 2 mwezi wa Tir 1404 Shamsia.[1] Shambulio hili lilifanyioka kama hatua ya kulipiza kisasi kwa shambulio la Marekani dhidi ya miundombinu ya nyuklia ya Iran. Kituo cha Al Udeid kinatambuliwa kama kituo kuu cha Kikosi cha Anga cha Marekani (USAF) katika kanda ya Asia Magharibi.[2] Baadhi ya vyanzo vinaripoti kuwa chombo-anga kisicho na rubani (drone) kilichotumika katika mauaji ya Qassim Suleimani kiliratibiwa kutoka katika kituo hicho.[3] Shambulio hili linawakilisha tukio la pili la aina yake, kufuatia shambulio la awali la mwaka 1398 Shamsia (sawa na mwaka 2020 Miladia), ambapo Kikosi cha Sepah Pasdaran (IRGC) kilikilipua kwa makombora kituo cha Ain al-Asad kilichoko nchini Iraq, kama ni jibu la moja kwa moja katika kujibu na kulipiza kisasi mauaji ya Kamanda wa Kikosi cha Quds, Qassim Suleimani.[4]
Uzinduzi wa Operesheni Besharate Fath, ulifanyika kwa kaulimbiu ya kimkakati isemayo: 'Ya Aba Abdillah al-Hussein (a.s.)' (Ukenja usemao: Ewe Abaa Abdillahi Al-Hussein). Aidha, hii operesheni ilizingatia kanuni ya jibu la kimlingano, ambapo idadi ya makombora yaliyorushwa na Iran, ilikuwa ni sawa na idadi ya mabomu yaliyotumiwa na Marekani dhidi ya miundombinu yake ya nyuklia.[5]
Kufuatia operesheni hiyo, kulizuka ripoti kadhaa zilisambaa kwenye anga za kimtandao (online) kuhusu maandamano ya wananchi nchini Qatar, kupinga uwepo wa kijeshi wa Marekani nchini humo.[6] Pia, baadhi ya uchambuzi unaamini kuwa; operesheni hii ndiyo sababu iliyoilazimisha Israeli kukubali usitishaji wa mapigano kati yake na Iran.[7] Kufuatia operesheni hii, rais wa wakati huo wa Marekani, Trump, alitoa wito rasmi wa kusitishwa kwa mapigano kati ya Iran na Israeli.[8]
Rejea
- ↑ «Tanbih Sheitan; Amaliyat Bisharat Fat-h Alaeih Peygha Amerikayi al-Udeid Qatar», Shirika la Habari la Mehr.
- ↑ «Al-Udeid; Buzurghitarin Peyghah Nidhami Amerika Dar Khavirmiyane; Muhimtarin Markaz Farmandehi Amaliyat Havay Manteqe», Shirika la Habari la Tabnak.
- ↑ «Riwayat Jadid Az Pehpadehaye Ke Sardod Suleiman Ra Ahdaf Girftand», ISNA.
- ↑ «Intiqam Sakhte Ba Shalik Dahehaye Moshak», Shirika la Habari la IRNA.
- ↑ «Tanbih Sheitan; Amaliyat Bisharat Fat-h Alaeih Peygha Amerikayi al-Udeid Qatar», Shirika la Habari la Mehr.
- ↑ Tazama:«Itiradhat Mardum Qatar Be Hudhur Peyghahaye Nidhami Dar Keshvareshun + Film », ILNA.
- ↑ Ateshbas Ba Bisharat Fat-h», Duniyaye Iqtisadi.
- ↑ «Ateshbas Be Dushmane Suh-hyuni, Dar Py Amaliyat Muwafaq Bisharat Fat-h», Shirika la Habari la Mehr.
Vyanzo
- «Tahmil Atesh Bas Be Dushman Suhyuni, Dar Pi Amaliyat Muwafaq Bisharat Fat-h», Shirika la Habari la Mehr, Tarehe ya kuwekwa makala: Julai 3, 1404, Tarehe ya kupitiwa makala: Julai 3, 1404.
- «Tanbih Sheitan; Amaliyat Bisharat Fat-h Alaih Peyghah Amerikayi Al-Udeidah Qatar»، Shirika la Habari la Mehr, Tarehe ya kuwekwa makala: Julai 2, 1404, Tarehe ya kupitiwa makala: Julai 3, 1404.
- «Al-Udeid; Buzurghitarin Peyghah Nidhami Amerika Dar Khavarmane; Muhimtarin Mrkaz Farmandehi Amaliyat Hawayi Manteqe»، Shirika la Habari la Tabnak, Tarehe ya kuwekwa makala: Julai 2, 1404, Tarehe ya kupitiwa makala: Julai 3, 1404.
- «Itiradhi Mrdum Qatar Be Hudhuri Peyghahaye Nidhami Amerika Dar Keshvarshun + Film », ILNA, Tarehe ya kuwekwa makala: Julai 26, 1404, Tarehe ya kupitiwa makala: Julai 1, 1404.
- Habar Diplomasi-64/4190977-Tahmil Atesh Bas Ba Bisharat Fat-h « Tahmil Atesh Bas Ba Bisharat Fat-h», Ulimwengu wa Uchumi, Tarehe ya kuwekwa makala: Julai 24, 1404, Tarehe ya kupitiwa makala: Julai 1, 1404.
- «Riwayat Jadad Az Pahpad Ke Sardod Suleiman Ra Hadaf Girift»، ISNA, Tarehe ya kuwekwa makala: Januari 28, 2020, Tarehe ya kupitiwa makala: Julai 1, 2025.
- «Intiqam Sakhte Ba Shalik Dahe Moshaq Be Peyghah Ameika Aunu al-Asad»،Shirika la Habari la IRNA, Tarehe ya kuwekwa makala: Januari 8, 2019, Tarehe ya kupitiwa makala: Julai 1, 2025.
- «Tahmil Atesh Bas Be Dushman Suhyuni, Dar Pi Amaliyat Muwafaq Bisharat Fat-h»،Shirika la Habari la Mehr, Tarehe ya kuwekwa makala, 1404, Tarehe ya kupitiwa makala: Julai 1, 1404.