Hammalat al-Hatab

Kutoka wikishia

Hammalat al-Hatab (Kiarabu: حَمّالَةُ الْحَطَب) ina maana ya mchukuzi wa kuni (mtu aliyebeba kuni mabegani). Qur’ani tukufu imempatia mke wa Abu Lahab[1] sifa hii. Mke wa Abu Lahab ni dada wa Abu Sufiyan na shangazi yake Muawiyya.[2] Kuniya yake ni Ummu Jamil na jina lake ni Arwa, Jamila[3] na Sakhra.[4]

wasifu huu unapatikana katika Surat al-Masad. [5] Hii kwamba, kwa nini Qur’an imetumia wasifu huu kuna nukta kadhaa zilizotajwa:

  • Ummu Jamil alikuwa akikusanya miba kutoka jangwani na kuibeba na alikuwa akiweka katika njia anayopita ili kumuudhi.[5]
  • Ummu Jamil kutokana na mambo aliyokuwa akiyafanya alikuwa akijiandalia moto wa jahannamu na kuni zake.[6]
  • Alikuwa akimdhihaki Mtume (s.a.w.w) kwa kuwa fakiri na Mwenyezi Mungu pia akamdhalilisha kwa wasifu huu.[7]
  • Maneno haya ni kinaya ya umbea na ufitinishaji wake.[8]

Imekuja katika tafsiri ya Nemooneh kwamba, hilo halikinzani na inawezekana yote hayo kutambuliwa kuwa yamekusudiwa katika Aya hii.[9]

Rejea

  1. Makārim Shīrāzī, Tafsīr-i nimūna, juz. 27, uk. 420.
  2. Ibn ʿAbd al-Barr, al-Istīʿāb,
  3. Ṭūsī, al-Amālī, uk. 265.
  4. Maybudī, Diwān-i Amīr al-Muʾminīn (a.s), uk. 92.
  5. Ṭabrisī, Majmaʿ al-bayān, juz. 10, uk. 852.
  6. Motahhari, Majmūʿa-yi āthār, juz. 28, uk. 852.
  7. Fakhr al-Rāzī, Mafātīḥ al-ghayb, juz. 32, uk. 353.
  8. Ṭūsī, al-Tibyān, juz. 10, uk. 428.
  9. Makārim Shīrāzī, Tafsīr-i nimūna, juz. 27, uk. 421.

Vyanzo

  • Fakhr al-Rāzī, Muḥammad b. al-ʿUmar al-. Mafātīḥ al-ghayb. 3rd edition. Beirut: Dār Iḥyāʾ al-Turāth al-ʿArabī, 1420 AH.
  • Ibn ʿAbd al-Barr, Yūsuf b. ʿAbd Allāh. Al-Istīʿāb fī maʿrifat al-aṣḥāb. Edited by ʿAlī Muḥammad al-Bajāwī. Beirut: Dār al-Jail, 1412 AH.
  • Motahhari, Morteza. Majmūʿa-yi āthār. Qom: Intishārāt-i Ṣadrā, 1389 Sh.
  • Makārim Shīrāzī, Nāṣir. Tafsīr-i nimūna. 1st edition. Tehran: Dār al-Kutub al-Islāmīyya, 1374 Sh.
  • Maybudī, Ḥusayn b. Muʿīn al-Dīn. Diwān-i Amīr al-Muʾminīn (a). Translated to Farsi by Muṣṭafa Zamānī. 1st edition. Qom: Dār al-Nidā al-Islām li-Nashr, 1411 AH.
  • Ṭabrisī, Faḍl b. al-Ḥasan al-. Majmaʿ al-bayān fī tafsīr al-Qurʾān. 3rd edition. Introduced by Muḥammad Jawād Balāghī. Tehran: Naṣir Khusruw, 1372 Sh.
  • Ṭūsī, Muḥammad b. al-Ḥasan al-. Al-Amālī. 1st edition. Qom: Dār al-Thiqāfa, 1414 AH.
  • Ṭūsī, Muḥammad b. al-Ḥasan al-. Al-Tibyān fī tafsīr al-Qurʾān. Edited by Aḥmad Qaṣīr al-ʿĀmilī. Beirut: Dār Iḥyāʾ al-Turāth al-ʿArabī, [n.d].