Mtumiaji:TawakkalMS8/3
سَأَلَنِي أَبُو قُرَّةَ الْمُحَدِّثُ صَاحِبُ شُبْرُمَةَ- أَنْ أُدْخِلَهُ عَلَى أَبِي الْحَسَنِ الرِّضَا ع فَاسْتَأْذَنَهُ فَأَذِنَ لَهُ فَدَخَلَ فَسَأَلَهُ عَنْ أَشْيَاءَ مِنَ الْحَلَالِ وَ الْحَرَامِ وَ الْفَرَائِضِ وَ الْأَحْكَامِ حَتَّى بَلَغَ سُؤَالُهُ إِلَى التَّوْحِيدِ فَقَالَ لَهُ أَخْبِرْنِي جَعَلَنِيَ اللَّهُ فِدَاكَ عَنْ كَلَامِ اللَّهِ لِمُوسَى
Safwan bin Yahya anasema kwamba Abu Qurra, mtaalamu fani ya Hadithi na rafiki wa Shubruma, alimuomba kupanga mipango ya kukutana na Imamu Ridha (a.s). Safwan akakubaliana na ombi hilo na akamwomba ruhusa Imamu Ridha (a.s) ili amkaribishe nyumabi kwake. Abu Qurra akatumia fursa hiyo na akafika mbele ya Imamu Ridha (a.s). Abu Qurra alipofika alianza kumuuliza Imamu Ridha (a.s) maswali kuhusiana na masuala ya halali na haramu, hukumu za faradhi mbali mbali, na hukumu za kifiq-hi. Baada ya kumaliza maswali hayo, alielekeza maswali yake kwenye uwanja wa masuala ya Tawhid. Alimuuliza Imamu akimwambia: "Ewe bwana wangu roho yangu iwe ni fidia kwako, tafadhali nieleze jinsi Mungu alivyomzungumza na Musa."