Uimamu katika hali ya utotoni

Kutoka wikishia

Uimamu katika hali ya utotoni (Kiarabu:الإمامة في الصغر) humaanisha uongozi wa mtu fulani ambaye bado hajafikia ukomavu wa ‎kisheria. Kwa imani ya Shia, Imamu Jawaad (a.s), Hadi (a.s) na Mahdi (a.s), ni miongoni mwa Maimamu ‎‎12 wa Shia ambao walifikia cheo cha uongozi (Uimamu) hali wakiwa na umri kati ya miaka 5 hadi 8. ‎Mashia Imamiyyah wanaamini kuwa; Uimamu ni nafasi takatifu ambayo ukomavu sio sharti ya kufikia ‎cheo nafasi hiyo.‎

Wafuasi wa Shia hujibu wapinzani wa imani yao hiyo kwa kutumia Aya za Qur'an zinazo zungumzia ‎utume wa Nabii Suleiman, Nabii Yahya (a.s) na Nabii Isa (a.s) wakiwa utotoni. Hoja nyengine ‎zitumiwazo kama ni vielelezo vya kuthibitisha imani ni; Uwezo wa kielimu wa Maimamu wakiwa bado ‎wamo katika maisha ya utotoni pamoja na uteuzi wa Imam Ali (a.s) kama ni mrithi wa bwana Mtume ‎‎(s.a.w.w) katika tukio la Yaumu al-Dar hali akiwa na umri mdogo.‎

Pia, kuna maandiko yaliyo andikwa kwa ajili ya kufafanua imani ya Shia kuhusiana na iamani ya uongozi ‎wa utotoni na kujibu pingamizi za wapinzani wa imani hiyo.‎

Umuhimu wa Suala Hili katika Imani ya Imamiyyah

Uongozi wa utotoni bila kufikia ukomavu wa kimwili na kisheria, ni mojawapo ya masuala muhimu ‎yanayo husiana na Uimamu, yanayo jadiliwa katika vitabu vya theolojia. [1] Tafit za mjadala huu ‎zinahusiana zaidi na kujibu pingamizi za wapinzani wa Shia juu ya imamani ya uongozi wa baadhi ya ‎Maimamu wa Shia (Imamu Jawad (a), Imamu Hadi (a), na Imam Mahdi (a)) ambao walipata uongozi ‎kati ya umri wa miaka 5 hadi 8. [2] Suala hili lilisababisha shaka na wasi wasi kwa baadhi ya wafuasi wa ‎Shia katika kuukubali uongozi wa Imamu Jawad (a.s), kwani hadi wakati huo, watu walikuwa waiamini ‎kwamba; moja ya masharti ya mtu kushika na nafasi hiyo, ni kuwa na ukomavu wa kisheria ‎‎(kubaleghe). [3] ‎

Kwa mtazamo wa wanazuoni wa Ahlu-Sunna, ukomavu ni mojawapo ya masharti muhimu ya uongozi. ‎‎[4] Hata hivyo, wanazuoni wa Shia wanaamini kwamba; Uimamu ni nafasi ya Kiungu ambayo Mwenye ‎Ezi Mungu humpa nafasi hiyo mtu maalumu mwenye sifa zinazostahili kushia cheo hicho. [5] Mashia ‎Wanaamini kuwa; isma (kutokosea), kuwa na sifa ubora, na kuwepo kwa maandiko ya wazi, ndio ‎masharti muhimu kwa ajili ya cheo cha Uimamu. [6] Imani ya Shia Imamiyyah isemayo kwamba; ‎ukomavu sio sharti kwa Imamu, imezua pingamizi kadhaa kutoka kwa wapinzani wao, jambo amabalo ‎lililazimisha wanateolojia wa Kishia kusimama na kutoa majibu dhidi ya wapinzai hao. [7]‎

Ibnu Taymiyyah (aliye fariki dunia mnamo mwaka 728 Hijria), Ibn Hajar al-Haytami (aliye fariki mnamo ‎mwaka 974 Hijria), na Ahmad al-Katib, ni miongoni mwa waliotoa pingamizi kuhusiana na imani ya ‎uongozi wa utotoni. [8] Baadhi ya sababu walizotoa kuhusiana na maoni yao ya kwa nini uongozi wa ‎mtoto si wa kimantiki, wamesema kwamba; Mtoto yatima huwa chini ya uangalizi wa watu maalumu, ‎‎[9] hali ya mtoto ya kutokuwa na uwezo au haki ya kufanya maamuzi, [10] kutokuwa na mamlaka, ‎kutokuwa na wajibu wa kidini, [11] na kutokuwepo kipindi na nafasi ya kujifunza. [12]‎

