Mwanzo

Karibu
Ensaiklopidia ya Maktaba Ahlul Bayt (a.s.), inayosimamiwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s.)
Kuna makala 322 za Kiswahili
Makala ya Wiki
Ziara ya Imam Husein (a.s) ni kutembelea kaburi la Imam Hussein (a.s), kutoa salamu kwa Imam na kusoma ziyara ya Imam Hussein (a.s) zilizoko katika vitabu mbalimbali.

Ziyara ya Imam Hussein (a.s) ni miongoni mwa matendo yenye fadhila nyingi sana Kwa Mashia. Wanazuoni wakishia wamenuku hadithi nyingi kuhusiana na thawabu zinazopatikana katika ziyara hii, Ikiwemo fadhila ambazo Mwenyezi Mungu amewapatia Wanaotembelea kaburi la Imam Hussein (a.s) na dua za Mtume (s.a.w) na maimamu kwa ajili yao. Inapendekezwa kufanya ziyara ya Imam Hussein (a.s) Kwa niaba ya mtu mwengine, na mtu ambae hawezi kufika katika kaburi hili tukufu anaweza kufanya ziyara hii Kwa kusoma ziyara ya Imam Hussein akiwa mbali.

Katika vitabu vya Hadithi kuna adabu nyingi sana ambazo zimesisitizwa Kwa mtu ambae anataka kumtembelea Imamu Husein (a.s). Miongoni mwa adabu hizo ni; Kumtambua Imamu Husein (a.s), kuoga/kufanya ghusli, kuvaa nguo safi, kumuomba Mwenyezi Mungu ruhusa ya kuingia kwenye kaburi la imam, na kusoma Ziyara ya imam hussein (a.s). Mnamo tarehe 20 safar ya Kila mwaka (Arbaini ya imam Hussein) wanazuoni mbalimbali kama vile Sheikh Morteza Ansari na Sheikh Jafar Kashif al-Ghitaa walikua wakitembea Kwa miguu kutoka mji wa najaf kuelekea kaburi la imam Hussein (a.s). Leo hii, matembezi ya Arbaeen ni mojawapo ya mila muhimu ya Mashia na mamilioni ya watu hushiriki katika hilo.

Soma zaidi...
Maeneo mengine ya Bunge la Dunia la Ahle Bayt
Picha Iliyoangaziwa
غدیر خم فرشچیان.jpeg
Picha ya Ghadir ya bwana Farshchian


Lugha