Nenda kwa yaliyomo

Israeli (Lakabu)

Kutoka wikishia
Usichanganywe na utawala wa Israel.

Israeli (Kiarabu: إسرائيل) ni lakabu ya Nabii Yaqub au Yakobo. Kulingana na kitabu cha tafsiri ya Majma‘u al-Bayan, neno Israeli katika lugha ya Kiebrania humaanisha Mteule wa Mungu au Mtumishi wa Mungu.[1] Sheikh Tusi maana ya jina hili, anasema kwamba; «Israeli' limeundwa kunatokana na maneno mawili; la kwanza ni Isra, ambalo linamaanisha mtumishi, na la pili ni «Il», linalomaanisha Mwenye Ezi Mungu, na hivyo «Israeli» likawa na maana ya Mtumishi wa Mungu.[2] Kulingana na wafasiri wa Kishia, neno 'Israeli' lililopo katika Aya ya 93 ya Surat Al-Imran, na Aya ya 58 ya Surat Maryam, linamhusiana moja kwa moja na Yakobo au Yaqub.[3] Hii ndiyo sababu hasa ya wana wa nabii Yakobo au Yaqub na vizazi vyake kumepewa jina la Bani Israeli katika Qur’ani.[4]

KatikaTaurati kuna kisa kinachoeleza kwamba; Moja kati ya nyusiku (wingi neno usiku), Mwenye Ezi Mungu alishindana na Yakobo kwa kupigana naye mieleka, na baada ya Mwenyezi Mungu kushindwa na kudhibitiwa na nabi 'Yakobo/Yaaquub', alimwambia nabi huyo kwa kusema: 'Niachilie, kwa kuwa tayayari usiku umeshaanza kupambazuka,' Hapo Yakobo au Yaqub akajibu: 'Sitakuachilia hadi unibariki.' Mwenye Ezi Mungu akamwuliza: Jina lako ni nani? Naye akajibu: Yakobo au Yaqub, Mwenye Ezi Mungu akamwambia: Kuanzia sasa hvi jina lako si Yakobo au Yaqub, bali utajulikana kwa jina la Israeli, kwa sababu umeonyesha nguvu zako dhidi ya Mungu pamoja na binadamu na hatimae ukawashinda.[5]

Rejea

  1. Tabarsi, Majma' al-Bayan, juz. 1, uk. 182.
  2. Sheikh Tusi, Al-Tabiyan fi Tafsir al-Quran, Dar Ihya al-Turath al-Arabi, juz. 1, uk. 180.
  3. Tabarsi, Majma'u al-Bayan, 1415 AH, juz. 2, uk. 344; Subhani, Manshor Jawid, Muasase Imam Sadiq (a.s), Qom, juz. 11, uk. 325.
  4. Rouhi, «Kuonekana kwa Wana wa Israeli katika Quran na Maagano», 1384 S, uk. 58.
  5. Agano la Kale, 1393 S, juz. 1, uk. 234-236.

Vyanzo

  • Rouhi, Abulfadhl, «Simayi Bani Israil Dar Qur'an wa Ahdein», katika Jarida la Marafat, Na. 95, Aban 1384 S.
  • Subhani, Jafar, Manshor Jawid, Qom, Muasase Imam Sadiq (a.s), 1390 S.
  • Sheikh Tusi, Muhammad ibn Hassan, Al-Tabiyan fi Tafsir al-Qur'an, Beirut, Dar Ihya al-Turath al-Arab, Beta.
  • Tabarsi, Fadhl ibn Hassan, Majma’ al-Bayan fi Qur’an, Beirut, Muasasat al-Aala Lil-Matbuat, 1415 AH.
  • Agano la Kale (juz. 1: Books of the Law or Torah), iliyotafsiriwa na Pirouz Sayar, Tehran, Nashr Hermes, 1393 S.