Maimamu Waliofikia Uongozi Wakiwa Watoto

  • Imamu Jawad (a.s): Alipata uongozi akiwa na umri wa takriban miaka minane. [13] Kwa mujibu ‎wa Hassan bin Musa Nawbakhti (aliyeaga dunia mano mwaka 310 Hijria), ni kwamba; Wakati ‎wa kifo cha Imamu Ridha (a.s) umri mdogo wa Imamu Jawad (a.s) ulisababisha kutoelewana ‎miongoni mwa wafuasi wa Shia, [14] na baadhi yao hawakukubaliana katu na wa mtoto huyo. ‎‎[15]‎
  • Imamu Hadi (a.s): Alipata nafasi ya uongozi akiwa na umri wa miaka minane. [16] Kwa mujibu ‎wa mtafiti wa kihistoria wa Kiiraqi, Jassim Hussein, kwa sababu suala la Uimamu wa utotoni ‎lilikuwa lilikuwa tayari limesha eleweka wakati wa Imamu Jawad (a.s), hilo lilipelekea uongozi ‎wa Imamu Hadi (a.s) kukubalika bila pingamizi. [17]‎
  • Imamu Mahdi (a.s): Alifikia uongozi akiwa na umri wa miaka mitano. [18] Inasemekana kuwa ‎kufikia uongozi kwa Imamu Jawad (a.s) na Imamu Hadi (a.s) wakiwa watoto kulisahilisha na ‎kuwaandaa wafuasi wa Shia kukubaliana na uongozi wa Imamu Mahdi (a.s) hali akiwa na umri ‎mdogo. [19]‎

Hoja za Wafuasi wa Shia Katika Kuutetea Uongozi wa Utotoni

Wanateolojia wa madhehebu ya Imamiyyah wakisimamisha hoja zao wamesme kwamba; ukamilifu wa ‎akili hauhusiani kabisa na ukomavu wa kimwili, na kama uongozi wa mtu utakuwa umetibitishwa kwa ‎ushahidi wa yakinifu kabisa, basi kiotomatiki sifa ya isma (kutokosea) na elimu ya Kiungu itathibiti kwa ‎mtu huyo, na umri wa Imamu hauna athari wala uhusiano wowote ule katika suala hilo. Pia, vizuizi ‎ambavyo sharia imeweka kwa ajili ya umri wa utotoni vinahusiana na wanadamu wa kawaida ambao ‎hukua kiakili na kielimu kwa kadri wanavyo endelea kukua, na sio kwa Imamu maasumu ambaye ana ‎elimu asilia kutoka kwa Mungu (elimu laduni). [20]‎

Uwezo wa Kielimu wa Maimamu Wakiwa Watoto

Kama ilivyosimuliwa na Sheikh Mufid kutoka katika moja ya Riwaya ya kwamba; Imamu Jawad akiwa ‎bado ni kijan mdogo, alishiriki katika mjadala na Yahya bin Aktham na kujibu swali la Yahya kwa namna ‎iliyowashangaza waliokuwepo katika mjadala huo. [21] Kafuatia tukio hili la kushangaza, Mamun ‎alisema kuwaambia waliomzunguka ya kwamba; utoto wa Imamu Jawad (a.s) si kigezo cha upungufu ‎wa elimu na akili yake. [22]‎

Kwa mujibu wa maelezo ya Sheikh Mufid (aliye fariki dunia mnamo mwaka 413 Hijria), ni kwamba; ‎tukio la kushiriki kwa Hassan na Hussein (a.s) katika tukio la Mubahala kati Mtume (s.a.w.w) na ‎Wakristo wa Najran linaonyesha kwamba, hata mtu akiwa ni mtoto, pia naye anaweza kuwa na ‎majukumu makubwa ya Kiungu katika jamii. [23] Hata, imani ya Imamu Ali (a.s) ya kumuamini bwana ‎Mtume (s.a.w.w) alikiwa bado ni kijana mdogo, inaonyesha uwezekano wa mtoto kuwa na uelewa na ‎akili ya juu kuliko wengine. [25]‎

