Nenda kwa yaliyomo

Khasifun-Na'al (Lakabu)

Kutoka wikishia

Khasifu Al-Na’al (Kiarabu: خاصِفُ النَّعْل) (Mkarabati Viatu au Mfungafunga Viatu), ni moja ya lakabu za Imam Ali (a.s), ambaye ni Imamu wa kwanza wa Waislamu wa madhehebu ya Shia ulimwenguni.[1] Lakabu hii imetokana na Hadithi inazojulikana kwa jina la Hadithi ya Khasifun-Na’al, ambayo kwa mujibu wake; Mtume Muhammad (s.a.w.w) ndiye aliyemwita Imamu Ali (a.s) kwa jina hili, jina ambalo alipewa pale alikuwa akirekebisha na kufungafunga au kutia viraka viatu vya bwana Mtume (s.a.w.w).[2]

Neno khasafa linamaanisha kukusanya au kuunganisha pamoja vitu fulani.[3] Na yule mtu anayekusanya vipande vya viatu na kuvirekebisha ili viungane na kurejea katika hali yake ya awali, huitwa Khasifun-Na’al.[4] Kile kitendo cha Imamu Ali (a.s) cha kurekebisha na kutia viraka viatu vya bwana Mtume (s.a.w.w), kimeonekana kuwa ni miongoni mwa ishara za unyenyekevu wake,[5] na ni kielelezo kinachoashiria hali ya maisha ya kawaida aliyokuwa akiishi Imamu Ali (a.s).[6]

Kila moja miongoni mwa Hadithi za bwana Mtume (s.a.w.w), zinazomtaja Imam Ali (a.s) kwa lakabu ya Khasifun-Na’l, zinaonekana kumsifu Imamu Ali (a.s) kwa mbalimbali. Miongoni mwa sifa zake (a.s) alizosifiwa ndani ya Hadithi hizo, ni pamoja na sifa ya uongozi wake (Uimamu) na ukhalifa wake, pamoja na vita alivyopigana dhidi ya washirikina na madhalimu mbali mbali.[7] Hadithi hizi zinapatikana katika vyanzo vya awali vya hadithi za upande wa madhehebu ya Kishia, vikiwemo vitabu vinavyojulikana kwa jina la Al-Kutub Al-Arba’a.[8] Pia Hadithi hizi zinapatika katika vitabu maarufu vya Hadithi za upande wa madhehebu ya Kisunni, kama vile; Sihah Al-Sitta,[9] Musnad bin Hanbal,[10] na Sunan Annasaai.[11] Wanazuoni wa Hadithi kutoka madhehebu ya Kishia pamoja na Kisunni, wanakubalia na usahihi wa baadhi ya Hadithi hizi na huzizingatia Hadithi hizo kuwa ni miongoni mwa Hadithi zenye kuaminika.[12] Baadhi ya wanazuoni wa madhehebu ya Shia, kama vile; Sharafuddin na Kaashifu Al-Ghita, wanasema kuwa: Hadithi hizi ni zenye sifa ya mapokezi yenye kiwango cha mutawatir (yaani, zimepokewa kwa wingi kupitia matabaka mbali mbali ya wapokezi wa Hadithi).[13]

Moja ya hadithi hizo, ambayo ianpatikana katika vitabu vya Hadithi za Kishia pamoja na Kisunni, ambayo inaeleza ya kwamba; Bwana Mtume (s.a.w.w) alimwita Imamu Ali (a.s) kwa lakabu ya Khasifun-Na’l, ni ile Hadithi iliyokuja ikisema kwamba: Pale bwana Mtume (s.a.w.w) alipokuwa katika mkusanyiko wa masahaba zake, alisema: «إِنَّ مِنْکمْ مَنْ یقَاتِلُ عَلَی تَأْوِیلِ هَذَا الْقُرْآنِ کمَا قَاتَلْتُ عَلَی تَنْزِیله ; Hakika miongoni mwenu, kuna mmoja atakayepigana kwa ajili ya kufasiri Qur’ani hii (kwa ajili ya kufikisha tafsiri sahihi ya Qur’ani), kama nilivyopigana kwa ajili ya kushushwa kwake (kwa ajili ya kuufikisha ujumbe ulioshushwa na Qur’ani)». Baadhi ya waliokuwepo wakamuuliza kama jee wao ndio mtu huyo aliyetajwa na bwana Mtume (s.a.w.w). Baada ya bwana Mtume (s.a.w.w) kwapa jawabu hasi juu ya swali lao, aliwatambulisha mtu huyo kwao, akiwaambia kuwa; Mtu huyo ni yule aliyekuwa akimshonea au akimtilia viraka viatu vyake (s.a.w.w). Wakati huo, Imam Ali (a.s) alikuwa akiungaunga viatu vya bwana Mtume (a.s).[14]

