Abdallah bin Abi Husayn al-Azdi

Kutoka wikishia
Abdallah huyu ni tofauti na Abdallah bin Abi Husayn al-Azdi Bajali

Abdallah bin Abi Husayn al-Azdi (Kiarabu: عبد الله بن أبي الحصين الأزدي) (alikufa shahidi mwaka 37 Hijria), ni mmoja wa masahaba wa Imamu Ali (a.s) na ni katika mashahidi wa vita vya Siffin. [1]

Katika vita vya Siffin, wakati jeshi la Imam Ali (a.s) lilipokuwa likivuka daraja huko Raqqa, kofia za Abdullah bin Abi Husayn Azdi na Abdullah bin Hajjaj Azdi zilianguka kutokana na msongamano wa umati wa watu. Wawili hao walishuka na kuchukua kofia zao. Abdullah bin Hajjaj Azdi alimwambia Abdullah bin Abi Husayn:

«Ikiwa dhana ya watabiri ni sahihi, basi hivi karibuni nitauawa, na wewe pia utauawa». Abdullah bin Abi Husayn akasema: «Sipendi chochote zaidi ya ulichosema». [2]

Abdullah bin Abi Husayn alikuwa mmoja wa Maqarii (wasomaji Qur'ani) waliokwenda katika medani pamoja na Ammar bin Yasir na akauawa. [3] Kabla ya kuondoka kwenda katika medani, Mikhnaf bin Sulaym alimwambia: Sisi tunakuhitaji zaidi ya Ammar, lakini alikataa na akaenda pamoja na Ammar na akauawa. [4]

Rejea

Vyanzo