Rejeleo la Utume wa Suleimani, Yahya na Isa (a.s) Hali Wakiwa ni Watoto

Mashia wametaja baadhi ya aya za Qur'an zinazozungumzia utume wa manabii fulani waliopata utume ‎hali wakiwa ni watoto. Wao wametumia Aya hizo kama ni vielelezo katika kuthibitisha mamlaka ya ‎uongozi wa utotoni. [26] Kwa mujibu wa maelezo ya Fakhru al-Din al-Razi, ni kwamba; Hukmu iliyo ‎tajwa katika Aya ya 12 ya Suratu Mariam, ambayo Mwenye Ezi Mungu alimpa Nabi Isa na Yahya (a.s) ‎wakiwa bado ni wadogo, ni “hukmu” ya Utume. Vile vile, Ja'far Subhani, mwanatheolojia wa Shia, ‎anasema kwamba; Aya ya 30 ya Suratu Mariam, inayozungumzia matamshi na maneno ya utotoni ya ‎Nabi Isa (a.s), yaonesha kwamba, kama Mwenye Ezi Mungu atapenda, bila shaka anaweza kumpa mtu ‎elimu, akili, na hekima maalumu zinazohitajika kwa ajili ya uongozi hali akiwa bado ni mtoto mdogo. ‎‎[28]‎

Imesimuliwa na kuelezwa ya kwamba; Imamu Ridha (a.s) alimtambulisha mwanawe (Jawad) kama ni ‎Imamu hali akiwa na umri wa miaka mitatu, alifanya hivyo huku akitolea mfano wa Nabii Isa (a.s), ili ‎kuonesha kwamba, uongozi wa utotoni si jambo la muhali bali ni kitu kinacho wezekana. [29] Pia, ‎Imamu Jawad (a.s) katika Hadithi nyingine alitaja kisa cha Nabi Suleimani (a.s) kuwa mrithi wa Nabii ‎Daud (a.s) hali akiwa bado ni mtoto mdogo, alifanya hivyo ili kuonesha kuwa jambo hilo linawezekana. ‎‎[30]‎

Rejeleo la Kitendo cha Mtume (s.a.w.w) cha Hadithi ya Yaumu al-Dar

Kwa mujibu wa maelezo ya Sheikh Mufid, mwanatheolojia wa Shia, ni kwamba; Kitendo cha bwana ‎Mtume (s.a.w.w) katika Hadithi ya Yaumu al-Dar kinaonesha ya kwamba, iwapo Mungu akitaka, basi ‎yuwaweza kumfanya mtoto kuwa hoja yake (mjumbe wake) kwa ajili ya waja wake. [31] Kwa mujibu ‎wa makubaliano kati ya Shia na Sunni, ni kwamba; Katika Yaumu al-Dar, bwana Mtume (s.a.w.w) ‎alimteua Imamu Ali (a.s), ambaye bado hakuwa amefikia ukomavu wa kimwili, kama ni mrithi na khalifa ‎wake anaye stahiki kushika nafasi yake baada yake. [32]‎

Bibliografia (Vitabu Vilivyoandikwa Kuhusu Uongozi katika Umri wa Utotoni)‎

Kitabu cha Uimamu katika hali ya utoto, kilichoandikwa na Ali Asghar Rizvani

Kuna vitabu kadhaa vilivyoandikwa juu ya suala la uongozi katika umri wa utotoni, miongoni mwavyo ‎ni:‎

  • Kitabu "Imamaamat Dar Sinne Kuudakiy / Uimamu katika Umri wa Utotoni" kilichoandikwa na Ali-‎Asghar Ridhwani, kikiwa na kurasa 48, kitabu hichi kilichapishwa mwaka 1385 Hijria Shamsia (2006) na ‎Shirika la Uchapishaji la Msikiti Mtakatifu wa Jamkaran. [33]‎
  • Kitabu "Setaaregane Hidaayat: Imaamat Dar Kuudakiy / Nyota za Uongozi: Uongozi wa Utotoni", ‎kilichoandikwa na Mohammad Baamiri, kikiwa na kurasa 176, hichi ni kitabu kilicho chapishwa mwaka ‎‎1391 Hijria Shamsia (2012) na Shirika la Uchapishaji la A-imma. [34]‎
  • Kitabu "Imaamat Dar Kuudakiy / Uimamu katika zama za Utotoni: Mwelekeo wa Kichambuzi juu ya ‎Uongozi katika Utotoni," kilichoandikwa na Hadi Turkmani, kikiwa na kurasa 166, ambacho ‎kilichapishwa mwaka 1402 Hijria Shamsi (2023) na Shirika la Uchapishaji la Daa'iyah. [35]‎

Rejea

Vyanzo