Rejea

  1. Sibt ibn Jawzi, Tadhkirat al-Khawas, 1418 AH, uk. 16; Muqaddas Ardabili, Hadiqat al-Shi'a, 2004, juz. 1, uk. 16; Shi'i Sabziwari, Ra'hat al-Arwah, 1999, uk. 86.
  2. Bahrani, Ghayat al-Maram, 1422 AH, juz. 6, uk. 285; Arbali, Kashf al-Ghamma, 1381 AH, juz. 1, uk. 335; Allama Hilli, Nahjul-Haq, 1982, uk. 220, Ibn Shahr-Ashub Mazandarani, Manaqib Aal Abi Talib (a.s), 1379 AH, juz. 3, uk. 44.
  3. Ibn Mandhur, Lisan al-Arab, Beirut, juz. 9, uk. 71.
  4. Tabataba'i, Al-Mizan, 1417 AH, juz. 8, uk. 35.
  5. Atiyeh, Ali (a.s), Khasifu Al-Na’al al-Nabii (s.a.w.w), 1436 AH, uk. 13.
  6. Makarim Shirazi, Payam Imamu Amir al-Mu'minin (a.s), 1385 AH, juz. 2, uk. 303.
  7. Bahrani, Ghayat al-Maram, 1422 AH, juz. 6, uk. 285; Arbali, Kashf al-Ghamma, 1381 AH, juz. 1, uk. 335; Allama Hilli, Nahjul-Haq, 1982, uk. 220, Ibn Shahr-Ashub Mazandarani, Manaqib Aal Abi Talib (a.s), 1379 AH, juz. 3, uk. 44.
  8. Kulayni, Al-Kafi, 1407 AH, juz. 5, uk. 11-12; Sheikh Tusi, Tahdhib al-Ahkam, 1407 AH, juz. 4, uk. 116.
  9. Tirmidhi, Sunan Tirmidhi, 1419, juz. 5, uk. 452.
  10. Ibn Hambal, Musnad al-Imam Ahmad bin Hambal, 1416 AH, juz. 17, uk. 391.
  11. Nasa'i, Sunan al-Nasa'i, 1411 AH, juz. 5, uk. 127-128.
  12. Tazama: Tirmidhi, Sunan Tirmidhi, 1419, juz. 5, uk. 452; Muqaddas Ardabili, Hadiqa al-Shi'a, 2004, juz. 1, uk. 232.
  13. Sharaf al-Din, al-Murajaat, 1426 AH, uk. 319; Kashif al-Ghitaa, Kashf al-Ghitaa, 1422 AH, juz. 1, uk. 37.
  14. Ibn Hambal, Musnad al-Imam Ahmad bin Hambal, 1416 AH, juz. 17, uk. 391, juz. 18, uk. 296. Kwa tofauti ndogo katika: Sheikh Mufid, Al-Ifsah Fi al-Imamah, 1413 AH, uk. 135; Tabari, Al-Mustarishd Fi Imamat Ali ibn Abi Talib (a.s), 1415 AH, uk. 357; Sayyid Ibn Tawus, al-Taraif, 1400 AH, juz. 1, uk. 70.

Vyanzo

  • Ibn Hambal, Ahmad bin Muhammad, Musnad al-Imam Ahmad bin Hambal, Beirut, Muasasat al-Risala, 1416 AH.
  • Ibn Shahrashub Mazandarani, Muhammad bin Ali, Manaqab Aali Abi Talib (a.s), Qom, Allamah, 1990 AH.
  • Ibn Mandhur, Muhammad ibn Makram, Lisan al-Arab, Beirut, Dar Sadir, Chapa ya Tatu, Bita.
  • Arbali, Ali ibn Issa, Kashf al-Ghumma Fi Maarifat al-Aimah, Tabriz, Bani Hashimi, 1381 S.
  • Bahrani, Sayyid Hashim, Ghayat al-Maram na Hajj al-Khassam Fi Taayiin al-Imam Min Tariq al-Khassa wa al-Aam, Beirut, Muasasat Tarikh al-Arab, 1422q.
  • Tirmidhi, Muhammad bin Issa, Al-Jaami' al-Sahih wa Huwa Sunan al-Tirmidhi, Cairo, Dar al-Hadith, 1419 AH.
  • Sibt ibn Jawzi, Yusuf bin Qazaughli, Tadhkirat al-Khawas Min Umma Fi Dhikr Khasais al-Aimah, Qom, Manshurat al-Sharif al-Ridha, 1418 AH.
  • Sayyid bin Tawaus Hasna, Ali bin Musa, Al-Tara'if Fi Maarifat Madhhab al-Tawaif, Qom, Khayyam, 1400 AH.
  • Sharafuddin, Sayyid Abdul-Hussein, Al-Murajaat, Qom, Al-Majmau al-Alami Li Ahlul-Bayt, Chapa ya Pili, 1426 AH.
  • Sheikh Tusi, Muhammad bin al-Hassan, Tahdhib al-Ahkam, Tahqiq Khurasan, Tehran, Dar al-Kutb al-Islamiyah, Chapa ya Nne, 1407 AH.
  • Sheikh Mufid, Muhammad bin Muhammad bin Nu'man, Al-Ifsah Fi al-Imamah, Qom, Al-Mutammar al-Alami Li Sheikh al-Mufid, 1413 AH.
  • Shi'i Sabziwari, Abu Said, Ra'hat al-Arwah, Tehran, Mirath Maktub, Chapa ya Pili, 1378 S.
  • Tabatabai, Sayyid Muhammad Hussein, Tafsir al-Mizan, Qom, Ja'mia Madrasein, 1417 AH.
  • Tabari, Muhammad bin Jarir ibn Rustam, Al-Mustarshid Fi Imamat Amir al-Mu'minin (a.s), Qom, Muasasat al-Wasif, 1415 AH.
  • Atiyeh, Majid bin Ahmad, Ali (a.s) Khasif, Ali (a.s) Khasif al-Na'al al-Nabii (s.a.w.w), Karbala, Al-Atabah al-Husseiniyah, 1436 AH,
  • Allamah Hilli, Hassan bin Yusuf, Nahj al-Haq wa Kashf al-Sadaq, Beirut, Dar al-Kitab al-Lubnan, 1982.
  • Ka'shif al-Ghita'a, Sheikh Ja'far, Kashf al-Ghita'a Min Mubhamat al-Shari'a al-Ghara'a, Qom, Intisharat Daftar Tablighat Islami Hawze Ilmi Qom, 1422 AH.
  • Kuleini, Muhammad bin Ya'qub ibn Is-haq, Al-Kafi, Tehran, Dar al-Kitub al-Islamiyyah, Chapa ya Nne, 1407 AH.
  • Maqadas Ardabili, Ahmad ibn Muhammad, Hadiqat al-Shi'a, Qom, Intisharat Ansarian, Chapa ya Tatu, 1385 S.
  • Makarim Shirazi, Payam Imamu Amir al-Mu'minin (a.s), Tehran, Dar al-Kutub al-Islamiyyah, 1385 S.
  • Nisa'i, Ahmad ibn Ali, Al-Sunnah al-Kabri, Beirut, Dar al-Kutub al-Ilmiyah, Manshurat Muhammad Ali Baidhun, 1411 AH.